Ni ngumu sana kujua anachotaka computer mimi niliacha sooner baada ya kuona anaandika sana mazingaombwe. Ni sahihi kila mtu kua na mawazo yake ila kama kila mtu anakuambia mawazo yako ni miyeyusho take a step back yaangalie tena.
Week in week out
computerarsenal anachagua tu week hii nanung'unikia kikosi. Week ijayo kama tukishinda nanung'unikia kocha.
Muda mwingine naona anaandika komedi natamani kumjibu ila napita kushoto mfano nimeona komenti yake akisema Arsenal haivutii tena big players lakini mimi kwavile angalau nafuatilia mpira nilitaka kumuuliza kama anajua united imekataliwa na wachezaji wangapi mpaka wakaamua kununua wale watoto wakina Pellistr? Thiago alikataa kwenda united, Reguillon alikataa, wawili wengine wamenitoka.
Msimu huo huo Dest akagoma kujiunga Bayern akaenda Barcelona. Bayern hapo imetoka kuchukua uefa na imeipiga 8 barca dest akaenda kule kulikopigwa 8. Wijnaldum akagoma kwenda barca akaja kwenye hiyo timu yako mpya psg.
Huyu Renato amekaa anasubiri ofa kutoka Arsenal. Mchezaji anayesubiri hata salamu kutoka Arsenal ni Zaha, Tammy alitaka kuja Arsenal pia.
Kwani liva wachezaji unaowaona leo imewatoa timu gani? Anza na front three yao Mane Southampton, Salah reject wa chelsea akachukuliwa kutokea Roma hakuna mchezaji ambaye alikua on fire alitakiwa na timu zingine halafu liva ikamfuata.
Zaidi ya misimu 6 au 7 Arsenal anamaliza juu ya liva, Arsenal amemiss kucheza michuano ya ulaya msimu huu lakini kwa liva ilikua kawaida. Klopp anaanza kuifundisha liva ilikua ni vipigo defense inacheza kama maguire forward ya sturridge haina kitu.
Sasa
computerarsenal unatamani leo hii Arsenal labda iseme inamtaka Kimmich au Mbappe halafu wakubali kuja? Hiki ndiyo nimekisema unaandika mazingaombwe. Baada ya kujiestablish vizuri ndiyo Liva imeweza kumfuata mchezaji kama Thiago.
Mchezaji kama Dusan ni sahihi kwake kutamani kua sehemu ambayo itamfeed ego lakini Klopp alimuambia Coutinho "Baki Liva utakua supastaa ukienda Barca utakua ni mchezaji wa Barca" huu ushauri ilitakiwa aupate Jovic alipoamua kwenda Madrid n.k.
Umetoa hoja ya kwamba atafutwe kocha mzuri kumzidi Arteta. Taja majina. As in jamani Arteta ni kinabo achukuliwe fulani, ambacho haujui pia ni kwamba makocha wakubwa wanakuja na matakwa makubwa. Conte aliacha kazi Inter kwakua aliambiwa bajeti inakatwa na key players watauzwa.
Akaigomea kazi ya Spurs baada ya Levy kusema hana mpango wa kuinvest. Spurs ikamchukua Nuno, imempiga chini, imemrudia Conte. This means ama Levy yupo tayari kuongeza pesa au anataka kumtapeli Conte.
Hata Arsenal ikisema inamtaka kocha wa viwango unavyotaka wewe mahitaji yake yatamfanya asichukuliwe yaani Artet akiachwa kocha wa kuja pale aweza kua Rooney, Vieira hivi au kocha wa mid table kutoka ligi nyingine.
Unanung'unika sana huku haujui vitu vingi. Emotion ziko mbele mno. Nitaappreciate kama ukiamua kujibu useme kwamba 'Mkinionyesha kitu A, B, C kitawezekana vipi nitaacha hii tabia' siyo zile za 'Arsenal ana negative GD this is unbelieavable' huku unasahau kuangalia title contenders wawili spurs na united wana GD gani.
Man up grow a spine