Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Ufaransa inachukua kombe Giroud kafunga magoli mangapi?
 
Unaangaika kwingine wakati nyumbani kwako kunaungua
 
Kwani mkuu unadhani mimi ni rafiki au mnazi wa mmiliki?? Hapana mkuu nisieleweke vibaya. Simpendi kroenke, lakini nakataa kabisa asishushiwe lawama asizostahili.

Wasitokee washenzi wakajificha nyuma ya kivuli cha kwamba Kroenke ndio tatizo wakati wao ndio matatizo.

Hebu tumfuatilie William Saliba. Case yake tu ilitosha kutuonyesha Arteta ni mtu wa aina gani. Mtu ambae anajikuta tu ameshakuwa kiji-guardiola mdogo. Mpaka anavyovaa anajifananisha na Guardiola kumbe ni uharo mtupu. Sababu ya kumpiga exile Guendouzi kiukweli kabisa haina mashiko. Yaani unashangaa kabisa. Alilolifanya Guendouzi kwa maupay ndio alilolifanya Keown kwa Van Nestolrooy na Keown ni shujaa ila Guendouzi is regarded hana nidhamu. Stupid mentality, wapambanaji kuonekana hawana nidhamu, Genaro Gattuso angempenda Guendouzi to the moon and back because we need fighters in the team.

Arteta alivyomtreat Torreira inastaajabisha sana. Inastaajabisha kwa kweli mpaka unajiuliza ni nini haswa shida hapa?? Jibu ni kwamba arteta got it wrong on how a manager can establish authority. Bro mimi nipo katika field ya management na najua ninachoongea. Common mistakes ambazo managers wanafanya arteta amezofanya again and again tangu apewe ajira pale arsenal.

Twende kwenye issue ya Martinelli. With his work rate how in hell he doesn't start??? How?? Specifically game ya jana, kama issue ni match fitness kwanini asingeanza na saka beki ya kushoto ili martinelli acheze wing ya kushoto??? Jibu ni simple tu, Martinelli hakumsajili yeye na hivyo alitaka kulazimisha odergard acheze. Kama aliamua kucheza formation ya washambuliaji watatu maana yake ni wings mbili ili kukava spaces na forward mmoja ambae ni auba. Odergaard alikuwa hovyo kabisa Jana maana aliwekwa acheze wing.

Mkuu, sasa katika issue kama hizi tunamlaumu vipi kroenke???
 
Huu uzi unatakiwa kushushwa huko chin ..


Mods hizi timu zinazocheza Europa ,hazitakiwa ku pin nyuzi zao huku juu kwa wanaume was CL ..


Hii timu inatakiwa kushuka chini huko

Mkuu ivi nyuzi yenu ya man city ipo wapi?
 
Mimi mshabiki wa Liver ila ukisikia msiba kwa jirani lazima uende kushirikiana na wafiwa. poleni sana ila kwa ukweli team bado sana jana hata nilikuwa sijui wanacheza mfumo gani, mabeki kivyao, viungo kivyao na mbele kivyao unaona kabisa hakuna game plan ni kama walikuwa wanabahatisha tu. Mimi sidhani kama wachezaji wote wabovu inaweza kuwa wengine viwango vidogo lakini kwanini kocha asicheze 3-4-3 au 3-5-2 ili Lacazete na Aub wacheze mbele nadhani 3-5-2 better kwa wachezaji alionao sio kulazimisha 433 huna viungo wazuri. Mimi namlaumu kocha hii team nadhani Brendan akipewa na uhakika ataibadilisha.
 
Relief Mirzska at one point ulikua unasema Stan ametoa pesa kwaajili ya Arsenal, ilienda mpaka nikaja na references za kupingua ulichosema.

Stan alitrick mashabiki kuamini Wenger ni tatizo, same kwa Emery ila kwa Arteta inakua ngumu as hatimaye kila kitu kipo wazi. Majibu yao yameonyesha hawana mpango ni timu kuchukua trophies.

So when Arsenal secure trophies ni bahati mbaya hua haipo kwenye mipango.

Kuhusu Tierney, Saka, Xhaka, LB na Martinell kabla mechi haijaanza na nilipoona maelezo yake ndicho hata mimi nilisema.

Hiki kikosi kilifika fainali chini ya Emery, chini ya Ancelotti kingeshindwa? Ranieri? Arteta anatosha? Hapana. Na hili nililisema kwamba bado hatoshi na ndiyo sababu amekubali dili ya Arsenal ni makocha wachache wenye uzoefu na wakakubali kuishi kama Wenger.

So Arteta ni option kwakua tunakua pamoja, Arteta anakua professionally na Arsenal inajikusanya kuelekea njia sahihi.
 
Arsenal kaanza na 3 4 3 na hakuna muda kacheza 4 3 3. Baada ya 3 4 3 ikaja 4 1 4 1.

Lacazette ni majeruhi medical walisema anaweza kucheza kwa dakika 10 au 15 tu.
 
Arsenal kaanza na 3 4 3 na hakuna muda kacheza 4 3 3. Baada ya 3 4 3 ikaja 4 1 4 1.

Lacazette ni majeruhi medical walisema anaweza kucheza kwa dakika 10 au 15 tu.
Hakuna prof player anaenda katika game na kusema huyu mgonjwa anaweza kucheza dakika 10. Kama umepass fitness ina maana uko fit 100% hizi team huwezi kupanga mtu hayuko fit anaweza kukosa match fitness lakini sio kuwa 80% fit hapangwi. 343 hao 3 wa mbele ukitoa Pepe na Aub nani mwingine yule Mnorway. yule ni kiungo ningemwelewa kama unavyosema 343 mbele angekuwa Pepe, Aub na Martino. Nadhani tatizo kubwa ni kocha hakuna ID ya team.
 
Kuhusu hizo dakika 10 au 15 za Laca ni majibu ya kocha. Nimekujibu kwa kuhisi haujamsikia alichosema sasa tena unataka kuanzisha ubishi na mimi utafikiri mimi ndiye nimetoa majibu hii siyo fair.

Odegaard ni RW/ CAM so ni sawa tu alipopangwa.
 
Kuhusu hizo dakika 10 au 15 za Laca ni majibu ya kocha. Nimekujibu kwa kuhisi haujamsikia alichosema sasa tena unataka kuanzisha ubishi na mimi utafikiri mimi ndiye nimetoa majibu hii siyo fair.

Odegaard ni RW/ CAM so ni sawa tu alipopangwa.
Ndio maana nimesema tatizo ni kocha wala sio wachezaji. Nimesikia mara anasingizia Malaria. Kocha hafai watafute mtu anayeweza kujenga team na mfumo wa team ili kila mchezaji ajuwe hivi ndio Arsenal wanacheza.
 
Nyie Arsenyeto bado mmelala tu? Hamkeni bwana kumekucha..
 
Ndio maana nimesema tatizo ni kocha wala sio wachezaji. Nimesikia mara anasingizia Malaria. Kocha hafai watafute mtu anayeweza kujenga team na mfumo wa team ili kila mchezaji ajuwe hivi ndio Arsenal wanacheza.
Tatizo la arsenal sio kocha ngoja wamfukuze arafu wamlete mwingine bila kuinvest pesa ndio utajua tatizo sio kocha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…