Arteta bado anajifunza, arsenal walikosea sana kumchukua huyo jamaa!
ARTETA NDIYE KOCHA SAHIHI WA KUIFIKISHA ARSENAL SEHEMU SAHIHI
Bodi ilishaamua hata fukuzwa, labda itokee timu ifikie kiwango kama cha unai emery, timu ilifikia hata kufanya buildup haiwezi....
Binafsi najivunia kuwa na kocha kama ARTETA...ana mbinu nyingi...ambazo zinahitaji muda na wachezaji aina anayoitaka .
Pep Guardiola alisema BODI ya arsenal itafanya kosa kubwa sana wakija kumfukuza Arteta ...
FERGUSON..alichukua misimu minne akikoswakoswa kufukuzwa kabla ya kuanza kuipa mafanikio man u...Pep alihitaji mwaka 1, Klopp alihitaji miaka mi 3
Arteta ameshatengeneza MFUMO sahihi wa KUKABA, KUSHAMBULIA, wote tunakumbuka timu ilikuwa na beki nzuri ila haitengenezi nafasi... tumetoka huko sasa...
Kilichobaki sasa, ni kuyatumia vizuri madirisha ya usajiri kwa kusajiri wachezaji sahihi wanaoingia kwenye mifumo iliyowekwa,
Wanaolalamika kila siku hawajui hii timu ARTETA kaichukua
kwa UNAI EMERY ikiwa haiwezi hata kufanya buildup, haiwezi hata kushinda away, ilifikia hiyo hatua.....
Leo tunaona wachezaji walewale wanaanzia mpira nyuma na wanakwenda mbele, wanazuia kwa mfumo sahihi, makosa ya kukosa wachezaji QUALITY , yatatibiwa na usajiri sahihi, mfano mtu kama CEBALLOS, BELLERIN na baadhi yao kwa ARTETA wanaonekana kukosa kile anachokihitaji .
Mfano mechi V/S man city, tulicheza vzr tukazidiwa kwenye quality, lkn binafsi nilifarijika na timu ilivyochez nikaamini LEICESTER atakula kipigo iwapo Tutacheza kama dhidi ya city.....
Lakini kuhusu kocha binafsi huyu ndiye Atakayetufikisha mahala sahihi,
UNAYEWAZA BODI IMTIMUE ARTETA, UTAKAWIA SANA, TIMU INAMAENDELEO MAKUBWA KULIKO ALIPOIKUTA,
ARTETA anahitaji madirisha kadhaa ya usajiri.... ndio kwanza amepata dirisha moja kubwa la usajiri na madirisha madogo mawili, huku moja ni pale alipopewa timu tu.