Bado safari ni ndefu. Mantra ni ile ile kama una moyo mdogo endelea kujificha huko ulipo.
Kwa game ya leo Tierney na Partey hawatakuwepo, katikati itabidi awepo Xhaka na Elneny. Kuna msimu utafika Partey na Tierney wataonekana strong huo msimu ukifika tutafute wa kumtapeli kama tulivyowatapeli united kwa Sanchez na Van Persie.
Leeds habadilishi formation iwe jua iwe mvua yeye ni 4 1 4 1 tu dakika zote za mchezo anafanya ndani ya boksi la mpinzani kuwe na wachezaji zaidi ya 3. Ni nadra leeds kusecure clean sheet wakati formation inamruhusu kukaba na kushambulia, hapo ni mawili ama timu haina stamina au mabeki ni wabovu.
As in utakuta anashinda 4 na yeye anakua kafungwa 2. Maajabu yake first leg tulitoka nao bila bila, kwamba defense yetu ilikua poa sana, ila attacking yetu haina makali siyo kwa leeds pekee.
Kuna wachezaji wakibadili kitu fulani wanakua hovyo, Iwobi wakati ana panki alikua hatari alivyoanza dredi akawa utumbo, Aguero bila bleach alikua hatari alivyoweka bleach na majeruhi yakamkumbuka, same kwa Messi. Magalhaes afanye kuondoa kale kableach ile ndiyo laana yake. Inamfanya asionekane kama yupo serious.
Anyway, tulitoka bila bila na leeds tukiwa tunacheza 4 2 3 1 game ilikua ngumu hii siku. Arteta alikua anajaribu AM gani atasaidia timu na alimpa namba Willock, jamaa mmoja akapata red ya kizembe kweli kweli. Na matokeo yake?
Leeds wakapossess mpira kwa asilimia 66.
Leeds wakapiga mashuti 25 dhidi ya 9 ya Arsenal.
Leeds ikatengeneza big chance 2 dhidi ya moja ya Arsenal.
Leeds ilipiga pasi 610 dhidi ya 310 za Arsenal.
Watu wakakimbia uzi.
Ilionyesha Arsenal bado safari ndefu. Kadi moja nyekundu kwa timu iliyokamilika siyo kitu kabisa ila kwa Arsenal hua ni dhahma.
Alloski anasema ana hamu ya kukutana na rafiki yake Pepe hii ni mind play ili Pepe arudie komedi ile ile apate tena red.
Ila siku hizi Peoe hachezi upande wa Alloski so kama Alloski atapangwa kumfuata Pepe basi tutajua kua Leeds wako serious na ushindi wa leo as huu ushindi utamfanya azidi kuweka gape kati yake na sisi tunaoshika nafasi ya 11 kushuka chini.
Again, betting companies hazina imani na Arsenal, zimetoa odds kuanzia 1.80 mpaka 2 wakati leeds kapewa 4 mpaka 4.10. Sofascore inasema kwa hizo odds Arsenal hugewa asilimia 55 za kushinda ila hushinda kwa asilimia 34.
Leeds hugewa asilimia 25 kushinda wakiwa na odds hizo ila hushinda kwa asilimia 47. Hivyo basi katika hii game anayetarajiwa kushinda ni Leeds. Plus majeruhi tuliyonayo so you know where this is going.
Nafikiri tufocus na Europa. Kwa sasa Arsenal hata ikifight vipi haitashika zaidi ya nafasi ya pili ambayo matokeo yake ni kwenda uefa, ukichukua europa unaenda uefa ila u go with style, so tufocus huko. Thom na KT3 wagonjwa ila itakua vyema wakiwepo katika game ya Benfica.