Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Game inaonyeshwa na channel gan king'amuzi gani?
Inaoneshwa hapa..
Screenshot_20210218-222654_Live%20Football%20TV.jpg


Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Naweza nikaanza ongelea namna defense yetu inavyofanya kazi na nisimalize sasa hivi. Kuna wachezaji inabidi wapumzike, funny thing ni kwamba atakayeingia ni Willian.

Auba msimu uliopita alilia tulivyotolewa na Olympiacos, unamuona leo? Hata mtangazaji anasema haoni spark. Kwa formation na defense ya Benfica anahitajika Pepe na Lacazette, two players ambao hawana kigugumizi cha miguu katika kushuti hata nje ya box.
 
Naweza nikaanza ongelea namna defense yetu inavyofanya kazi na nisimalize sasa hivi. Kuna wachezaji inabidi wapumzike, funny thing ni kwamba atakayeingia ni Willian.

Auba msimu uliopita alilia tulivyotolewa na Olympiacos, unamuona leo? Hata mtangazaji anasema haoni spark. Kwa formation na defense ya Benfica anahitajika Pepe na Lacazette, two players ambao hawana kigugumizi cha miguu katika kushuti hata nje ya box.
Tusubiri tuone mpira dak 90!!!
 
Game haikua nzuri. Imeexpose kua tukipakiwa basi bado tuna tatizo la creativity.

Tumepigiwa penati dakika ya 55 tukasakama lango kwa dakika 2 tu tukapata goli. Kisha tukapoa.

Unamtoaje mtu aliyekupa assist ya goli? Kama hoja yako ni mbona Benfica wamemtoa aliyewafungia goli kumbuka kua goli lao ni penati.

Pepe amefunga games 3 mfululizo europa, kwanini alikaa nje?

Defense yetu ni inataka kufanya constant pressure ila haina wachezaji wa kufanya hilo liwezekane kwa asilimia zote, hii imepelekea kuwapa Benfica chances zaidi ya mbili ambazo wangeweza kuscore tatizo ni kwamba walikuja kua wasimamizi wa handballs na si kingine. Ndiyo maana tukicheza na timu kama city au liva hii defense huonekana kichekesho.

Msimu uliopita first leg ya Juve na Barca Morata aliscore magoli 3 na yote yakawa offside hizi offside za leo ndiyo zilichonikumbusha, siyo ilitakiwa forward ijue kua inatakiwa kusearch magoli nje ya box? kwa sababu Benfica made sure kwamba kuna wachezaji tisa kwenye boksi lao kila muda Arsenal ikipandisha mashambulizi ila mkitaka kuwapiga kaunta wanawategea offside. This explains back passes za kumwaga.

It also explains why we needed Pepe earlier. I always say Emile ana strength moja tu 'Passing' ndiyo maan hakukua na attempts zozote za Emile kutumia skills kubreak defense, imagine Pepe angekuepo tangu mwanzo wa mchezo.

Mambo mengine kocha anayataka.

Msimu uliopita tuliwafunga Olympiacos moja walivyokuja Emirates wakatufunga 2 kwa 1 so hii moja moja ya leo haitugarantii chochote bado yeyote anaweza kufungwa.
 
Tunaifuata game na city kinyonge kweli kweli. Suluhu ambayo tulitakiwa tushinde huku defense ikiwa hovyo.

Ni lini umewahi kuona Arsenal kagewa odds 6+? Betika wameipa Arsenal odds 6.50, Betpawa wametoa odds 6.00 kwa Arsenal. Hili kwangu ni jipya, tumetembelea sana odds za 2 na 4 ila kwa game ya kesho sasa ndiyo tunaenda kiunderdog zaidi.

De Bruyne kapona, majeruhi walionao ni Nathan Ake ambaye hata alivyocheza alionyesha bado ana mchango mdogo, kisha na Gundogan, recently Gundogan is on fire.

Juzi Auba alipata chances 2 moja alibaki yeye na kipa baada ya krosi ya Saka akatoa nje ya pili alitaka kumfinya beki ila beki akaunasa.
Gundogan aliupokea mpira mrefu wa Ederson akamtesa Sanchez, Sanchez chali kama gunia akascore easily.

So we know jeuri ya kukabidhiwa odds 6 imetoka wapi.

Muda huu naandika Livescore inaonyesha Arsenal ina 35% ya ushindi City 42% na draw ni 23%. Sofascore inaonyesha watu 4876 wanatabiri Arsenal kushinda, watu 9727 wanatabiri City kushinda na watu 2572 wametabiri draw.

Zile back passes za juzi zilitokana na benfica kupaki basi au siyo now City hawatapaki basi na hivi karibuni wamerudia 4 3 3 na wanatumia mid na attacking fullbacks kutafuta magoli unlike baadhi ya opponents tuliokutana nao.

City ni superior kimbinu na quality ya wachezaji kwa sasa ni fair tukienda kujilinda na tukawa na striker ambaye anaweza kutoboa katikati ya watu, hivyo kwangu mimi Elneny na Xhaka wakae kati, Auba awe LMF, Odegaard awe AM, Saka awe RMF na ST awe Lacazette.

Pablo Mari kapona, Rob Holding yupo, Gabriel yupo, duo ya Rob na Gabriel na Rob na Mari ilitugea clean sheet nyingi sana, Luiz asicheze as City ni wazuri kwa kujiangusha na ni tatizo kua na beki kama Luiz unapocheza na divers.

Bellerin amekua shit, advantage yake huyu jamaa ni spidi. Kwa Arsenal ndiye mchezaji mwenye spid kabla ya Saka juzi kugewa 96 kwenye pace na Tierney kuja. So unatarajia aweze kumtrack Sterling, ila Sterling ana pace kubwa, diver na skills za kumwaga so ni sawa kabisa kuhisi atamsumbua Bellerin. Na kwa recent form unaona wazi Bellerin kazi anayo.

Ila kama mbwai iwe mbwai, Cedric awe RB na Tierney awe LB. Kimahesabu Arsenal hatuna chance ila hapana, tuna chance nzuri tu, lolote litatokea tulishawadisappoint City so kesho haitakua mara ya kwanza.

Wa kuchungwa ni mawinga, na Debruyne kama akipangwa. Kesho ni kesho anapasuka mtu.
 
Siku hiyo mjitahid mshindi aisee, tumechoka kuwatania kila mara.
 
Lazima tubanduliwe,

Haya watoto, semeni kwa nguvu

'LAZIMA TUBANDULIWE'
 
Back
Top Bottom