Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Niliandika awali mlolongo huu kufikia malengo Özil, Kolasinac, Mustafi, Elneny, Xhaka na Pepe.

Sokratis papa aliyekuwa na experience aliachwa na kuwekwa Saliba ambaye hakutaka hata kumtumia unafahamu kwa nini?
Sokratis siyo muislamu.

Huo mlolongo wako unaweza kufeli kwasababu Arsenal iko tayari kumuuza Pepe kiangazi kama asipoimprove.

Hivi kwa mpira wa siku hizi utajisikia amani kua na beki kama Kolasinac? Hajui krosi, pace ndogo, na siyo mzuri passing.

Mustafi je? Unakumbuka tunacheza na Leicester game iko dakika ya 80+ Mustafi alichotufanyia?

Je Carabao?

Leo timu yetu umri wastani ni 25.6 ni dhahiri kuna watu inabidi waende waje youngsters. Youngsters wengine watatoka academy na ni waislamu.

Na mlolongo wako umelenga umri ukijua hawa watu umri utawatupa mkono na wataenda haujabase kwenye dini wala performance.

Anayeweza andika thread kudebunk maoni yako afanye hivyo.

Shareholder Aliko Dangote ni muislamu pia.
 
Itakuwa vizuri mkiachana na mambo ya Imani na hiyo mnaita haki, hayana afya wala maana yoyote.

Tunataka uchambuzi wa kisoka.
 
Sitaki kuamini chama langu lina mambo ya ubaguzi wa aina yoyote ule, iwe dini, rangi, sexual orientation wala siasa za vyama. Na sisi huwa ni mfano wa kuigwa kwa wengine.
 
Tatizo ni kusoma na usielewe, hapa nitamjibu na Castr swali ulilofanyia quote hii. Nimewataja wote even Xhaka kwa sababu ni moja ya mshakaji wangu wa karibu.

Naandika tulipo na tunakoenda (Under Edu na Arteta) ambao wao wana hila sio Arsene Wenger aliyetengeneza familia kwa miaka 20+ hawa wanakuja kuvuruga.

Currently wachezaji wenye mlengo wa Kiislam Arsenal hawatakiwi kuonekana.
Nonsense
 
Arteta akiongelea uwezekano Aubameyang kucheza dhidi ya United:

"Sijui. Mambo yana onekana yako vizuri kwa sasa hivi lakini itabidi tusubiri tuone. Ni kapteni wetu na moja ya mchezaji muhimu. Tunafanya kila linalo wezekana ili kumpata haraka iwezekanavyo."
 
Arteta akiongelea uwezekano wa Nelson kuondoka kwa mkopo:

"Hayo ni mazungumzo tunayokua nayo na wachezaji wasio pata nafasi ya kucheza mechi nyingi. Ni wazi kwamba tunataka waendelee vizuri na tutafanya maamuzi ndani ya siku tatu zijazo na baadhi yao ili tuone inakuwaje. "
 
Mark Bryans - Arsenal bado wana mawasiliano ya karibu na Aubameyang ambae ameweka wazi jioni hii kwamba anauguliwa na mama yake mzazi jambo lililo mfanya akose mechi mbili za hivi karibuni.

Aubameyang mwenyewe amethibitisha kuimarika kwa afya ya mama yake lakini uamuzi wa kumtumia kwenye mchezo dhidi ya Man United bado haujafikiwa.
 
Odegaard atakuwa anacheza nafasi ya Smith-Rowe #10 na kina Pepe na Willian kulia?
 
Back
Top Bottom