MATTEO BADO HATOSHI KWENYE KIUNGO CHA ARSENAL
Huu ni ukweli ambao haupingiki , ni ukweli ulio dhahiri
Utajiri wa timu utapata kwenye kiungo , kupitia Kiungo bora utapata nafasi nyingi za Magoli
Arsenal imezorota toka mwanzo wa Msimu sababu ya kiburi cha Unai kumfanya Matteo Gunduz ndio backbone ya Kiungo , huku akimuacha MTU mwenye uwezo Lucas toreira na Ceballos bench ,
Ni ukweli uliodhahiri aliyemponza Xhaka kuonekana Hafai ni Matteo Gunduz ,
Muunganiko wa Matteo gunduz na Xhaka ,ulimfanya Xhaka awe Na kazi mbili hivo kupelekea kufanya Makosa mengi sana na kuonekana Xhaka ni mbovu ,
Wote ni mashahidi Combination ya Xhaka na Lucas toreira huifanya Timu iwe stable eneo la kati kati.
Kiburi cha emery kumkumbatia Matteo Guondouz Kama muhimili wa midfield , alikuwa anatushusha daraja kama asingefukuzwa
Leo Ukiweka viungo xhaka na Ceballos utapata Stability , ukimuweka Ceballos na Lt11 bado timu itakuwa stable
Kwanini Ukimuweka tu Matteo na xhaka au Matteo na Yeyote lazima Kiungo kipate taabu kwanini?
Kwa muono wangu Arsenal Ili tuende mbele zaidi tunatakiwa kuongeza Watu zaidi eneo la kiungo na Kuwatoa mkopo kina Matteo na willock ,
Matteo amekuwa hatimizi majukumu yake ipasavyo , wengi huwa wanafurahia anavyozunguka zunguka WA naona anajituma sana , lakini ndiye mchezaji anayepiga pass za nyuma sana , ndio maana kwa Muda mwingi aliopewa Arsenal ana assist 1 kama sijakosea kwenye EPL , na hana goli lolote KWENYE EPL ,
Hii inadhihirisha Timu inahitajika viungo wanyumbulifu ,wakupiga Key passes kwenda mbele zenye madhara .
Tuliona mechi na Newcastle jinsi Ceballos alivyokuwa anapeleka mipira mbele na kumrahisishia kazi Ozil .
Kitu ambacho Gunduz hana , ni kiungo pia Anakosa creativity, shooting accuracy ,
Tayari Kwa kuliona hili Arsenal inatajwa kufatilia kiungo wa Valencia mithili ya David Silva , anaitwa Carlos Soler ,
Pia wiki iliyopita Arsenal ilituma maskauti kumfatilia kiungo wa Roma anayeitwa BRYAN CRISTANTE
Ni mtizamo tu .