Guardiola alipofika Man City baada ya muda Yaya akawa anaonyeshwa dalili za kutotakiwa, ni ukweli timu ikawa kama inelegea hivi lakini baada ya Yaya kuondoka na muda kupita Man City anacheza mpira mzuri kuliko alivyokua Yaya.
Sir Alex Ferguson alikua na Beckham, mtu mbaya wa dead balls, Beckham akaonyeshwa njia akiwa wa motoooo. Baada ya pale Man U haikuacha kuonyesha ushindani na hatimaye kutwaa vikombe.
Neymar akatwaliwa Barcelona, alikua poa. Yeye na wenzake wakaunda utatu wa MSN, Messi & Suarez & Neymar, akajiona anahitaji kuanzisha ufalme wake akaruhusiwa kwenda.
Mourinho akiwa Man U akakutana na bishoo Pogba, akaona hawataivana akawa anamzoesha benchi taratiiiibu. Mashabiki wa Man U wakachochea kutochezeshwa kwa Pogba iwe chanzo cha Mou kuondoka kwakua haitakii timu mema wakisaidiwa na wakina Scholes na Giggs.
Emery akatua Arsenal. Arsenal imechoka haina hata beki kiasimpaka CMF Niles anachezeshwa beki wa kulia, siyo jambo baya maana Wenger alishamfanya Eboue akawa beki badala ya Winger na Kolo Toure akawa beki badala ya striker, anyway timu ilikua hovyo. Ngungwa ngungwa Arsenal ikafika fainali Europa.
Emery pengine hajui, hajui kua shabiki hakosagi goli na hakosei. Kwahiyo mashabiki walivyokua wanamtajia kikosi wanachotamani fainali ya Europa kwenye page yake na ya Arsenal huko IG alitakiwa kupuuza, badala yake akapanga kikosi kilekile kilicholiliwa na mashabiki na matokeo ikawa Arsenal kufa nne bila.
Mashabiki walimlilia Ozil, alikuepo pia siku hiyo. Pengine siyo wote tuliomsikia Ospina, jamaa alisema Mesut ni mchezaji ambaye siku akiwa vizuri anakua vizuri mara mbili ya kawaida, hiyo ndiyo vile anatengeneza nafasi sita katika dakika 71, na siku akiwa vibaya ni anakua vibaya mara saba ya kawaida, hiyo ndiyo siku unaona watu mnapigwa na playmaker wa kuaminiwa haonekani.
My point is, mashabiki tunakosea tunapolazimisha Emery awe Wenger, kila mmoja ana dira na falsafa zake. Kama Emery anaona Ozila hafai kwenye mechi hii akamuweka nje hilo siyo tatizo, Guardiola alimuona Yaya hafai, Neymar, Beckham wote hao yet teams survived.
Timu ni kubwa kuliko mchezaji.,