Richard
Platinum Member
- Oct 23, 2006
- 16,636
- 25,617
Mkuu kuna watu wenyewe wanaona emery yupo sawa, lkn hata wakuu wa bodi hawaridhishwi na timu inavyocheza
Mkuu Aaron, mimi nakuelewa sana tena sana tu.
ila Arsenal hii si ile tuloizoea siku zote.
Emery huchezesha timu kulingana na mipango ya timu adui, hivyo Arsenal kushindwa kuwa na game plan za maana.
Game plan za maana za Arsenal ambazo hutoa matokeo ya moja kwa moja ni zile zinazohusu ligi ya Europa kwani zile ni timu ambazo hazipo kwenye PL.
Timu nyingi za PL chini ya Top 6 hucheza sana kwa kujihami huku zikifanya "counter attack" na mipira mirefu.
Hivyo strategy ya Unai Emery ni kusoma kila timu kabla ya kucheza mbinu ambayo ni ya kipekee kidogo.
Lakini mwisho wa siku tunapata points kama za leo, na hata hiyo bodi itakuwa inaangalia matokeo zaidi.
Ukitaka kufahamu zaidi kuhusu msimamo wa Arsenal kwenye ligi, basi fuatilia wakati wa Xmas ndipo patatoa picha halisi.
Arsenal ikiwa ndani ya 3 bora baada ya Boxing Day basi tutamaliza ligi ndani ya top 4.