- Wachezaji wengi kuuzwa au kuondolewa Arsenal ikijiandaa na msimu ujao wa 2019/20
- Nicolo Barella wa Gagliari ya Italia anafukuziwa kuziba nafasi ya Aaron Ramsey.
- Schodran Mustafi anaongoza orodha ya wachezaji wasohitajika.
Arsenal wanamhitaji nahodha wa Cagliari na kiungo mshambuliaji Nicolo Barella.
Bodi ya Arsenal imemhakikishia kocha Unai Emery kitita cha kutosha kufanya usajili wa aina yake endapo tu Arsenal itafuzu kucheza ligi ya mabingwa wa Ulaya msimu ujao.
Pamoja na mabeki Calum Chambers (yuko Fulham kwa mkopo) na Rob Holding ambae alikuwa majeruhi na sasa amepona, pia yupo beki wa kulia Hector Berellin.
Ipo orodha ya wachezaji ambao endapo Arsenal itawasajili msimu ujao basi Arsenal haitakuwa na shida ya kuwa moja ya timu tishio.
Wachezaji kama mshambuliaji wa pembeni wa Crystal Palace Winfried Zaha, beki wa kati Samuel Umtiti wa Barcelona, Malcom wa Barcelona ni miongoni mwa wachezaji kadhaa aliopo kwenye orodha ya mahitaji kusajiliwa msimu ujao.
Mchezai wa kiungo wa Cagriali Nicolo Barella ndie anaeangaliwa kuja kuziba nafasi ya Aaron Ramsey.
Barella ana uwezo wa kupokonya mipira katikati na kumpasia Alexandra Lacazette ili aweze kufunga, kazi ambayo imemshinda Mesut Ozil kwa kiasi kikubwa khasa kwenye mechi za ugenini.
Kazi afanyazo Barella awapo katikati ya uwanja na timu yake hufanana kabisa na kazi wafanyazo Christian Eriksen wa Tottenham, au Bernado Silva wa Machezster City au Willian wa Chelsea.
Hivyo Iwapo Barella atasajiliwa na Arsenal basi atacheza akiwa mbele ya Granit Xhaka na Lucas Torreira na nyumba ya mshambuliaji Alexandra Lacazette.
Ntaanza kushuka na baadhi ya "target" za Arsenal kwa msimu ujao baada ya mechi na leicester kesho mchana.
Arsenal inahitaji wachezaji kama 5 hivi ili kuwa timu imara zaidi khasa kwenye nafasi ya mabeki, kiungo na mshambuliaji wa pembeni.