Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Msiwe na wasiwasi, Arsenal watashinda mechi ya marudiano kwenye uwanja wa Emirates.

Mechi ya jana ilichezwa kwenye joto la chini ya nyuzi 0 kwenye baridi kali hivyo kwa kiasi fulani kuliathiri uchezaji wenye ufanisi.

Halafu msisahau Lacazette alifunga goli na likakataliwa kwa sababu ya kuwa offside.

Isitoshe kuna wiki nzima ya kujiandaa kuja kuwashughulikia hawa watengeneza matrekta Alhamisi ijayo.

Ila hawa jamaa walijiandaa kwa kuwa na likizo ya baridi (winter break) kwa wiki tisa mfululizo hivy kuipa mechi ya Arsenal umuhimu wake.

Pia kama mnamkumbuka Alexandre Hleb nae alikuwa ni mmoja wa wachezaji wa kiungo wa timu hii huku akiwahamasisha wachezaji wadogo kwake kucheza kwa bidii (Hleb ana miaka 37 sasa).

Alex Hleb amehirisha kabisa kustaafu kucheza soka mpaka acheze na Arsenal mechi zote mbili nyumbani na ugenini, hivyo utaona jinsi hawa jamaa walivyojiandaa.

1550193813999.png

Nacho Monreal, Alexandre Lacazette na Saed Kolasinac wakiwa wamevaa sweta za mikononi (Gloves) kutokana na baridi kali la nyuzi chini ya 0 mjini Barisaw nchini Belarus.
 
Msiwe na wasiwasi, Arsenal watashinda mechi ya marudiano kwenye uwanja wa Emirates.

Mechi ya jana ilichezwa kwenye joto la chini ya nyuzi 0 kwenye baridi kali hivyo kwa kiasi fulani kuliathiri uchezaji wenye ufanisi.

Halafu msisahau Lacazette alifunga goli na likakataliwa kwa sababu ya kuwa offside.

Isitoshe kuna wiki nzima ya kujiandaa kuja kuwashughulikia hawa watengeneza matrekta Alhamisi ijayo.

Ila hawa jamaa walijiandaa kwa kuwa na likizo ya baridi (winter break) kwa wiki tisa mfululizo hivy kuipa mechi ya Arsenal umuhimu wake.

Pia kama mnamkumbuka Alexandre Hleb nae alikuwa ni mmoja wa wachezaji wa kiungo wa timu hii huku akiwahamasisha wachezaji wadogo kwake kucheza kwa bidii (Hleb ana miaka 37 sasa).

Alex Hleb amehirisha kabisa kustaafu kucheza soka mpaka acheze na Arsenal mechi zote mbili nyumbani na ugenini, hivyo utaona jinsi hawa jamaa walivyojiandaa.

View attachment 1022896
Nacho Monreal, Alexandre Lacazette na Saed Kilasinac wakiwa wamevaa sweta za mikononi (Gloves) kutokana na baridi kali la nyuzi chini ya 0 mjini Barisaw nchini Belarus.
UONGO TU KWANI WAO WALIKUJANA JIKO WAKIOTA MOTO
 
UONGO TU KWANI WAO WALIKUJANA JIKO WAKIOTA MOTO
Mambo ya hali ya hewa si chochote kwa timu yetu kwani kila mchezaji alitimiza wajibu wake kosa ni maamzi mabovu ya refa kwani wachezaji wetu wamechezewa vibaya hatoi adhabu yoyote hali iliyopelekea wapinzani wetu kupata viburi wakawa wanafanya wawezavyo.
Lacazette amepita kwa shida akafunga goli wakadai offside,mara ya pili amechezewa faulo refa kimya mchezaji akabembea kiunoni kabisa lacazette kamburuza na mpira refa kimya lacazette akaamua kumtwisha kipepsi hapo ndo akatoa red card. Tumefanyiwa umafia sana na waamzi, wengi hawajui kwa kuwa hata mpira hawakuuona.

We are the GUNNERS forever.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa nyie ndugu huko Europa mkipigwa na msipoingia top four mnakuwa na utofauti gani na Everton

Sent using simu mbovu
 
Footballer yeyote duniani mwenye kiwango bora ndoto yake ni Real Madrid na Barca

Sent using Jamii Forums mobile app


Sio wote mkuu, wengi wenye ndoto hizo ni washamba fulani wa mpira kutokea Amerika kusini

Watu kama Pogba, lewandoski, Robben na wengi tu ambao ni wajanja wa kuzaliwa ulaya hawashobokei Barca/Real. Kwa sasa timu kubwa ni nyingi hasa hasa za EPL Big 6,,,,,,,,,,,, sasa washamba wanashobokea Barca/Real
 
Sio wote mkuu, wengi wenye ndoto hizo ni washamba fulani wa mpira kutokea Amerika kusini

Watu kama Pogba, lewandoski, Robben na wengi tu ambao ni wajanja wa kuzaliwa ulaya hawashobokei Barca/Real. Kwa sasa timu kubwa ni nyingi hasa hasa za EPL Big 6,,,,,,,,,,,, sasa washamba wanashobokea Barca/Real
Huyo Robben mwenyewe kashapita huko. Lewandowski mwenyewe alitaka kwenda ila deal yake haiku materialise.
Pogba hajaitajika tu, angeenda mbio sana, stail ya mpira wake sio ya Spain. Kule akili nyingi zinahitajika zaidi ya nguvu. Ndio mana anakomaa na Italy na hapo Uingereza. Timu kubwa EPL ni kubwa kwa hapo EPL na ligi nyingine ndogo ndogo. Timu kubwa laliga ni timu kubwa duniani. Ila kama unazungumzia ukubwa wa kelele basi EPL ni kubwa sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa nyie ndugu huko Europa mkipigwa na msipoingia top four mnakuwa na utofauti gani na Everton

Sent using simu mbovu
Kwani tulienda Europa kwa sifa ipi mpaka sasa. Mkiambiwa ukweli mnasema tunawatukana kumbe ufinyu wa akili zenu wa kutokuelewa mambo ndo unawafanya msijue lolote kuhusu mpira.

We are the GUNNERS forever.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hmm.. Maisha haya acha tu. Yule dully Jr kapotea, mla panya anatukana watu sa ivi. Aroon uko wapi mbona hamji kwenye majukwaa yetu kutuletea umbea.

Sent using Jamii Forums mobile app
Game tumeumizwa na waamzi openly as if ni game la mchangani halafu mtu unavamia jukwaa kuleta zengwe mie nakujibu vizr tu ila wewe utatafsiri kuwa ni matusi.
All in all simlaumu kocha nawalaumu waamzi tu. Tulipiga mpira mwingi wa maana tunafunga magoli yanakataliwa, penalty zinagomewa, tunapewa red card ambazo source ni waamzi. Yamepita tunawasubiri Emirates.

We are the GUNNERS forever.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom