Arsenal huenda ikakamilisha usajili wa Denis Suarez kabla ya mechi na Manchester City
View attachment 1008480
Denis Suarez.
Klabu ya Arsenal mwishoni wa juma hili inatarajiwa kutangaza usajili wa kwanza wa mchezaji wa kiungo Denis Suarez ambae anakuja kuchukua nafasi ya Aaron Ramsey ambae anaondoka baadae kwenda Juventus.
Arsenal imemchukua Suarez kwa mkopo hadi mwisho wa msimu ambapo inaweza kumsajili kiukamilifu kwa pauni milioni 20.
Hapo awali nilisema mchezaji huyu angekuwa asajiliwe wiki ilopita lakini kutokana na timu yake ya Barcelona kutaka Arsenal wamchukue moja kwa moja Deni bila kufanya mkopo kukawa na mazungumzo marefu juu ya dili hilo la mkopo na kwamba Arsenal hawako tayari kumsajili mchezaji yoyote yule hadi msimu ujao.
Denis pia alikuwa kiviziwa na timu za Real betis na Sevilla ambayo meneja Unai mery aliwahi kumfundisha Denis alipokuwa timu ya pili.
Denis Suarez ni matunda ya kitalu cha wachezaji wadogo wa Manchester City ambao endapo Arsenal watamsajili mwezi juini mwaka huu basi Manchester City watapata kiasi cha fedha cha pauni milioni 4, kwasababu waliweka kifungu kidogo cha kupata faida itayopatikana na usajili wa mchezaji huyo.
Karibu Arsena Denis Suarez.