Aaron Arsenal
JF-Expert Member
- Jul 24, 2014
- 24,504
- 28,691
Tetesi-Arsenal yatuma maombi ya kumsajili Gelson Martins
Wakati zikiwa zimebaki siku 10 kufikia tamati kwa dirisha hili la usajili, timu ya Arsenal imehusishwa na usajili wa winga wa Atletico Madrid Gelson Martins.
Kocha wa Arsenal Unai Emery yupo sokoni kutafuta wachezaji wa kukiimalisha kikosi chake hasa kwa upande wa mawinga na mabeki wa kati lakini kutokana na Arsenal kutokuwa na pesa za kufanya usajili kazi hiyo imekuwa ngumu maradufu kwani kwa sasa Arsenal inaweza kusajili kwa mkopo tu.
Gazeti maarufu la soka la Ureno O Jogo limeandika ya kwamba Arsenal imetuma rasmi maombi ya kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23.
Gelson Martins aliwasili katika timu ya Atletico Madrid msimu uliopita, lakini ameshindwa kuwika katika kikosi cha Diego Simeone kiasi cha kukosa namba ya kudumu katika kikosi cha kwanza.
Inasemekana ya kwamba Atletico Madrid wapo tayari kumuachia mchezaji huyo kwa mkopo ili kumpisha Alvaro Morata ambaye wapo mbioni kumsajili kutoka Chelsea.
Iwapo mpango huo utafanikiwa Arsenal itamsajili mchezaji huyo kwa mkopo wa miezi 6 na kama atafanya vizuri wana mpango wa kumsajili moja kwa moja.
Wakati tetesi hizo za Martins zikipamba moto taarifa nyingine ni kwamba Arsenal imeshaafikiana na Barcelona kuhusu usajili wa Denis Suarez na bado mambo madogo madogo yanayokwamisha kutangazwa kwa usajili huo.
Sent using Jamii Forums mobile app
Wakati zikiwa zimebaki siku 10 kufikia tamati kwa dirisha hili la usajili, timu ya Arsenal imehusishwa na usajili wa winga wa Atletico Madrid Gelson Martins.
Kocha wa Arsenal Unai Emery yupo sokoni kutafuta wachezaji wa kukiimalisha kikosi chake hasa kwa upande wa mawinga na mabeki wa kati lakini kutokana na Arsenal kutokuwa na pesa za kufanya usajili kazi hiyo imekuwa ngumu maradufu kwani kwa sasa Arsenal inaweza kusajili kwa mkopo tu.
Gazeti maarufu la soka la Ureno O Jogo limeandika ya kwamba Arsenal imetuma rasmi maombi ya kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23.
Gelson Martins aliwasili katika timu ya Atletico Madrid msimu uliopita, lakini ameshindwa kuwika katika kikosi cha Diego Simeone kiasi cha kukosa namba ya kudumu katika kikosi cha kwanza.
Inasemekana ya kwamba Atletico Madrid wapo tayari kumuachia mchezaji huyo kwa mkopo ili kumpisha Alvaro Morata ambaye wapo mbioni kumsajili kutoka Chelsea.
Iwapo mpango huo utafanikiwa Arsenal itamsajili mchezaji huyo kwa mkopo wa miezi 6 na kama atafanya vizuri wana mpango wa kumsajili moja kwa moja.
Wakati tetesi hizo za Martins zikipamba moto taarifa nyingine ni kwamba Arsenal imeshaafikiana na Barcelona kuhusu usajili wa Denis Suarez na bado mambo madogo madogo yanayokwamisha kutangazwa kwa usajili huo.
Sent using Jamii Forums mobile app