Arsenal (The Gunners) | Special Thread

No, kumbuka msimu uliopita tulishinda games ngapi ugenini. Mwanzo mzuri naona.

Kupata matokeo chanya ugenini ni faraja sana nakumbuka msimu uliopita ugenini tumepigika sana hata hawa Newcastle walitupiga hapo St. James' Park 2-1 tena tulianza sisi kufungua goli la Auba ila wakachomoa na kipigo tukakipata,naona Ozil leo kafurahi nimemsikia jinsi anavyoongea inaonyesha anakerwa na critics kutoka kwa watu ni kitu kizuri kama atakaza zaidi(mshahara alioubeba utamsumbua sana hasa waandishi wa UK)
 
Kuna kitu nakiona kinajengwa kwani msimu uliopita kushinda mechi tatu mfululizo ilikuwa shughuli.

Arsenal imebadilika kidogo na sasa wanacheza mpira wa akili na mpangilio na kila mchezaji anaonyesha anashiriki kucheza game.

Ni tofauti ya Arsenal ya Arsene Wenger ambapo Arsenal walikosa plan B pale plan A ilipofeli. Sasa hivi wanaweza kubadili mchezo na angalau kupata sare kwenye mechi ngumu.

Newcastle walikuja na "game plan" kwamba wanawaruhsu Arsenal waingie eneo lao halafu wafanye counter attack.

Lakini Arsenal walimweka Guendouzi katikati kwa ajili hiyo (plan A) na kipindi cha pili Guendouzi alitolewa harakaharaka wakamwingiza Lucas Ferreira (plan B) ambae alisababisha Arsenal wacheze kwa uzito wake na kupata hilo goli la kwanza.

Ingawa kipindi cha kwanza Arsenal walikuwa wanaonyesha kutetereka lakini kipindi cha pili waliweza kutumia nafasi mbili kwa ubora na kufunga.

Na hivyo ndivyo inavyotakiwa unapocheza ugenini.
 



Hahahahahahahahahah

Hivi anakula ngapi vile kwa wiki?
 
Nakusalimu Richard.
 
Chief Executive Ivan Gazadis to AC Milan, inaathari gani kwa timu?
 
Chief Executive Ivan Gazadis to AC Milan, inaathari gani kwa timu?

Uyu jamaa kapigwa kitu wanaita "Double Your Money Offer" maana anaenda AC Milan kupokea £3.6 million kwa mwaka wakati Arsenal alikua anakunja £1.7 million ivyo ilikua lazima tu asepe pamoja na Stan kujitahidi ili abakie Arsenal,simply kwa amekua Arsenal kwa miaka almost 10 ivo alikua anaijua organization culture ya Arsenal nje na ndani.
Athari kubwa ni kwenye biashara maana inasemwa jamaa amekua msaada mkubwa kwenye mabadiliko ya kiuchumi ambayo Arsenal imepitia,Ivan pia ndio alieleta msukumo wa kuondoka AW na yeye jicho lake likamuona Unai ila hata kabla hajaondoka jamaa alileta new organizational structure ambayo Arsenal inaenda kuitumia kuanzia sasa kwa ku-introduce nafasi ya Head Of Recrutment ambayo amepewa Sven Mislintat na Head of football iko chini Raul Sanllehi,lazima tukubali anaacha pengo kubwa tu kwani ni mtu muhimu sana kwa Arsenal.
Tar 31.Oct rasmi anasepa na tarehe 1.Nov atakua anawatumikia Milan naamini tutamkumbuka kwa mabadiliko aliyo-inject kwetu.
 
Chief Executive Ivan Gazadis to AC Milan, inaathari gani kwa timu?
Haina madhara upande wa perfomance uwanjani, toka aje miaka 10 sasa timu haijafanya chochote cha maana, kwa kifupi ndio kwanza imeshuka viwango.
 
Lakini toka aje arsenal-fc haijawahi kufikia zile 'heights' za 2002-2006. Huoni nae alikuwa ovyo tu?
 
Hajawa Arseanl kwa miaka 20, kaja arsenal mwaka 2008 hivyo ni miaka 10. Toka aje timu haijashinda epl. That's a failure.
 
Lakini toka aje arsenal-fc haijawahi kufikia zile 'heights' za 2002-2006. Huoni nae alikuwa ovyo tu?

Nilishawai kusema siku moja matatizo ya Arsenal yanaanzia kwa wamiliki ukiangalia hapa kati Arsenal imezungukwa na mediocre players wengi ambao tunajiaminisha wangeweza kufanya maajabu,tulizoe kununua cheap players na kuwafanya kua bora ila wakiiva wamiliki wanatazama wapi wauzwe sababu wanaangalia uimara wa timu kwa jicho la kiuchumi zaidi.
Hawa akina Ivan ni mbuzi tu wa kafara ndio maana pamoja na furaha kuondoka AW niliwai kusema yule babu aliponzwa na ubahili wa wenye timu na akiamini anaweza kumfanya Diaby kua Vierra kuna upuuzi mkubwa wamiliki wanaufanya ila sisi tunaishia kuangalia kinachoendelea uwanjani tu kaangalie weekly wages ya squad yetu utacheka alafu tunataka matokeo chanya bado kuna safari ndefu swahiba.
 
Katika matatizo ya arsenal Wenger alikuwa part kwani kwenye wage bill arsenal kama mwaka juzi walikuwa kwenye level moja na Chelsea.tuna wachezaji wa kawaida wanalipwa mishahara mikubwa
 
Katika matatizo ya arsenal Wenger alikuwa part kwani kwenye wage bill arsenal kama mwaka juzi walikuwa kwenye level moja na Chelsea.tuna wachezaji wa kawaida wanalipwa mishahara mikubwa

Arsenal Players Salaries 2018/19 (Weekly Wages)
Bernd Leno £60,000
Petr Cech £100,000
David Ospina £40,000
Laurent Koscielny £75,000
Rob Holding £25,000
Nacho Monreal £65,000
Héctor Bellerín £100,000
Aaron Ramsey £110,000
Lucas Torreira £50,000
Mkhitaryan. £180,000
Mesut Özil £350,000
Alex Iwobi £30,000
Danny Welbeck £70,000
Aubameyang. £200,000
Lacazette £100,000

Nimejaribu kuweka ya hao wachache ambao wengi wao ni regular players hapo huo mishahara mikubwa iko wapi ukiacha na Ozil ambae anongoza kulipwa tena baada ya mbilinge sana kidogo aondoke zake hii naizungumza tukiangalia uwezo wa kiuchumi wa Arsenal pia.
 
Mjikaze sn Safari hii na huyu muhindi wenu Unai vinginevyo mrudisheni Babu Wenger
 
Siyo shida akiondoka kwani pia inatoa nafasi nzuri kwa uongozi mpya kuamua kwa maslahi ya timu bila kulaumu mtu.
Nionavyo arsenal inaelekea kuzuri zaidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…