Alexis Sanchez hakuwa "full fit" hivyo angeingia kipindi cha pili hivyo kumwachia Lacazette aanze mechi kama siku ya kwanza dhidi ya Leicester.
Hivyo akamwambia Wenger kwamba anaweza kuanza mechi ilhali hayuko full fit.
Hizi timu huwa zina utaratibu uitwao "fitness test" kabla ya mechi yoyote ile hivyo mchezaji huweza kutoa maoni yake kwamba yupo fit na akapangwa kwenye mechi.
Kama si Alexis Sanchez Arsenal isingefungwa goli hizo nne bali kungekuwepo matokeo mengine tofauti.
Pili, Wenger alikosea kuanza na Nacho Monreal kama namba nne wakati inafahamika wazi kuwa Nacho Monreal ni beki wa kushoto na hawezi kucheza kama beki wa kati.
Hivyo hivyo kwa Robert Holding ambae badala ya kucheza namba 4 ambayo ndiyo aliyokuwa akichezea hata kule Bolton Wenger akampanga kucheza namba tatu yaani upande wa kushoto, wakati yupo beki Saed Kolasinac ambae alicheza vizuri dhidi ya Leicester.
Tatu, Wenger alianza na Ramsey kama DM defensive Midfielder badala ya Mohamed Elneny ambae katika mechi ya kwanza dhidi ya Leicester alianza na alicheza vizuri.
Wenger kwa sasa amesahau kabisa principles zake anapokuwa anatafuta ushindi na timu ya Arsenal ya leo si ile niliyoiona mwaka 2000 hadi 2004.
Na bodi ya Arsenal imekuwa ikimsikilza sana Arsene kwa kuwa tu anahakikisha Klabu inaingiza mapato yake ya kila mechi na yale ya masoko.
Ndiyo maana kunatakiwa mabadiliko makubwa kwenye klabu na mabadiliko hayo yatakuja lakini baada ya Wenger kuondoka.