Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Sanchez 'OUT '

Arsene Wenger amethibitisha kwamba Alexis Sanchez atakosa mechi ya ufunguzi wa ligi dhidi ya Leicester kwasababu ya maumivu ya tumbo.

Gunners watamkosa nyota huyo wa Chile siku ya Ijumaa ambapo kikosi cha Craig Shakespeare kitakapo safiri kwenye mtanange utakaopigwa Emirates.

Sanchez alipata maumivu hayo akiwa mazoezini kuelekea mechi ya ngao ya jamii dhidi ya Chelsea na Wenger amekiri kwamba hana uhakika ni kwa muda gani Sanchez atakuwa nje ya dimba , licha ya kwamba anaamini kwamba atakosa pia mechi ya kwanza ya ugenini dhidi ya Stoke City Agosti 19.

"Sanchez hatopatikana kikosini. Ana maumivu ya tumbo aliyoyapata katika mazoezi siku ya jumapili asubuhi kabla ya mechi ya jioni Wembley."

"Alifanyiwa vipimo siku mbili kabla na atakuwa nje kwa muda.Sijui ni kwa muda gani atakuwa nje - wiki mbili au wiki moja zaidi. "

"Hatocheza dhidi ya Stoke."

Sanchez amekuwa akihusishwa na kuhama Emirates majira haya ya kiangazi na Paris Saint-Germain na Manchester City ndio wanapigana vikumbo kuwania saini yake.
 
Sanchez 'OUT '

Arsene Wenger amethibitisha kwamba Alexis Sanchez atakosa mechi ya ufunguzi wa ligi dhidi ya Leicester kwasababu ya maumivu ya tumbo.

Gunners watamkosa nyota huyo wa Chile siku ya Ijumaa ambapo kikosi cha Craig Shakespeare kitakapo safiri kwenye mtanange utakaopigwa Emirates.

Sanchez alipata maumivu hayo akiwa mazoezini kuelekea mechi ya ngao ya jamii dhidi ya Chelsea na Wenger amekiri kwamba hana uhakika ni kwa muda gani Sanchez atakuwa nje ya dimba , licha ya kwamba anaamini kwamba atakosa pia mechi ya kwanza ya ugenini dhidi ya Stoke City Agosti 19.

"Sanchez hatopatikana kikosini. Ana maumivu ya tumbo aliyoyapata katika mazoezi siku ya jumapili asubuhi kabla ya mechi ya jioni Wembley."

"Alifanyiwa vipimo siku mbili kabla na atakuwa nje kwa muda.Sijui ni kwa muda gani atakuwa nje - wiki mbili au wiki moja zaidi. "

"Hatocheza dhidi ya Stoke."

Sanchez amekuwa akihusishwa na kuhama Emirates majira haya ya kiangazi na Paris Saint-Germain na Manchester City ndio wanapigana vikumbo kuwania saini yake.
Dah, siyo dalili nzuri, isije ikawa kama mambo ya nasri na v parsie, alimchezesha nasri akacheza chini ya kiwango tukachapwa akakimbilia city, bora ampumzishe mpaka dirisha lifungwe au amuuze tu!
 
5fde2e401c89a894a1f8762b93675b7f.jpg
 
Back
Top Bottom