Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Gap kubwa sana hii ya magoli, inabidi kupunguza kwa mechi hii

Kabisa, maana ianyoonekana mechi ijayo na Leicester ndio itaonesha muonekano wa nani atakuwa bingwa. Tottenham watacheza na Man City.

Mpira ni mapumziko sasa.

Bournemouth 0 Arsenal 2
 
Gap kubwa sana hii ya magoli, inabidi kupunguza kwa mechi hii
Tofauti ya magoli sio threat sana, kati ya Araenal, leicester na Mancity sidhani kama goal difference ndo itaamua, tottenham wana mecho zilizobaki ngumu zaidi ya Arsenal, tottenham kwangu naona wamemshikia tu mtu hapo, watashuka.
 
Arsenal wapo mapumziko wakiwa mbele kwa goli 2-0

Wametawala mchezo ingawa Bournemouth nao wamejaribu mara kadhaa kutafuta magoli.

Arsenal wanaweza tu kupoteza magoli hayo kama hawatakuwa makini na Benik Afobe na pia kama walinzi wake watajisahau kidogo.

Bournemouth kwa voyote vile watafanya mabadiliko kipindi cha pili.

Ila yote ni kwamba Bado Olovier Giroud na Alexis Sanchez nao bado hawajafunga.

Tusubiri kipindi cha pili.
 
Arsenal wapo mapumziko wakiwa mbele kwa goli 2-0

Wametawala mchezo ingawa Bournemouth nao wamejaribu mara kadhaa kutafuta magoli.

Arsenal wanaweza tu kupoteza magoli hayo kama hawatakuwa makini na Benik Afobe na pia kama walinzi wake watajisahau kidogo.

Bournemouth kwa voyote vile watafanya mabadiliko kipindi cha pili.

Ila yote ni kwamba Bado Olovier Giroud na Alexis Sanchez nao bado hawajafunga.

Tusubiri kipindi cha pili.
Nakubaliana nawe, vijana wakiwa makini kutakuwa na magoli mengi zaidi Leo.
 
Kabisa, maana ianyoonekana mechi ijayo na Leicester ndio itaonesha muonekano wa nani atakuwa bingwa. Tottenham watacheza na Man City.

Mpira ni mapumziko sasa.

Bournemouth 0 Arsenal 2
Spurs hamna kitu, watashuka. Timu yenye mechi auheni ni leicester, wakikaa sawa! Ni kombe lao ila pressure ile yenyewe itawakuta tu.
 
Bournemouth wameanza vizuri kwa mpango wa kufanya mashambulizi mengi na Arsenal inabidi kuwa makini,

Inaonekana meneja wa Bournemouth Eddie Howe amezungumza kitu,
 
Bournemouth wanakwenda mbele kwa idadi kubwa huku Benik Afobe, Dan Gosling, Adam Smith na Ritchie wakiwa wanahaha uwanjani.

Dakika inakwenda ya 53

Bournemouth 0 Arsenal 2

Kona kwa Arsenal na inaokolewa na kipa.
 
Combo ya Ramsey na Flamini inagoma kwa mtazamo wangu na hii itakuja kutagharimu.

Unaweza kuwa sahihi lakini huenda Francis Coquelin akaingia usihofu.

Bournemouth wanafanya mabadiliko kwenye sehemu ya kiungo (kwa kudhani Arsenal hawaoni hio)

Josh King na Junior Stanislas wanaingia badala ya Gosling na Matt Ritchie
 
Arsenal wanafanya mabadiliko OX anatoka na Francis Coquelin anaingia.

Hivyo Arsenal wana viungo watatu huku Ramsey akishambulia mbele yao na nyuma ya Giroud kwa upande wa kulia.

Dakika inakwenda ya 65
 
Bournemouth wanafanya mabadiliko kwa kumuingiza mshambuliaji Lewis Grabban badala ya Benik Afobe
 
Bournemouth wanaonekana kukata tamaa na Arsenal inaelekea kunyakua point zote tatu.

Arsenal wanafanya mabadiliko na Kieran Gibbs anaingia badala ya Alexis Sanchez

Dakika inakwenda ya 81
 
Bournemouth wanafanya mashambulizi na kidogo wafunge lakini wanapoteza mpira.

Inabakia kuwa Bournemouth 0 Arsenal 2

Dakika inakwenda ya 88
 
Kwa hizi sub inaonyesha AW ameridhika na matokeo yaliyopo aaaagggghrrrrr

Nafikiri Arsenal wanajiandaa kwa mechi na Leicester Emirates Jumapili ijayo.

Hivyo uchezaji wao wa leo una handbrake.

Si Giroud wala Sanchez walocheza sana lakini ni kwa maelekezo maalum.
 
Natamani mpira uishe maana sipati burudani bali pressure tu. .hizi point 3 muhimu sana
 
Back
Top Bottom