Richard
Platinum Member
- Oct 23, 2006
- 16,635
- 25,612
Mkuu uko america nn? habari za asubuhi wenzio huku saa 8 mchana dsm jua kaliii..!
Tukirudi kwa asenali na wenga wetu kiukweli mi nishamchoka huyo mzee.Kwann anasubiri mpk dkk mbaya kama hizi ndio aanze kuleta habari za kumsajili mshambuliaji na kiungo mkabaji.?toka msimu uliopita kila mwenye macho alikua anaona mapungufu ya arsenal,mpk wachezaji wenyewe wakawa wanasema wanahitaji kuongezewa nguvu (refer cazorla), but wenger kama kawaida yake ni kutia pamba masikioni tu.
Leo ligi imeanza mechi ya tatu tumeshaachwa pointi 5 na gd 9 na mancity,hata kama tutajidanganya bado mapema ukweli ni kwamba arsenal haina ubora wowote wa kushindana na mancity na chelsea msimu huu labda itokee miujiza.
Hapana mkuu, nilipokuwa naandika wakti ule huku nilipo ilikuwa ni asubuhi.
Sasa napenda kuwahakikishia kuwa Arsenal watafanya usajili ila itakuwa ni kati ya Ijumaa na jumanne ijayo.
Meneja mwenyewe Wenger amesema kwamba Arsenal wapo sokoni na akipatikana mchezaji mwenye ubora unaotambulika basi watasajili.
Wenger ameishagundua kwamba Arsenal safari hii watapata tabu sana kushinda mechi zote iwe na timu za kawaida au zile kubwa kama Man City.
Ila meneja mzee Wenger ana tatizo na upangaji wa timu na hii imeonekana kwenye meci zote tatu zilizokwishachezwa.
Timu inayotakiwa kuwa inaanza mechi zote za ligi kuu ni ile timu ilianza kuceza mechi na Chelsea kwenye kombe la ngao.
Yaani Walcott anatakiwa aanze mbele, Oxdale Chamberlain pembeni, Ozil namba 10, Cazorla katikati akipanga vyumba. Nyumba kunakuwa na Ballerin kulia na Monreal kushoto. Kati Mertesacker na Cosy.
Tuna mechi ngumu zinakuja na tunaanza na Newcastle, halafu Stoke, Chelsea na Tottenham Hotspur.