Taaratibu tunasonga mbele. Carlzora mechi chache zilizopita naona amerudi kwenye yule carlzora tuliyemtoa Malaga, safi kabisa. Alexis kama kawaida, The Ox anakimbiza watu na huyu dogo Couqlin jana kanikosha. Kwa ujumla wachezaji wote walikuwa poa jana. Hii timu inahitaji marekebisho kidogo ili tuwe serious title contender, na pia nimefurahi Babu kiasi fulani anabadili badili angalau ktk tactics. Jana tulikuwa physical kidogo. Kikawaida Le prof hata kama tunaongoza moja dk za majeruhi huwa ana-encourage open game, ila mechi ya Qpr na jana naona dk hizo akaweka wakabaji wengi. Tulikuwa defensive minded ila deadly on the counter attack. Big Sam amekuwa akimsumbua sana Le prof kwenye mechi za "rugby", ila kwa jana ali-match naye. Pia Wamshukuru Adrian la sivyo ingekuwa zahma kwao. Next, St. Marry's. Pagumu ila tutatoka tu maana hata Upton sio kwepesi ila tumetoka na pts 3 muhimu.
Mkuu Sauthampton tuliwaachia carling cup, then tukawapiga kwenye EPL na sasa tunkwenda kuwabamiza hawatupi shida na chichi hatuna ugomvi nao wachezaji wengi tu tumenunua kutoka kwao , Theo, Ox, Chambers etc una kumbuka mlichema nini kwa West ham ambao walipanga timu dhaifu dhidi yenu? Kos is back, Ozil atakuwa bench .... jongea tu siku ya kitale. COYG
tukishinda game ya alhamis na wale kunguni waendlee kutoa sare zao itakuw poa sana
Bad first day of the year. Kulaleki tunahitaji zaidi ya beki na kiungo. Huyu Selfie taking kipa wetu huwa simwamini(sio leo tu) jamaa katu-cost sana, goli la kwanza kanikumbusha Almunia . Anyway, bado kuna mechi kibao tunaweza kurudi juu (Champions league) spots. Kikubwa tunatakiwa kurudisha wachezaji wetu wote walio majeruhi. Leo tuliokosa wachezaji 12 kitu ambacho nadhani hakuna timu yoyote iliyoweza kukipata msimu huu.
Ebu wataje hao wachezaji 12....ina maana mlikosa timu nzima?
Szczesny, Debuchy, Mertesacker, Koscielny, Gibbs, Coquelin, Chambers, Oxlade-Chamberlain, Cazorla, Rosicky, Alexis....hii ndiyo ilikuwa starting eleven ya leo...sasa katika hao 12, ina maana timu iliyocheza leo ni timu B ama C?!?
Goons kwa sababu siwawezi...anyway, hongereni kwa kuanza mwaka mpya na mambo mapya....
Lol sijatoa kisingizio wala sababu ya kufungwa. Tumefungwa fair and square sababu kubwa ni uzembe wa kipa wetu. Ndio tulichofungiwa. Hata hivyo huwezi kutozingatia idadi ya wachezaji tuliowawakosa leo. Kama wangekuwepo inawezekana mechi ikawa tofauti au la. hatutaweza kujua kama wachezaji hawa wangeweza kubadili sura ya mchezo au kutobadili, ndicho nachosema.
Wachezaji waliokosekana leo kwa ujumla, keyword UJUMLA ni hawa Welbeck, Ramsey, Arteta, Wilshere, Ozil, Gnabry, Ospina, Giroud(suspended), Sanogo, Podolski, Flamini, Diaby. Wengi wao ni maumivu/Majeruhi, wachache ni match fitness na suspensions. Idadi inasikitisha kwa kweli. Medical team yetu itakuwa imetoka chuo cha afya Muhimbili.