RRONDO usipotee Leo bhana Au usijifiche ukaja baada ya mpira...!
Hakuna wakoloni waliyokuja hapa na wakatulazimisha kuvipenda hivi vilabu vya ulaya…bali sisi wenyewe tulianza kuvutiwa na kuanza kuipenda hii ligi miaka ile DTV,CHANNEL TEN na baadae DSTV walipoanza kutuonyeshea live.
Ila hizi dini tuliletewa…wengine walituletea hizi dini kwa kutumia mashuwa na wengine wakatuletea kwa meli.
Jon Champion
"The final whistle is blown
arsenal win the match
3-0"
Jon Champion
"The final whistle is blown
arsenal win the match
3-0"
arsenal haijaifunga timu yoyote iliopo juu ya top 10 msimu huu.....katika mechi 14 zilizopita za mashindano yote arsenal kamfunga man utd mara moja tu! jiongeze.
Manchester united imecheza ucl misimu 20 mfululizo jiongeze
man utd imeshinda TWO UCL TITLES and ARSENAL has won ZERO UCL.....Arsenal has never beaten MAN UTD in UCL and man utd imeifunga arsenal at least mara mbili kwenye UCL. JITOE HUU MZIKI MNENE SHINDANA NA TOTTENHAM.
mkuu..naangalia mpira kibanda umiza,sina DSTV halafu jf naingia kwa kutumia pc sio simu. kwahio kuniona hapa ni mpaka mpira uishe labda niwe naangalia home CL kwa hisani ya TBC2 ndio nitakuwa jf kupiga porojo...kwahio usifikiri huwa nakimbia
Naipenda Arsenal na nimeifia Arsenal kwangu mimi Arsenal ni Dini niko teyari kubadili hizi dini walizotuletea wakoloni na kuhamia kwenye dini nyingine,lakini siko teyari na haitokujatokea eti niihame Arsenal kwenda timu nyingine.Noo!
Ila linapokuja swala la Arsenal kucheza na Manchester United ushabiki na upenzi wote huwa naweka pembeni na naziaacha akili zangu zifanye kazi bila kuendeshwa na hisia namaanisha LEO ARSENAL HATUWEZI au HAIWEZI KUIFUNGA MAN U kwani Arsenal ikikutana na Man U ni kama mbwa kamuona chatu'hata kama Man U wakipanga kikosi cha pili ni lazima watufunge tu.
Ushindi wa Arsenal leo labda ni droo au tuombe Mungu mchezaji mmoja wa Man United atolewe kwa kadi nyekundu mapema sana tena kwenye kipindi cha kwanza na huenda tunaweza shinda lakini hawa jamaa wakiwa kamili ni lazima tutachezea kichapo au tumejitahidi sana droo TIME WILL TELL
BAK, najuwa umeisoma comment yangu ya utabiri pale juu lakini umeamuwa kunipotezea kwa kile nilichokisema.Leo Mkuu tukichapa mtu tatu bila, basi kibarua cha Van Girl kinaota manyasi, kikubwa katika mechi hii ya leo ni kuingia uwanjani kwa confidence ya kwamba YES WE CAN BEAT MANU na pia kuhakikisha tunapata at least goli mbili za haraka haraka kabla ya HT badala ya kusubiri yale magoli ya lala salama kwenye dakika za nyongeza. Umeuona uzi wetu Mkuu? Kama sikosei huu ndio utakuwa uzi wa kwanza hapa JF kuangaliwa na watu milioni moja, ule wa Kombe la dunia 2014 ulikaribia lakini haukuona ndani.