Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

dia nimefurahi jana
warest in peace tupumue hawa jamaa wekundu.....

teheteeteetehetehhh wenye timu wakikusikia we acha hiyo muneno kamoja tu mbina wanataka kupotezaa wasaa kamoja tu..
 
Kama niliyowahi kueleza huko nyuma kwamba usajili wa Podolski ulikuwa "iminent" mchezaji huyo amekubali kutia saini mkataba na timu ya Arsenal FC ya Uingereza.

Baada ya kukamilisha usajili wa Lucas Podolski, Arsene Wenger sasa anashughulikia suala la usajili wa Jan Vertonghen ambae ni beki wa Ajax Amsterdam na timu ya taifa ya Belgium na ikiwa mambo yatakwenda vizuri usajili muhimu utakamilika kwa kumsajili mchezaji wa kiungo wa Rennes ya France Yann M' Villa.



Vertonghen amebakiza muda mfupi kwenye mkataba na Ajax na ikiwa mipango yote itakwenda uzuri basi mchezaji huyo atajiunga na beki mwenzie wa Belgium thomas Vernaelen.

Arsenal wanategemea kumsajili mchezaji huyu kwa kiasi cha paundi milioni 7 tu.

Usajili wa Podolski umegharimu kiasi cha paundi milioni 11 na mchezaji huyo atajiungana wenzake baada tu ya kumalizika kwa michezo ya Euro 2012.

article-2137594-12DB3F76000005DC-259_468x632.jpg

Lucas Podolski akiwa na jezi ya Arsenal.

Usajili wa Arsenal mwaka huu umekuja kwa kuhofia kuchelewa kupata wachezaji ambao ni muhimu kwa baadhi ya sehemu za uchezaji wa timu hiyo hasa kwenye ulinzi, kiungo na ushambuliaji na Arsene Wenger ameona ni bora kufanya biashara mapema asubuhi.

Yann M' Villa anatarajia kugharimu kiasi cha paundi milioni si chini ya 18 na hata timu za Man Utd na Tottenham nao wanaangalia maendeleo yoyote yanayotokea.
Yann+M%27Vila+gestures+during+the+French+cup+football+match+Rennes+against+Nancy


Yann M' Villa

Hopefully kama mambo yatakwenda kama yanavyopangwa basi Arsenal itakuwa ni timu pekee ambayo ina rasilimali ya wachezaji wengi wa viungo akina Alex Song, Jack Wilshere, Mikel Arteta, Aaron Ramsey, Tomas Rosicky na Alex Oxlade-Chamberlain.
 
Ushindi utatuweka pazuri, kipigo na draw bom, kazi nzito kwa vijana wetu leo.
 
Starting eleven

Szczsney

Sagna, vermealen, Koscielny, Gibbs

Song, Ramsey, Rosicky, Benayoun, Gervinho

Van Persie

Substitutes
Park, Oxlaide, Santos, Djourou, Chamakh, Conquelin, Fabianski


mku rejao naona leo atatusoma kama guest User!
 
Nakubaliana na Rejao...hapa kipa hatuna! Goli la kizembe sana hili.
Arsenal 1, Norwich 1
 
Yaani kipa katulostisha kimtindi. T'ham wanakuja fasta sana yaani kushindwa kushinda hii game itakua big blow. May be AW may be ataliona hili mapema.
 
gervinho haelewani na sagna.. benyoon anapoza saana
 
song nayeye ana bore sana.. sehemu ya kufunga anatafuta pasi...
 
kama AW anataka kushinda hii game inabidi afanye mabadiliko mapema kipindi cha pili kwa kumtoa muisrael au gervinho na kumuweka Ox ili dogo aongeze mashambuli mbele
 
kama AW anataka kushinda hii game inabidi afanye mabadiliko mapema kipindi cha pili kwa kumtoa muisrael au gervinho na kumuweka Ox ili dogo aongeze mashambuli mbele

Huyo Ox sijui kamtukana Wenger mazoezini, naona anachuniwa kinoma.Baada walcott kuumia watu walijua Ox ndio atachukua namba na anaweza kuleta mashambulizi lakini Wenger haoni hilo.
 
Back
Top Bottom