Mmawia
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 122,521
- 96,267
Kwenda CCM ilikuwa ni zuga tu,lengo lake ni kwenda ACT migebuka.
Kule ataenda kufa na njaa maana shida yake ni ubunge
Kwenda CCM ilikuwa ni zuga tu,lengo lake ni kwenda ACT migebuka.
Ndio ataisoma kwa shida ya vumbi
Hapo sasa itambidi aangalie chama kisicho na mgombea hapo kwenye hilo jimbo,na siasa ilivyo ya ajabu tusishangae aka win
Wasaka tonge utawajua tu kwa matendo wanataka wao ndio wawe washindi kila uchaguzi hawaamini kama wapo wengine ,wakishindwa hukimbilia kwingine,tatizo sio vyama,vyama havipigi kura ,kura inapigwa na wale waliokuchagua hao ndio wakiona umekuwa zigo wanakutosa ,matokeo wasaka tonge hubadili vyama kama vile wanavyobadili vyupi.Mbona kuatapatapa hivyo. Utulivu hana.
Mzee ALFI tulia Mkuu CCM ina mpango Wa kukupa UKURUGENZI Wa Halmashauri ya MILELE?
Mzee ALFI tulia Mkuu CCM ina mpango Wa kukupa UKURUGENZI Wa Halmashauri ya MILELE?
Aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Tanzania Bara, Ndg.Said Amour Arfi ambaye alijiunga na Chama cha mapinduzi (CCM) hivi karibuni amesema anafikiria kujiondoa CCM na kujiunga na chama kingine cha upinzani (hakukitaja jina), kwa kuwa hakuna demokrasia ya kweli ndani ya CCM.
Akizungumza na Mwandishi wa Habari hii kwa njia ya simu, Arfi amesema alijiondoa CCM mwaka 2000 na kujiunga na TLP kwa sababu CCM haikua na demokrasia, hivyo alitegemea miaka 15 aliyokaa nje ya CCM ingeweza kuibadilisha lakini hadi sasa hali ni ileile.
Arfi alitupwa nje kwenye kura za maoni ndani ya CCM kupitia jimbo la Mpanda Kati ambalo ameliongoza kwa miaka 10. Hata hivyo anafikiria kutetea kiti chake hicho cha ubunge kupitia chama kingine nje ya CCM. Watafiti wa masuala ya siasa wanasema huenda akajiunga na ACT wazalendo.
Arfi alikuwa mwanachama wa CCM hadi mwaka 2000 alipoondoka na kujiunga na TLP. Mwaka 2005 alijiondoa TLP na kujiunga CHADEMA ambapo alipata fursa ya kugombea Ubunge na kushinda kwa vipindi viwili mfululizo.
Mwaka huu alijiondoa CHADEMA na kurudi CCM, lakini ameangushwa kwenye kura za maoni na hivyo anafikiria kuondoka CCM na kujiunga na chama kingine cha upinzani ambacho hakukitaja.
Mchumia tumbo tu huna hana mbongo ya kuchanganua mambo.