App Mpya ya JamiiForums - Agosti 2026

App Mpya ya JamiiForums - Agosti 2026

Wakuu,

Nachukua fursa hii kuwafahamisha kuhusu ujio wa App Mpya ya JamiiForums!

Hii sio update ya kawaida, bali tumeisuka upya kuanzia chini. Haya ni baadhi ya mambo mapya (features):

Brand-New Interface (Muonekano Mpya kabisa) - Tume-design app iwe cleaner, faster, na more readable. Tumezingatia suala la mobile-first experience. Kusoma nyuzi (threads) sasa hivi ni rahisi na haichoshi macho. Ukiitumia utaelewa naongelea nini.

View attachment 3647685
View attachment 3647686
View attachment 3647688

JamiiCheck Imerahisishwa - Tumeongeza sehemu maalum (dedicated place) kwa ajili ya mada zote zilizofanyiwa fact-checking. Sasa itakuwa rahisi sana kuziona taarifa zilizochakatwa JamiiCheck.

FichuaUovu Katika Feed Moja - Kwa wale wapigania haki, sasa unaweza kuwasilisha KERO, DOKEZO au HOJA na kufuatilia uwajibikaji wake. Aidha, imekuwa rahisi kuona submissions zote kutoka kwa wadau kwenye feed moja.

Switch Regions (Chagua Nchi Yako)

JamiiForums inakua, hivyo kila tutakapokuwa tunatoa huduma patahitaji kuhudumiwa bila kuingiliana! Sasa unaweza kuchagua nchi yako (Tanzania, Kenya, Rwanda, Uganda, n.k.) na kuona trending discussions zilizo karibu na wewe. Tunalenga kurahisisha mijadala ya eneo flani kujadiliwa kwa lugha wanayotaka bila kuingiliana.

Smoother Threads - Kwenye nyuzi ndefu (huge threads), sasa unaweza ku-jump kwenda kwenye post ya kwanza, ya mwisho, au pale ulipoishia kusoma (last-read post) kwa click moja tu. Pia, replies zitakuwa zina-load automatic kadri unavyo-scroll chini (infinite scroll). Mfumo wa replies umebadilishwa.

Composer Mpya (Eneo la Uandishi limeboreshwa) - Sehemu ya kuandika mada au comments imesukwa upya. Tumeleta rich text editor yenye BBCode inayoendana na App. Ku-format maandishi yako, ku-upload picha (images), na kuweka files sasa ni seamless kwa sasa.

App tayari ipo hewani. Fanyeni ku-update au ku-download, kisha mtupatie feedback. Maoni yenu ni muhimu sana ili tuendelee kuiboresha zaidi.

MSISITIZO: Feedback itasaidia kuondoa kasoro zitakazoianishwa na kuiboresha zaidi App ili iweze kurahisisha upatikanaji na matumizi ya JamiiForums.
Umekua muongo muongo kama Lucas Mwashambwa

Mmenisumbua na kimuhemuhe kwenda playstore kudowload halaf nakuta hakuna kitu

Kila jukwaa liwe na moderator wake
 
Hakuna App inaitwa JamiiAfrica. Kama ipo, si yetu.

Hapa upo JamiiForums; ni tofauti na JamiiAfrica.
Nauliza kwakuwa kuna wakati iliandikwa humu kuwa Jamiiforums inabadilishwa kuwa Jamiiafrica

AI Overview

1786376030990.png



JamiiForums imebadilisha jina na kuwa JamiiAfrica ili kutanua wigo wa huduma zake na kufikia wananchi wengi zaidi barani Afrika. Licha ya mabadiliko haya ya jina la taasisi, jukwaa lenyewe linaendelea kutumia jina lake la zamani la JamiiForums katika shughuli zake za kila siku. [1]

Sababu na Malengo
    • Kutanua wigo wa huduma na ushawishi nje ya Tanzania.
    • Kuimarisha uwajibikaji na upatikanaji wa taarifa sahihi.
    • Kukuza sauti za wananchi kupitia mijadala huru.

Hali Halisi ya Jukwaa
    • Jina la JamiiForums bado linatumika kwenye tovuti na mifumo ya mijadala.
    • Huduma na kanuni za uendeshaji ziko pale pale.
    • Taasisi mama sasa inatambulika rasmi kama JamiiAfrica.
 
Hongera sana Maxence Melo kwa maboresho , hongera pia mkuu kwa kuwa vision mpya kila leo kulingana na mahitaji.
Sija update bado ila kuna kitu nakifikiri kama kinawezekana , kwa mfano ninataka kuona ama kupata mada za 2020 ama 2008 ama 2026 nk..
Kuwe kuna namna ya kupata mada ya tarehe na mwaka fulani kwa urahisi .



Yote ya yote hongera sana na pongezi nyingi kwa maboresho ya kila mara kulingana na nyakati na mahitaji.
 
Hongera sana Maxence Melo kwa maboresho , hongera pia mkuu kwa kuwa vision mpya kila leo kulingana na mahitaji.
Sija update bado ila kuna kitu nakifikiri kama kinawezekana , kwa mfano ninataka kuona ama kupata mada za 2020 ama 2008 ama 2026 nk..
Kuwe kuna namna ya kupata mada ya tarehe na mwaka fulani kwa urahisi .



Yote ya yote hongera sana na pongezi nyingi kwa maboresho ya kila mara kulingana na nyakati na mahitaji.
Nimeipenda hii
 
Back
Top Bottom