Anguko la Upinzani nani alaumiwe?

Anguko la Upinzani nani alaumiwe?

Vipimo vya great thinker ni Vipi Mkuu koko mbwana
Hivi Kawe na wewe ni great thinker? Forum imeingiliwa kwa sasa! Yani unaandika vitu ambavyo vipo chini kabisa ya viwango vya kufikiri.
Hivi ni kweli vyama vya upinzani vimeanguka? Hivi hufahamu kabisa wanayokutana nayo wakati wakitaka kufanya wajibu wao kama wanasiasa?
 
Basi inaweza kuwa vyama tulivyo navyo vina mapungufu Mengi
UPINZANI HAUFI MKUU. ILA VYAMA TAWALA NDIO VINAANGUKA, UPINZANI SIO CHAMA, UPINZANI NI WATU, CHAMA NI KAMA NJIA TU AMBAYO LEO INAWEZA KUFUNGULIWA WATU WAPITE KESHO IKIFUNGWA WATU WASIPITE WATU WATATFUTA NJIA NYINGINE YA KUPITA.

UPINZANI NI WATU. WATU WAKIISHA DUNIANI BASI UJUE NA UPINZANI NDIO UTAISHA BUT NOT OTHER WAY AROUND.
 
Tume huru itasaidia wapinzani kushinda?
Tumesikia leo Mhs Mkapa anasema kuwe na tume huru ya uchaguzi na uchaguzi huru.
Hapo utajua kama upinzani upo au umekufa, weka tume huru ya uchaguzi!!
Ufanyike uchaguzi huru!!
 
Mkuu hoja zako zinaweza kuwa na mashiko au zikose mashiko

Unajua kuwa waliojiandikisha 2019 ni wengi zaidi katika historia ya Uchaguzi wa Serkali za mitaa
Tuchukue uchaguzi mdogo kama case study kuweka mizani juu hojaza hizi.

Hebu fikiri, wakati inasemwa ati chama tawala kinafanya vizuri kiasi kwamba upinzani unaishiwa pumzi ni katika kipindi hiki hiki ambacho watu wanahamasishwa na kubembelezwa kujiandikisha ktk daftari la kura ili wapige kura, hiyo ni kujiandikisha tu achilia mbali bado kupiga kura.


Najiuliza, hivi hawaoni mazuri ya chama tawala watumie fursa ya kijiandikisha kwa wingi ili waunge mkono juhudi na mema ya serikali hii tukufu ili kuwamaliza wapinzani kabisa tena kabla ya 2020??

Nilitarajia kuwe na mwamko kuliko kipindi kingine chochote cha watu kwenda kujiandikisha, maana sasa hivi mema ni mengi yanayosemwa kuliko awamu nyingine yoyote iliyowahi tokea nchini, la hasha! mwamko ni mdogo huenda kama zamani, kwanini???
 
Waliposema lowassa mtu safi wakati walisemaga ni fisadi. Tangu siku hiyo sitaki kusikia upuuzi unaoitwa upinzani nchi hii
 
Je kuanguka na kupoteza ushawishi kwa vyama vya upinzani nani alaumiwe?

Tukizungumzia Upinzani kwa miaka 15 mfululizo tunawazungumzia chadema

Hawa ndio walikuwa wanawavuruta wenzao

Lakini toka awamu ya tano iingie madarakani ni km wameishiwa pumzi kwa lugha ya mtaani tunasema wamekuwa kama mbwa mwenye mapengo hata wakibweka sauti inarudi tumboni

Je walikosea wapi mpaka kupoteza ushawishi? Je nini kifanyike waweze kuaminika tena?

Je wanaweza wakapotea kabisa 2020 na TLP kikaibuka kama chama kikuu cha upinzani?

Tuwashauri Wapinzani walijikwaa wapi? Ili waweze kwenda sawa na mchapa Kazi Rais Magufuli
Anayepuuza matakwa ya kikatiba ya vyama vingi na pia kupuuza sheria ya vyama vya siasa ikiwemo haki ya kufanya mikutano ya kisiasa na kandamana pamoja na kutoa maoni huru ndiye wa kulaumiwa kwa anguko unaloliongelea mkuu.
 
Je kuanguka na kupoteza ushawishi kwa vyama vya upinzani nani alaumiwe?

Tukizungumzia Upinzani kwa miaka 15 mfululizo tunawazungumzia chadema

Hawa ndio walikuwa wanawavuruta wenzao

Lakini toka awamu ya tano iingie madarakani ni km wameishiwa pumzi kwa lugha ya mtaani tunasema wamekuwa kama mbwa mwenye mapengo hata wakibweka sauti inarudi tumboni

Je walikosea wapi mpaka kupoteza ushawishi? Je nini kifanyike waweze kuaminika tena?

Je wanaweza wakapotea kabisa 2020 na TLP kikaibuka kama chama kikuu cha upinzani?

Tuwashauri Wapinzani walijikwaa wapi? Ili waweze kwenda sawa na mchapa Kazi Rais Magufuli
sema anguko la ccm laja nani alaumiwe?
 
Je kuanguka na kupoteza ushawishi kwa vyama vya upinzani nani alaumiwe?

Tukizungumzia Upinzani kwa miaka 15 mfululizo tunawazungumzia chadema

Hawa ndio walikuwa wanawavuruta wenzao

Lakini toka awamu ya tano iingie madarakani ni km wameishiwa pumzi kwa lugha ya mtaani tunasema wamekuwa kama mbwa mwenye mapengo hata wakibweka sauti inarudi tumboni

Je walikosea wapi mpaka kupoteza ushawishi? Je nini kifanyike waweze kuaminika tena?

Je wanaweza wakapotea kabisa 2020 na TLP kikaibuka kama chama kikuu cha upinzani?

Tuwashauri Wapinzani walijikwaa wapi? Ili waweze kwenda sawa na mchapa Kazi Rais Magufuli
Wewe sishabiki kindaki wa ccm ebu tueleze
 
Mi naona upinzani upo imara na kamwe hauwezi kufa. Kukiwa na fursa sawa za kisiasa kati ya CCM na Upinzani. Ni wazi CCM kitatoweka kama ilivyokuwa KANU ya Kenya.
Endelea kuota ndoto za jioni.
 
Mkuu hoja zako zinaweza kuwa na mashiko au zikose mashiko

Unajua kuwa waliojiandikisha 2019 ni wengi zaidi katika historia ya Uchaguzi wa Serkali za mitaa
Kihisabiti na kinadharia, jibu ni rahisi waliojiandikisha ni wengi sababu mwaka huu idadi ya waliokidhi vigezo vya kupiga kura ikiwa pamoja na waliotimiza umri wa miaka 18 imeongezeka haiwezi kuwa sawa ama linganishwa na miaka mingine.

Kiuhalisia, hao watu wanaodaiwa kwamba wamejiandikisha wengi kuwahi pata tokea ni baada ya kuongeza muda kutokana na hamasa kuwa ndogo.

Tena tunasema ni wengi huenda ni sababu ya malengo ambayo TAMISEMI walijiwekea kutimia lakini yumkini watu walipaswa kuwa wengi zaidi tena bila hata ya kuongeza muda.


Sasa tusubiri tuone hamasa ya kupiga kura tuone itakuwa kubwa licha ya upinzani kususia???

Je watu watajitokeza kupiga kura kwa mapenzi ya dhati na kwa wingi kuunga mkono mema ya mwenendo wa nchi ilihali kujiandikisha tu ilikuwa changamoto.
 
Watu wameanza kuwachoka wapinzani Mkuu tujiulize wapi walipokosea

Watu wepi hao wameuchoka upinzani?

Una takwimu?

Tuwekee takwimu wazi hapa!

Takwimu ya kweli ni approval rating ya mawe ni below 43% according to utafiti wa Twaweza!

Na huo utafiti mawe ilimuua mpaka kamnyang’anya CEO wa Twaweza passport!

What a loser!
 
Back
Top Bottom