Wana JF.
Chama cha Demokrasia na Maendelo (Chadema). Kimejipa jina hilo maudhui makuu katika jina hilo, ni mawili tu.
Demokrasia na Maendeleo.
Demokrasia kwa maana ya fursa kwa mwanachama na kiongozi wake asiyeweza kuipata katika chama kingine chochote kile nchini, fursa ya kushiriki katika maamuzi muhimu ya chama.
Maendeleo kwa kila Mtanzania, yanayotokana na mgawanyika sawa wa rasilimali za taifa hili.
Leo chama hicho kinapata mamilioni kwa ajili ya maendeleo ya chama kupitia ruzuku ya Serikali, lakini mamilioni yote hayo hatuoni yanavyoendeleza wanachama wake, achilia mbali chama chenyewe hicho.
Unapoandika allegations kama hizi uwe na facts. CCM ndio wanaopata mabilioni. Wao ndio wameshika dola, wanamamlaka na fedha yote inayotokana na mapato yote ya serikali. Je kwa ile ya ruzuku wanachama wake wanaendelezwaje? na ile ya serikali yake watanzania tunaendelezwaje? Au dio fasheni siku kukisema chadema tu hata kwa maelezo yasiyo na mashiko?
Watanzania wapenda amani wameishakuwa makini na Chadema kwamba chama hicho ni hatari kwa ustawi wa jamii.
Chama hatari kwa ustawi wa jamii hakistahili kuwepo kwa mujibu wa sheria. Sasa kama hayo ni kweli kwanini kipo au kwa nini msipeleke ushahidi huo kwa msajili ambaye pia ni wenu ili kifutwe? Tunajua zimaefanyika mbinu ya kutumia Polisi (JK alithibitisha hili kwa kusema CCM waache kutegemea Polisi). Goal ilikuwa hilo la mwisho wa siku ionekane CDM ni chama cha vurugu kichukiwe na watu na porobably ziwe ndizo grounds za kukifuta. Kule Mafinga anayeonekana anaua ni Polisi halafu mijitu kama wewe bila aibu mnajitahidi kuwaaminisha watanzania kuwa walioua ni Chadema. Inamaana hata wananchi walioshuhudia mnafikiri wajinga kiasi hicho?
Viongozi wanaounda Baraza Kuu na Kamati Kuu, ni wale waliokosa uvumilivu ndani ya vyama vya siasa walivyokuwamo mwanzo, wengi wao wakiwa wametokea CCM baada ya matamanio yao ya kupata madaraka waliyoyataka kukosekana huko, akiwamo DK. Slaa mwenyewe.
Unaonekana wewe ama unakariri, unaropoka bila kufikiri au unatake for granted kwamba Watanzania ni wavivu wa kufikiri na hawana kumbukumbu ya historia ya nchi yetu kama wewe. Labda nianze kwa kukuvua nguo kwa historia ya mfumo wa vyama vingi awamu ya pili (1992). Kabla ya 1992 Tanzania kulikuwa na Chama kumoja tu. hivyo ni ilikuwa ni lazima mtu awe mwana-CCM. Wanafunzi wa vyuo hawakupata admission au wamalizapo hawakupata ajira unless awe ni mwanachama wa CCM kwa kuthibitisha kuwa ana kadi. Sasa wakati vyama vingi vinaanza wewe akili yako inakutuma kuwa vyama vya upinzani vingetoa wapi wanachama kama si kutokana na pupolation ya watu hao hao? Au ulitaka watoke kenya au Uganda ili CCM wa-retain wanachama wao. Halafu ndugu yangu, hivi unajua hata maana ya Demokrasia? Ulitaka wale waliojiunga CCM huko zamani iwe ni marufuku kutoka either kwa kuacha kuwa mwanachama au kujiunga na vyama vingine? CCM mnaweweseka kwa sababu mshazoea na mna hang-over za kupora haki za watu kwa mgongo wa chama kushika hatamu, zidumu fikra za....... nk.
Ni wazi siku si nyingi anguko la Chadema tutaliona miongoni mwa hao watapatikana kina Yuda Iskarioti waliokata tamaa, na hilo ndiyo litakuwa anguko la Chadema.
Endelea kuota anguko hilo ila deep down unajua anguko linakunyemelea chama gani...