Anguko la CCM halizuiliki na linakaribia

Anguko la CCM halizuiliki na linakaribia

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
58,636
Reaction score
220,404
CCM kama ilivyo kwa waasisi wake TANU na ASP vilianzishwa ili kupigania uhuru wa mtu mweusi kutoka katika mikono ya weupe wachache. Ili kufanikisha hili ililazimu kuwaunganisha wananchi kwa njia mbali mbalimbali ikiwemo propaganda, viongozi wa jadi, viongozi wa dini nk.

Baada ya uhuru, lengo lilikua kusaidia nchi nyingine za Afrika kupata Uhuru. Vyama rafiki kama Frelimo, Swapo, ANC nk vilijiunga na sisi. Adui bado alikua ni Kaburu na Beberu. Kwa nia njema kutokana na uchaguzi wa nchi zetu, viongozi wetu waliamua kufuata mfumo wa Kijamaa ili kugawa kilichopo kwa watu wote sawa. Siasa za kijamaa zilitufanya kuwa wahanga wa Vita Baridi kwani tulikuwa upande wa Urusi na China. Mabeberu walituona ni tishio.

Nyakati zinebadilika, sasa hivi tunapigania mabadiliko ya kiuchumi na maisha bora. Mass Media imeleta mabadiliko makubwa. Vijijini watu wanafahamu kuwa wanaweza kuishi kwa umeme wa solar na wakavuna maji ya mvua na kuishi maisha bora zaidi. Mpinzani wetu si Kaburu tena bali ni sisi wenyewe tunataka kuishi maisha bora.

Propaganda za kutubagua na viongozi wa upinzani haziwezekani. Hawa viongozi ni ndugu zetu, tulijua nao, tulisoma nao na wengine ni ninamuonea zetu. Hawa si Makaburu wala si mabeberu. Kama vilivyoanguka vyama vingine vya siasa vilivyopigania uhuru. CCM haipiganii tena ukombozi.
 
Nimeahidi siku CCM ikifa au hata kuondolewa tu madarakani, ni lazima nifanye karamu nyumbani kwangu.

Kwa sababu mpaka kesho naamini, baada ya kifo cha CCM, nchi yetu itapiga hatua kubwa sana ya kimaendeleo.

Kwa hali ilivyo sasa, ni Wana CCM wachache pekee ndiyo wanao ifaidi keki ya Taifa vilivyo!
 
Kuna constructive critism upinzani wa Tanzania haujafikia huko wao ni kuporomosha matusi tu raisi unakuta hawamwiti mheshimiwa raisi wanamwita Jiwe hivi hata ungekuwa wewe ungewasikiliza?
 
kuna constructive critism upinzani wa Tanzania haujafikia huko wao ni kuporomosha matusi tu raisi unakuta hawamwiti mheshimiwa raisi wanamwita Jiwe hivi hata ungekuwa wewe ungewasikiliza?
Lakini Rais anapotoka hadharani ma kusema mimi ni Jiwe kweli kweli anaregemea mapokeo ya Raia wake yatakuwaje. Kwa kifupi uchaguzi unapofanyiwa figisu na wapinzani kukosa uwakilishi ni kujenga uhasama katika jamii.
 
Ila mm niseme kweli hiki chama changu pendwa kilishaanguka toka muda ila tunatumia dola kubaki madarakani tu, si unaona wenyeviti, madiwani, na wabunge si tuliwapitisha kwa mbeleko.
 
Lakini Rais anapotoka hadharani ma kusema mimi ni Jiwe kweli kweli anaregemea mapokeo ya Raia wake yatakuwaje. Kwa kifupi uchaguzi unapofanyiwa figisu na wapinzani kukosa uwakilishi ni kujenga uhasama katika jamii.
Kwani upinzani ulikuwa ukitetea jamii gani zaidi ya matumbo yao mbunge pekee upinzani aliyekuwa akitetea maendeleo ya jimboni kwake ni Mbowe tu. Wengine wote hakuna kitu akiwemi Lisu na Zitto kabwe nk.
 
kwani upinzani ulikuwa ukitetea jamii gani zaidi ya matumbo yao mbunge pekee upinzani aliyekuwa akitetea maendeleo ya jimboni kwake ni Mbowe tu .Wengine wote hakuna kitu akiwemi Lisu na Zitto kabwe nk
Ahha ndiyo maana aliwekwa afisa kipenyo kule Singida Mashariki baada ya Lissu kuvuliwa ubunge akiwa mgonjwa?
 
Shida si CCM kuanguka au kung'oka madarakani, shida ni je nani atakaeing'oa madarakani!?

Ukiangalia upinzani ulivyo yaani hawafikii hata nusu ya ubora wa CCM kuanzia ktk mfumo wa kidemokrasia, kiuchumi, wingi wa wanachama, rasilimali watu (hazina ya watu wenye ubora kiuongozi) nk

Mfumo wao wa Kidemokrasia utaona namna bora wenzetu CCM wanavyopokezana kiuongozi kwa mfano kuanzia mwaka 2005 mpaka leo hii 2021 wenzetu wameshakuwa na wenyeviti wa chama takribani WATATU (Mkapa, Jk, Jpm) pamoja na makatibu wasiopungua wanne,, ilhali ukija huku upinzani watu ni ving'aninizi wa madaraka kwa miaka yote wakiamini na kuwaaminisha wanachama kwamba wao pekee ndio wenye uwezo wa kuongoza hivi vyama.

Hvyo CCM inaashiria kwamba ina shehena ya talanta za kiuongozi ktk kila ngazi

Kwa kifupi pasipokugusia mambo mengine naomba niishie hapa, ila kwa aina ya upinzani dhaifu tulionao nchini basi itachukua miaka dahali kuiondoa CCM
 
Nahisi J.M.K atakuwa anaumia Sana kwa kuisusa katiba mpya, kwa jinsi mambo yanavyobadilika.

Enyi wanasiasa tuipiganie katiba mpya hata nyie mliopo huko CCM kwa maslahi mapana ya Taifa na uhuru wa kuamini siasa unazozihitaji kuliko kuendelea kuwa watumwa wa chama na kutoa akili zenu kwa ajili ya kumsikiliza mtu mmoja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kwani upinzani ulikuwa ukitetea jamii gani zaidi ya matumbo yao mbunge pekee upinzani aliyekuwa akitetea maendeleo ya jimboni kwake ni Mbowe tu .Wengine wote hakuna kitu akiwemi Lisu na Zitto kabwe nk
Kama mbowe alikuwa anatetea maendeleo jimboni kwanini jimbo lake "lilitakiwa" kwa udi na uvumba?
 
kuna constructive critism upinzani wa Tanzania haujafikia huko wao ni kuporomosha matusi tu raisi unakuta hawamwiti mheshimiwa raisi wanamwita Jiwe hivi hata ungekuwa wewe ungewasikiliza?
Alijiita mwenyewe Jiwe acha kujitoa ufahamu.
 
Alijiita mwenyewe Jiwe acha kujitoa ufahamu
Kujiita haikupi mandate ya wewe kumwita mheshimiwa raisi hivyo mfano umemtibua mzazi wako akasema mimi mwendawazimu nikilianzisha hapa mtahama nyumba utakuwa una mu adderess baba yako kama mwendawazimu? Kuwa ohhh wewe mwendawazimu nipe hela ya ada ya chuo nadaiwa? Sababu mwenyewe alijiita mwendawazimu?
 
Tatizo la Ccm nao wapo apudetedi wale uvccm wasingekuwepo labda ingekuwa rahisi sanaaaaa lakini kwa uwepo wao itaanguka ila sio hivi karibuni.....
 
Shida si CCM kuanguka au kung'oka madarakani, shida ni je nani atakaeing'oa madarakani!???

Ukiangalia upinzani ulivyo yaani hawafikii hata nusu ya ubora wa CCM kuanzia ktk mfumo wa kidemokrasia, kiuchumi, wingi wa wanachama, rasilimali watu ( hazina ya watu wenye ubora kiuongozi) nk

Mfumo wao wa Kidemokrasia utaona namna bora wenzetu ccm wanavyopokezana kiuongozi kwa mfano kuanzia mwaka 2005 mpaka leo hii 2021 wenzetu wameshakuwa na wenyeviti wa chama takribani WATATU (Mkapa, Jk, Jpm) pamoja na makatibu wasiopungua wanne,, ilhali ukija huku upinzani watu ni ving'aninizi wa madaraka kwa miaka yote wakiamini na kuwaaminisha wanachama kwamba wao pekee ndio wenye uwezo wa kuongoza hivi vyama

Hvyo CCM inaashiria kwamba ina shehena ya talanta za kiuongozi ktk kila ngazi

Kwa kifupi pasipokugusia mambo mengine naomba niishie hapa, ila kwa aina ya upinzani dhaifu tulionao nchini basi itachukua miaka dahali kuiondoa CCM
Mkuu tyc Nimeona.
 
  • Thanks
Reactions: tyc
Back
Top Bottom