Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Mwaka 2025, Android ilisafirisha simu 1,000,000,000 huku iPhone ikisafirisha 240,000,000, hivyo kwa idadi ya vifaa Android iko ligi tofauti kabisa. Hata hivyo, bei ya wastani ya iPhone ni dola 1,060 sawa na Tsh. 2.756 Milioni, ikilinganishwa na dola 370 sawa na Tsh 962,000 kwa simu za Android, jambo linalobadilisha kabisa taswira ya mapato.
Apple na Samsung zinadhibiti asilimia 40 ya mauzo ya simu janja duniani, ikionyesha kuwa soko limejikita zaidi kwa kampuni chache zilizo juu.
Hata hivyo, Nchini Marekani, iPhone ina umiliki wa asilimia 69 ya soko, hali inayompa Apple nafasi ya kuendelea kuuza bidhaa zake kwa bei ya juu
Maoni ya mdau
Hata hivyo, Nchini Marekani, iPhone ina umiliki wa asilimia 69 ya soko, hali inayompa Apple nafasi ya kuendelea kuuza bidhaa zake kwa bei ya juu
Maoni ya mdau
Apple Inc anamiliki simu (Kifaa) na Program Software (iOS) vyote ni vyake. Android hamiliki kifaa (Simu), vifaa (Simu/tablets) ni mali za watu wengine Samsung/Tecno/Infinix n.k.
Android anauza Software peke yake. Apple Inc lazima wawe na kipato kikubwa sababu wamedhibiti bidhaa zao, huwezi ipata iOS nje ya iPhone, lakini unaweza ipata Android nje ya Samsung/Tecno/Google pixel n.k.
Apple Inc lazima wauze bidhaa zao bei juu, sababu hakuna mbadala wa bidhaa zao (Yaan OS na Simu yaani iPhone). Android unaipata kwa wazalishaji wa simu wengi wenye kushindana.
Ingekuwa iOS inapatikana kwingine nje ya iPhone, kungekuwa na mbadala wa kifaa. Huna iPhone hujatumia iOS. Android is everywhere.