Andrew Chenge: Kwangu gamba limeishia kiunoni tu

Andrew Chenge: Kwangu gamba limeishia kiunoni tu

Hii kiburi chote mwisho wake September. hii itakuwa nafasi ya mwisho kwa wanamagamba kujisafisha. wakishindwa hapa tena then itakuwa kazi ya ziada kukirudisha chama 2015.
 
Hii kiburi chote mwisho wake September. hii itakuwa nafasi ya mwisho kwa wanamagamba kujisafisha. wakishindwa hapa tena then itakuwa kazi ya ziada kukirudisha chama 2015.

Hakuna kitu hawana lolote september watasema hadi january tena. Hongera gamba kiuno komaaaaa wasikuzingue
 
Mmoja wa wanaotakiwa na CCM kujivua gamba (kuondoka ndani ya chama) kwa madai ya ufisadi amelieleza mwanahalisi kuwa "kwangu gamba limeishia kiunoni,kuliondoa hapa lilipo sharti uje na shoka"Chenge alikuwa akijibu swali la mwandishi wa gazeti la mwanahalisi lililotaka kufahamu ni lini ataondoka katika uongozi wa chama chake kutokana na kutuhumiwa na ufisadi.

Nape Upo hapo?
Huyu anakiburi cha Sheria na analindwa na JK, kwa sababu JK alimtumia katika kumng'oa SITTA kwenye kiti cha usipika, ndiyo maana CCM na serikali wanamtetea kuwa siyo FISADI. Lakini Mkuu 40ID nakuhakikishia kwamba huyu mzee wa vijisenti kiboko yake ni makamanda wa CDM tu ndiyo wenyeuwezo wa kumng'oa, ngoja tusubiri uchaguzi Bariadi. Safari hii hatukufanikiwa yawezekana hatukuweka mgombea.
 
".........kwangu Gamba limeishia kiunoni kuliondoa hapa lilipo inabidi uje na Shoka"-Source Mwanahalisi la Leo kwenye Story ya JK KIGEUGEU
hivi kwanini Mafisadi hawataki kuwajibika? nawachukia sana, hasa huyu chenge na mapacha wenzake.
 
hivi kwanini Mafisadi hawataki kuwajibika? nawachukia sana, hasa huyu chenge na mapacha wenzake.
dah afadhali nimepata leo wa kumwuliza. Naomba unieleweshe ndugu yangu:
1. Mafisadi maana yake ni nini?
2. Ufisadi wa hao jamaa watatu ni upi?
3. Hakuna wengine waliofanya hayo ya jibu namba 2?
4. Kama wapo, wanaitwaje? Je watajivua gamba nao?
Asante
 
Chenge ana jeuri ya kufa mtu kwa sababu anao ushahidi kuwa JK naye alipata mgao wa fedha ya rada, hivyo hawezi kumfanya lolote vinginevyo anamwaga ugali, patamu hapo, JK unalo gamba hilo halivuki kama hutaki kunywa sumu ufe.
 
hivi kwanini Mafisadi hawataki kuwajibika? nawachukia sana, hasa huyu chenge na mapacha wenzake.


Unamwonea bure Chenge, wa kulaumiwa ni JK yeye ndiyo gamba kubwa kuliko yote baba wa ufisadi nchini
 
mbona hapa inaonekana mapacha watatu mi napendekeza katika mchakato wa katiba tumondolee kinga rais ili tupate mapacha watano
 
Dah! Hili jibu nimecheka sana. Sina hamu! Gamba hilo mpaka kulitoa lazima kuliendea si na shoka tu bali pia mwenye kulipiga shoka lazima awe jitu kwelikweli na shoka lenyewe lazima liwe limenolewa makali yake. Kwa lugha nyingine jamaa yuko tayari kufa na gamba lake. Loh!
 
kama anasema gamba lake lipo kiunoni haoni anatupa majoto wananchi kwani karaha zote za umeme na nyinginezo wamesababisha wao mapacha watano hili swala halitakiwi tuliweke kisiasa zaidi lipo kisiasa ndiomanaa wanajipangia wataachia madaraka lini kinachotakiwa tuwapeleke kisheria zaidi tunavyoongea hivi ilitakiwa wawe segerea ndio uchunguzi uendelee
 
hivi kwanini Mafisadi hawataki kuwajibika? nawachukia sana, hasa huyu chenge na mapacha wenzake.

We mwanaCCM nini? Sasa unajua kua ni Mafisadi, sasa unashangaa nini kuwa Hawawajibiki? Fisadi = Kutowajibika
 
Ahaa haaa haa Chenge bana anafurahisha sana,sasa alikuwa analivua kwa kwenda juu au chini? Chenge + Magogoni = Gamba la kobe.
 
Chenge ana jeuri ya kufa mtu kwa sababu anao ushahidi kuwa JK naye alipata mgao wa fedha ya rada, hivyo hawezi kumfanya lolote vinginevyo anamwaga ugali, patamu hapo, JK unalo gamba hilo halivuki kama hutaki kunywa sumu ufe.
kila nikisoma michango ya huyu william nashindwa kutofautisha na kinyesi.
This Again is KINYESI.
 
Hii kiburi chote mwisho wake September. hii itakuwa nafasi ya mwisho kwa wanamagamba kujisafisha. wakishindwa hapa tena then itakuwa kazi ya ziada kukirudisha chama 2015.

September kutakuwa na kitu gani tofauti (ukiondoa swala la ratiba) ambacho hakipo August?

Kikwete hata CCM wenzake wanamdharau sana.
 
Uongozi legelege na dhaifu huzaa huotesha viongozi wabinafsi na wenye kiburi. Kama uongozi ungekuwa makini katu hauwezi kumwagiza mkosa maadili ya uongozi eti ajiondoe mwenyewe. Tangu lini mkosaji au mwuaji akaenda kwa hiari kujisalimnisha kituo cha polisi?

Kuna kila dalili ya uongozi dhaifu na legelege wa CCM na serikali yake kama alivyokiri mwanasheria mkuu wa serikali wiki iliyopita akijibu hoja za Waziri Kivuli wa Chadema Mbunge Lema wa Arusha.

Ni nini kinawaogopesha serikali na CCM kuwawajibisha hao? Kwa nini wanawabembeleza na kuwakingia kifua wakati ni wahalifu na makosa yao yanajulikana?

Je Serikali na CCM wanaogopa kulipuliwa na hao mapacha watatu ndio maana wanawabembeleza hivyo wang'atuke kwa hiari yao?

Hapa kuna siri kubwa, lakini kuna siku yote yatafumuliwa ingawa yanajulikana.
 
wee chenge, sasa hilo gamba kiunoni linafanya nini, amua moja livue kabisa au ulivae vizuri mpaka usoni, hakuna hata atakaeshika shoka kukuvua kwa nguvu.
 
Back
Top Bottom