BRN
JF-Expert Member
- Nov 18, 2013
- 5,346
- 6,841
Hili ni jina la filamu ya kihindi iliyotoka miaka ya mwanzoni ya 1980 ikimhusisha mtaalamu Amitha Bachan.Kwenye filamu hii Amitha anahukumiwa kwa kosa la mauaji..kiukweli hakufanya kosa hila ila na uonevu tu ndio unafanya aonekane anahatia.Baada ya kutumikia kifungo na kutoka jela siku moja anakutana na mtu ambae alidaiwa kupoteza maisha yake,alichofanya Amitha ni kumwua mtu huyo mbele ya hakimu na kuieleza mahakama kwamba hana hatia kwani tayari alishatumikia kifungo. Naifananisha filamu hii na hali ilivyo kwenye mahusiano mengi kwa wakati huu ambapo wenzi hutuhumiana kwa kukosa uaminifu katika mahusiano kwa kubambikiziana kesi.Ikifikia hapo mwenza anaona aahh!! Kama anatuhumiwa kutoka nje ya mahusiano wakati sio kweli ni bora atoke tu na mtu mwingine nje ya mahusiano ili kuleta uwiano na tuhuma anazopata. Huo ni mtazamo wangu tu.