sanchez255
Senior Member
- Jun 9, 2015
- 171
- 312
basi ni noma sana maana wengine tuko dilema hadi hv sasa....safari haiko tena nnFungua moyo kijana utaingia tuu
najuavyo mm mtoto wa ndani ya ndoa haonyeshwi baba.pia uzalendo w nch yko huwez kufundishwa jkt hzoj fikra potof et ukipita huko huwez kula rushwa ingia ndan uone uozo
Wakuu mwenye kujua habari za JKT kujitolea 2015 Atujuze.
Mbona sisi tunaofanyiwa mipango mwaka huu wametuchelewasha kuingia kambini? Na wakati wenzetu mafunzo teali wameshaanza.. unakuta mtu anaekufanyia mipango yupo kule MMJKT anakwambia subiri utaingia!
Je kuna watu huwa wanaripot katikati ya six week?
Nilikua Nina pitia Website ya JKT nikakuta Wamegawanya makundi ya Vijana kwa sehemu mbili ..
Kundi la kwanza wamewaita Vijana wa kujitolea ambao ni wale wa kuanzia elimu ya darasa ya saba ambao wanahitaji wa kuanzia umri wa miaka 18 hadi 23
Alafu kundi la pili ni wale wa kuanzia kidato cha sita na kuendelea ambao umri wao ni miaka 18 hadi 35 ndio wanachukuliwa ..
Sasa hapa swali langu hawa ambao wanaoanzia kidato cha sita kwanini hawajaitwa wa kujitolea?? Hawa wa kidato cha sita Ina maana ukimaliza mafunzo na ukifanya vizur unakua muajiliwa wa JKT au inakuaje ? Na mikataba ya JKT imekaaje kwa askari wanaopewa mikataba?
Naomba kufahamishwa wakuu
jkt haiajiri.hayo makundii mawili yako hivi,
1.form six wanakwenda kufanya mafunzo kwa mujibu wa sheria.depo yako inakuwa rasharasha tu na huisha ndani ya miezi mitatu halafu uruhusiwa kuondoka kurudi majumbani kuendelea na vyuo etc.
2.vijana wa kujitolea ni wale wanaoenda jkt kwa mkataba wa miaka miwili.inakuwa hivi,unapiga depo miezi 6,baada ya hilpo depo la nguvu la miezi 6 mnagawanywa vikosi mbalimbali kwa ajili ya kwenda kufanya kazi za uzalishaji mali.mfano,kulima,ufundi,ushonaji etc.baada ya miaka miwili kuisha unapewa cheti na kurudi home ukaendelee kujitegemea.LAKINI ndani ya hiyo miaka miwili ikitokea ajira ya aina yoyote ile unaruhusiwa kwenda.mfano JWTZ inataka kuchukua watu kadhaa,itakuja huko makambini mliko au mtapelekwa kwenye kambi ambayo usahili utafanyika na mnafanya huo usahili,ukichukuliwa then good for you.polisi pia huja kuchukua huko,magereza,usalama wa taifa,tanapa,bandari,airport,etc.so ukibahatika unaweza pata ajira,usipobahatika utarudi nyumbani kujitegemea.
NB.nasikia pia kwa wale form six wa mujibu wa sheria kama atapenda kubaki ili kama ajira ikitokea ajaribu bahati anaruhusiwa ila sina uhakiaka na hilo
Utapata pesa, baada ya hapo utaamua uiite posho au mshahara.Hapo nimekuelewa kabisa mkuu .. Kwaiyo huo mkataba wa miaka miwili hua una ambatana na posho tu ila hamna mshahara? Au inakuaje
Poa nimewasoma wakuu na je JKT huko kazi za taaluma yako ulionayo unaweza ukapewa au huko ni jembe mtindo mmoja hadi pale utakapo maliza mkataba ..
Hapo kwenye umri naomba mnifafnulie..ina maana ata uyo kuanzia form 6 na kuendelea akitaka kujitolea umri ni mwisho miaka 23...?
Apo nimekupata mkuu..shukrani sana.Kuchukua mwisho miaka 23 ina maana kwamba,vijana kupelekwa jkt ni kama vile kuandaa kitalu kwa jwtz.leo kubwa ni kuandaa vijana tayari kwa kujiunga na jwtz.sasa basi jwtz kwa skari wa kawaida inachukua mwisho miaka 25.so wanaposema jkt mwisho miaka 23 wanalenga kuwa endapo jwtz litakuchukua ndani ya mkataba wako wa miaka miwili utakuwa bada ndani ya umri wa miaka 25 unaokubalika.
akale sumutaaluma yako utaiacha getini wakati unaingia kambini.kama itahitajika mtatangaziwa then utajitokeza na kupewa kitengo.siyo lazima iwe jembe tu,kuna kufuga kuku,samaki,ng'ombe,ushonaji,ujenzi,useremala,ufundi magari,na hata kama utakuwa mcheza soka utapelekwa kwenye timu husika.kazi zipo nyingi tu.jipange kijana ukale sumu ya kutosha