Anataka mchukua mwanangu kinyemela

Tafuta mwanasheria
ninavyojua mtoto chini ya miaka kumi anatakiwa kukaa na mama
unless kuwe na sababu zingine

anzia pia ustawi wa jamii
Na baada ya hapo huwa anaenda kukaa kwa baba kama mama anashindwa kumpa huduma mwenyewe na anahitaji msaada wa baba
 
Na unaanzaje kushindwa kumlea?pambana tu na utafanikiwa
 
Unafkiri ubaba ni uwezo wa kutoa mbegu tu na kuzalisha then ukimbie?chaaaa yaani kwanza baba asiyehudumia mwanangu nabadilisha mpaka jina la ukoo analotumia atatumia la kwangu na kingine hakuna ugumu mm kumwambia ww ulishakufa kitambo
 
Vilevile wakat huyo baba anagoma kutoa matunzo ya kuhudumia mwanae yy hakua mbinafsi?
 
Unafkiri ubaba ni uwezo wa kutoa mbegu tu na kuzalisha then ukimbie?chaaaa yaani kwanza baba asiyehudumia mwanangu nabadilisha mpaka jina la ukoo analotumia atatumia la kwangu na kingine hakuna ugumu mm kumwambia ww ulishakufa kitambo
Hata umwambie nimekufa nimeoza bado atabaki kuwa mwanangu, utanitenganisha nae tu lakini uhalisia utabaki kuwa ni damu yangu
 
Vilevile wakat huyo baba anagoma kutoa matunzo ya kuhudumia mwanae yy hakua mbinafsi?
Kuna sababu nyingi nyuma ya pazia you never know, tatizo lenu akina mama wagumu kuelewa mnataka kila mnachokitaka kifanyike kwa wakati huo, mtu akikuambia kafulia ujue kafulia kweli.
 
Bibie naona bado unampenda jamaa ndo maana anahangaisha serikali ya kichwa chao,una mahusiano na mtu mwingine kisha unabembelezana na baby dady wako eti uumpe mtoto atakupa mwingine na unakuja kuomba ushauri humu aiseeeee pole kwa mwanaume wako wa sasa

Mara malezi yakikushinda utampa ooh asubiri ifike miaka saba aje amchukue be serious mtoto sio jojo kusema ikiisha utamu utaitupa. Hakukuoa kiasi cha kuwa na haki zote za kujichukulia mtoto.
 
Mmmh mtu ana mimba yako unamuambia sikupanga kuwa na mtoto hivi karibuni means katoe hio mimba. Bidada kalea mtoto kakua jamaa anajirudisha kisingizio unachotoa ni hiki aiseee
Kuna sababu nyingi nyuma ya pazia you never know, tatizo lenu akina mama wagumu kuelewa mnataka kila mnachokitaka kifanyike kwa wakati huo, mtu akikuambia kafulia ujue kafulia kweli.
 
Tatizo lenu jambo dogo tu mnalikuuuuza, kwahyo ikitokea baba leo hana hela ya matumizi hata kesho hutamuomba?

Kipindi hicho hakua na kitu lakini sasa Kapata mwacheni atumie na mwanae
 
Tafuta mwanasheria
ninavyojua mtoto chini ya miaka kumi anatakiwa kukaa na mama
unless kuwe na sababu zingine

anzia pia ustawi wa jamii
Kama hakutoa mahari na hakuoa mwanasheria hatasaidia.
.
.
Bidada shikilia msimamo wako. Tena mwambie mtoto si wake, na kama ulimpa mtoto jina la baba yake badilisha mpe jina lako. Wajinga sana hawa vidume sometimes.
 
Dada zetu bwana.

Kwahiyo hapo unasema mtoto ana baba wakati hajawahi toa hata kilo moja ya sukari ya uji wa mtoto.

Ningekuwa ndio mimi huyo jamaa asahau kama ana mtoto.

Ila dada zetu mna huruma sana.
Hii huruma huruma ndio inafanya watudharau. Lea mtoto wako dada. Usiruhusu akamchukua. Km vipi subiri akue atamtafuta baba yake mbele ya safari.
 
Huyu nae Maelezo yake hayajitoshelezi, kasema jamaa hatoi Hata kumi mara huwa anakuja kumona mwanae simkataliagi,, anakujaje kumona mtoto nakuondoka asitoe hata mia???
 


LABDA KAMA UNATUDANGANYA, MTU ANAKUACHIAJE MIMBA MPAKA MTOTO ANAKUWA THEN ANATOKEA ANATAKA KUMLEA HALAFU UNASEMA NI MWANAE? HIVI AKILI ZIMEJAA KWELI? KAMA ALIIACHA MIMBA ANAJUAJE MTOTO BADO YUPO? KAMA UNGESHINDWA UKAITOA JE? YANI HUYO JAMAA INABIDI A ASSUME MTOTO HAYUPO, MAANA YAKE HAKUWEKA JITIHADA YEYOTE YA KUHAKIKISHA UHAI WA MTOTO, KAMA NI KWELI HAYA UNAYOYAONGEA HUYO JAMAA MPELEKE KWENYE VYOMBO VYA SHERIA ALIPE GHARAMA ZOTE ZA MTOTO MPAKA ALIPO KABLA YA CHOCHOTE! I WISH UNGEKUWA DADA YANGU!!!!! HUYO JAMAA HANA ADABU.
 
sijakuelewa hapo unaposema huna mpango wa kuzaa tena ingawa uko kwenye mahusiano na mwanaume mwingine au yeye pia hana mpango wa kuzaa na wewe.

kuhusu huyo ex wako muogope kama ukoma kwa kuwa lengo lake ni kukuharibia baada ya kuona umuulizi lolote kuhusiana na malezi ya mtoto.
 
Huyu nae Maelezo yake hayajitoshelezi, kasema jamaa hatoi Hata kumi mara huwa anakuja kumona mwanae simkataliagi,, anakujaje kumona mtoto nakuondoka asitoe hata mia???
Ha haaa ndugu. Kuna watu hawana mishipa ya aibu. Kuna mtu namjua fika anaenda kumuona mtoto wake hampelekei hata pipi na hapo hajamuona miaka mitatu.
 
Unao uwezo wa kumsomesha hadi chuo kikuu? Ukinijibu kuna jambo nitakwambia
Yes,panapo uzima na afya naweza,manake maisha anapanga Mungu hatujui ya kesho.Ndio sababu nimemwambia asubiri akue afate taratibu za kisheria.
Sitaki mwanangu mdogo akalelewe na watu nisowajua,hakuna wa kumpenda mwanangu zaidi yake mie mama yake.
 
Hataki kutoa chochote na hajawahi fanya hivyo.anachofanya ni kusifia tu mtoto kakua na kanawiri,utadhan muujiza.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…