KikulachoChako
JF-Expert Member
- Jul 21, 2013
- 19,884
- 40,053
Kila mtu kuna jambo linalomfurahisha nafsini mwake....ni kama vile mtu anayependa mpira wa miguu....au shabiki nguli wa masumbwi ambapo hufurahia kila amwonapo huyo shujaa wake ...kwa kawaida mapenzi hayo au ushabiki huo wa kitu hupelekea kumpenda pia yule muhusika wa sanaa hiyo au kile ambacho wewe kinakufurahisha....leo hiii si ajabu kukuta umati ukigombania kupata sign ya nyota Fulani si kwa sababu za kingono bali kwa kupenda sanaa yake au kuikubali kazi yake.....na huyo mpenzi wako anaangukia humo kwenye kundi la mashabiki wa kutupwa..ni kama vile wewe ambavyo unamhusudu LIONEL MESSI kinachoshindikana kuonyesha upendo wako kwake na kuikubali kazi yake ni umbali mrefu baina yenu.....