mangelengele
JF-Expert Member
- Nov 4, 2014
- 1,293
- 1,096
Kaka hayo yakawaida, yasikuumize kichwa. Posa na wewe, ili uwapunguzie majukumu ya kugharamia tu ila vichapo vinabaki palepaleKuna dada mmoja ambaye ni meneja msaidizi kwenye kampuni ninayofanya kazi kwa sasa, anatarajia kufunga ndoa mwezi ujao. Kwasasa anaishi na huyo mumewe mtarajiwa na wana watoto wawili tayari.
Kilichonisukuma kuandika uzi huu ni kutoka na tabia ya huyo dada kutoka kimapenzi na mfanyakazi mwenzetu. Na isitoshe yeye ndo anampenda sana jamaa. Amepanga achukue leave mwezi huu mwishoni ili waende tanga kabla ya ndoa yao na huyu jamaa wakale raha.
Kusema kweli inaniuma na ninajaribu kuwaza kwa sauti mpaka sipati jibu kwakweli. Kusema kweli nyie wanawake sio watu wa kuaminika hata kidogo.
Mbali na huyo mwanamke, pia kuna dada mwingine hapohapo ni mke wa mjeda ambaye amehamishiwa kikazi njombe. Naye anatoka kimapenzi na huyu jamaa yetu.
Najaribu kujiuliza kuhusu nyie wanawake nakosa jibu. Hivi mnakosa nini kwa waume zenu?