SnowBall
JF-Expert Member
- Sep 13, 2011
- 3,054
- 2,840
Heshima mbele wanaMMU
Ninayoiweka hapa ni mada ya ukweli ambayo rafiki yangu aliniletea tuidisscus..sasa katika kuidiscuss kuna mawazo ambayo nilimpa na of course kuna mengine ambayo tulishindwa kuafikiana. Lakini kwa sababu kisima cha JF hakikaukiwi maji nimeona kabla hajafikia uamuzi rasmi basi niwashirikishe nanyinyi hapa ili nione kama mnaweza kuchangia kitu gani katika huu mpango mzima!
Iko hivi..Jamaa yangu huyu alishawahi kuwa na rafiki wa kike kama miaka kumi iliyopita maeneo ya huko Mwanza. Na kama mnavyojua raha ya maisha kuhangaika, baada ya muda mrefu kila mtu kuwa kwenye mihanjo yake mawasiliano yalikatika na kila mtu kupata uhusiano mpya. Jamaa yangu alioa na kwenye ndoa yake kajaaliwa kupata mtoto mmoja, halikadhalika bibie naye aliolewa na kubahatika kupata mtoto mmoja pia. Kwa kipindi cha miaka ya karibuni kama miaka mitatu iliyopita marafiki hawa wa zamani walijikuta wameonana na wakawa wamebadilishana mawasiliano na wakaanza kuwa wanajuliana hali na vitu kama hivyo. Kwa mujibu wa huyu jamaa yangu, ilionekana kama mwanamke alikuwa anapenda wakumbushiane na jamaa yangu kwa mujibu wa alivyoniambia alimwambia waheshimu ndoa zao na wabaki kuwa 'friends'. Kwa mujibu wa mshkaji, mwanamke aliliafiki kwa shingo upande tu.
Sasa, tatizo limekuja,Mume wa yule mama alifariki..na mshkaji wangu hajui kilichomuua japo inasemekana ni 'pressure' na ofcourse ni kama mwaka mmoja uliopita na jamaa kwa mila na desturi baada ya siku nyingi za kutokwenda Mwanza alienda kwao na akaamua kwenda kumpa pole huyu mama. Cha ajabu huyu mama aliipokea pole yake lakini pia akamwambia angependa azae naye kwa sbb anahisi anahitaji mtoto na hayuko tayari kuolewa tena coz umri umeenda. Mshkaji wangu anadai alimchomolea, lakini yule mama alimwambia..'wewe nipe mimba tu hayo ya ulezi niachie mimi'!.
Sasa ili kufupisha habari hapo ndio kesi ilipo..Jamaa alifanikiwa kuchomoa kwa mara ya kwanza lakini huyu mama kaja hapa Dar na kampata jamaa na madai yake yamesimama vilevile!!..Naomba ushauri hapa 'Je? ampe tu hiyo mimba au asepe mazima!!..
NB: Matusi na Kejeli sio kitu cha maana hapa, na kama huna la kuchangia please ukimbie huu uzi!!
Ninayoiweka hapa ni mada ya ukweli ambayo rafiki yangu aliniletea tuidisscus..sasa katika kuidiscuss kuna mawazo ambayo nilimpa na of course kuna mengine ambayo tulishindwa kuafikiana. Lakini kwa sababu kisima cha JF hakikaukiwi maji nimeona kabla hajafikia uamuzi rasmi basi niwashirikishe nanyinyi hapa ili nione kama mnaweza kuchangia kitu gani katika huu mpango mzima!
Iko hivi..Jamaa yangu huyu alishawahi kuwa na rafiki wa kike kama miaka kumi iliyopita maeneo ya huko Mwanza. Na kama mnavyojua raha ya maisha kuhangaika, baada ya muda mrefu kila mtu kuwa kwenye mihanjo yake mawasiliano yalikatika na kila mtu kupata uhusiano mpya. Jamaa yangu alioa na kwenye ndoa yake kajaaliwa kupata mtoto mmoja, halikadhalika bibie naye aliolewa na kubahatika kupata mtoto mmoja pia. Kwa kipindi cha miaka ya karibuni kama miaka mitatu iliyopita marafiki hawa wa zamani walijikuta wameonana na wakawa wamebadilishana mawasiliano na wakaanza kuwa wanajuliana hali na vitu kama hivyo. Kwa mujibu wa huyu jamaa yangu, ilionekana kama mwanamke alikuwa anapenda wakumbushiane na jamaa yangu kwa mujibu wa alivyoniambia alimwambia waheshimu ndoa zao na wabaki kuwa 'friends'. Kwa mujibu wa mshkaji, mwanamke aliliafiki kwa shingo upande tu.
Sasa, tatizo limekuja,Mume wa yule mama alifariki..na mshkaji wangu hajui kilichomuua japo inasemekana ni 'pressure' na ofcourse ni kama mwaka mmoja uliopita na jamaa kwa mila na desturi baada ya siku nyingi za kutokwenda Mwanza alienda kwao na akaamua kwenda kumpa pole huyu mama. Cha ajabu huyu mama aliipokea pole yake lakini pia akamwambia angependa azae naye kwa sbb anahisi anahitaji mtoto na hayuko tayari kuolewa tena coz umri umeenda. Mshkaji wangu anadai alimchomolea, lakini yule mama alimwambia..'wewe nipe mimba tu hayo ya ulezi niachie mimi'!.
Sasa ili kufupisha habari hapo ndio kesi ilipo..Jamaa alifanikiwa kuchomoa kwa mara ya kwanza lakini huyu mama kaja hapa Dar na kampata jamaa na madai yake yamesimama vilevile!!..Naomba ushauri hapa 'Je? ampe tu hiyo mimba au asepe mazima!!..
NB: Matusi na Kejeli sio kitu cha maana hapa, na kama huna la kuchangia please ukimbie huu uzi!!