Amir Jamal aliyekuwa Waziri wa Fedha

Mkandara,

I wish ningekuwa Mzee ES. Huyo Sam nilimsikia sikuwahi kusoma maandishi yake. Lakini jamaa yule alikuwa maarufu sana. Mzee ES nimempenda kwa sababu ni Honest. Mkiwa na jamii ya watu wenye kuelezea mawazo yao bila kuona haya, nirahisi kuweka masuala mezani kuliko wale wanopitisha mgomo baridi.

Si umeona Mzee ES anasema viongozi wa CCM wanaogopa kusema hadharani kuwa Salim wanampinga kwa sababu ya uarabu wake? Utamu wa demokrasia siyo matokeo ya kura. Ni zile taratibu zinazotumika kuwapata wagombea, kuandikisha wapiga kura, kupiga kampeni, elimu kwa wapiga kura, na zoezi zima la upigaji kura. Watashi wanafupisha na kusema due process.

Sasa kama due process ya kumpata mgombea wa CCM, na vigezo vilivyotumika inakuwa ni jando, basi wanajua kuwa vigezo vyao siyo kwa manufaa ya taifa. Kama ni kwa manufaa ya taifa, inabidi ielezwe kwa msisitizo wa hali ya juu ili hata mtoto mchanga aelewe. Si kwa manufaa ya taifa bwana? sasa tunaficha nini? kwa nini wanaona haya kusema hadharani kuwa hatupendi waarabu?

Hivi CCM si walikuwa vinara na hasa kututia umaskini kutokana na sera zao za kupinga ubaguzi wa aina yoyote barani Afrika na dunia nzima. Au zilikuwa ni sera za Nyerere? Si wale wale akina Mkapa ndiyo walikuwa wakiziuza nchi za nje mpaka kikaeleweka? Au walikuwa hawajapata akili timamu. Ni lini wamebadilisha sera yao? Au ndiyo mambo ya unafiki?

Ni vizuri kubadili sera, itikadi, na mitizamo katika maisha, huna haja ya kuwaeleza watu kama misimamo yenyewe ulikuwa unafanyia bafuni wakati unaoga. Lakini CCM wametueleza msimamo wao juu ya ubaguzi wa rangi miaka nenda rudi. Wanaposhushiwa na mwangaza wa roho mtakatifu na kubadilika, inabidi watueleze ati! kwa nini waliamini yale waliyotuaminisha na kitu gani kimewafanya wabadilike na kuamini haya mapya. Si chama tawala? Umuhumi wa CCM kwa hili unatokana na udhoofu wa vyama vya upinzani, Mwalimu aliwahi kusema kuwa unapomtangaza mgombea uraisi wa CCM, si ajabu ukawa unamtangaza Raisi wa nchi. Ndiyo maana due process zao ni muhimu kwa mustakabali wa nchi yetu.

Kificho cha vigezo kinaashilia uhuni. Huu ndiyo utamadunu tunaotaka kuujenga. Mimi nadhani watu tuupinge bila kujali itikadi zetu za vyama. Hakuna jando kwenye mambo ya nchi. Hawa wasioweza kusema hadhalani kuwa ni wabaguzi, wataweza kusema kuwa ni wezi au wala rushwa? Mzee ES ebu nisaidie hapa.
 
Mzee Kyoma,

Hapana gazeti ninalo ambalo Mkapa, Salim, na Warioba, wamekaa mbele ya waandishi wa habari pale maelezo ile siku ya kwanza na ninayo unayoisema ya yeye na Ulimwengu, kwenye hili ni 100%, maana nilikuwa ninahusika na kambi moja ya uchaguzi huo,

Salim hakukataa kugombea urais 1995, isipokuwa aliwaambia CCM wamuombe rasmi publicly kuwa wanamuhitaji kuja kuwa rais,

Collin Powell alianza kuombwa na Bush pale tu kambi yake walipogundua kuwa kutakuwa na matatizo ya kura Florida, kwani mwanzoni walipomuomba alikataa kabisaaa, wakati anashughulika na shughuli za kuwasaidia Scout ku-raise funds, ni mpaka mambo yalipochacha Florida ndipo akaamua kuanza kukubali publicly kuwa anafikiria kujiunga kama alivyoombwa na hao wazungu ili kujiongezea umaarufu na soo ya Florida,

The rest ya hadithi ni progressive political talk ni very sound lakini sio realism ya siasa zetu, pole pole huko mnalotaka tutafikia, ila kwa sasa mkubali tu yaishe tutaendelea tu na hizi siasa za kitoto na kuwakataa waarabu, ndio maana kina Rostam wanajua siasa za bongo wamekataa vyeo wanatesa kwa milango ya nyuma kwani wanajua kuwa wakati bado, ila unakuja!
 
Mshikaji,

Sasa kidogo nakupata!

Nadhani picha kamili hapa inakwenda hivi:-

Ukweli umesimama kuwa, watu kama Salim hawana nafasi kabisa ya kuwa rais Tanzania na hata viongozi wa CCM wanaelewa hivyo.

Well, mbali na hadithi za haki za binadamu na sijui charter of rights nadhani kuna ukweli hapa.

Sidhani kama Watanzania watapenda kuona Mtu mweupe akichukua Urais achana na Salim na uarabu wake. Kwa hiyo nikitazama upande wako wa sarufi naweza kuelewa uzito wake kwani sintapenda kuona Zimbabwe, mzungu kachukua tena kiti cha urais ati kwa sababu wanayo haki ya kugombea kiti hicho na hasa mzungu huyo alitoka chama cha Smith!..Hii ni kucheza kamali na Zanu PF wanafahamu ukweli huo.

Na ukweli huo ndio baadhi yenu ama kwa lugha fasaha wengi kati yetu wanauunga mkono kutokuwa na mtawala mwarabu na hasa Salim, au sio Mzee Es? It make sense...na unayo kila haki ya kutoweka imani yako kwa Salim.
 
Unajua Bob,

Unapaswa kuelewa kuwa mimi si-create something new hapa, isipokuwa ninajaribu kuya-read matokeo ya uchaguzi kwa kuzingatia political facts zilizotokea, mpaka Salim akatolewa,

the matter of fact kuna mpaka theory za uchawi jinsi wachawi toka, Pemba, Nigeria, na Seychelles walivyoletwa kushughulikia uchaguzi na Wanamtandao, na kwamba Mwenyekiti wa CCM wa Ruvuma mzee Ndunguru aliyefariki wakati wa ziara ya Mkapa huko kusini, siku tatu kabla ya uchaguzi Dodoma, alikuwa ni kafara iliyomchanganya akili BM toka pale alikuwa hajui analofanya mpaka uchaguzi ulipokwisha ndipo akili zikamrudia tena, na kafara lingine la mabasi kama matatu ya abiria kuanguka na abiria wote kufa, baada tu ya ule uchaguzi,

na wenye hii theory wanaapa kwamba mkewe Mkapa waliporudi Dar alimuuliza mzee Ben kama he was all right, kwani hata yeye alikuwa shocked! Na habari hizo zinadai hawa wachawi wa Seychelles hawakuondoka wapo bado kuhakikisha kuwa ngoma ya umaarafu inaendelea kwa nguvu zote,

Binafsi sijui kuhusu haya lakini yapo, tena mimi binafsi nilionyeshwa mpaka hawa wachawi, man I do not know! But one thing I know for sure ni kuwa Salim alikataliwa kwa sababu ya uarabu wake na mimi I have nothing to do with it and I could care less!
 
Mzee ES

Kasheshe la Florida lilianza usiku wa siku ya kupiga kura na likaisha siku Mahakama kuu ya Marekani ilipositisha zoezi la kuhesabu kura huko Florida. Mambo ya intimidation, hanging chard, mtu mweusi kunyimwa haki ya kupiga kura, watu wenye umri mkubwa kushindwa kutoboa kitobo cha karatasi, udanganyifu na wizi wa kura, kura kuhesabiwa upya na kokoro zote zilizofuatia, suluhisho lake lilikuwa ni la kisheria tu. “Legal wrangling”. Umaarufu wa mtu haukuwa na nafasi tena kwa sababu hakukuwepo upigaji kura na kampeni zilisha isha. Mtu aliyekuwa anahitaji msaada Florida alikuwa Gore na siyo Bush.

Katika saga lile, strategy ya Bush ilikuwa ni kuweka watu kwenye ground Florida ili kuhakikisha kura hazihesabiwi tena. Jopo la Bush liliongozwa na James Baker. Strategy ya Gore, ilikuwa kinyume. Alitakiwa kuwa na watu wa kuhakikisha kura zinahesabiwa upya. Jopo la Gore liliongozwa na Wallen Cristopher. Kumbuka Florida’s battle haikuwa state nzima. Ilikuwa ni sehemu ambazo ni heavily Democrats ambao ni weusi, masikini, na wazee wengi wao ni wale waliohmia huko mfano jews etc. Sehemu hizo ni Broward, Palm Beach, Miami-Dade, na Volusia counties. Also, remember, one of the most controversial aspects of the Florida election was the so-called butterfly ballot used in heavily Democratic Palm Beach County. Many voters came out of the polls saying they were confused by the ballot design.

Kitendo cha kumpeleka Powel pale ingekuwa ni kutetea haki za weusi na wanyonge. Kumbuka Powel ni Republican, ingawa sera kama za affirmative actions ndizo zilimfikisha pale alipo, hata hivyo, haziamini na hapo ndipo anapotofautiana na Jesse Jackson. Huwezi kumvuta hata kwa mtutu wa bunduki kwenda kutetea weusi wasioenda shule. Powel kwenda kwenye saga la Florida kusingemsaidia Bush hata kidogo. Gore alihitaji msaada wa watu mashuhuri kwenda Florida kushinikiza ili kura zihesabiwe upya. Bush Hakuhitaji mtu mashuhuri kwasababu chombo kilichokuwa na mamlaka ya juu ya kusimamia na kutangaza mshindi Florida kilikuwa kinaongozwa na mwana mama wa Republicans ambaye mwaka huu anagombea usenetor. Pia, Bunge la Florida lilikuwa linaongozwa na Republicans. Jeb Bush ambaye ni gavana wa Florida na ndugu wa Bush, yeye alifanya umafia kabla ya uchaguzi, hivyo kwenye sakata alijifanya kukaa pembeni ili kujihusisha kwake kusilete nongwa (PR). Yeye alijifanya kuwa msimamizi wa sheria na kuangalia mipaka yake ya uongozi. Gore alichokuwa nacho ni Mahakam kuu ya Florida ndiyo imejaa watu waliteuliwa na viongozi wa Democrats

Strategy ya pili ya kambi za Bush na Gore ilikuwa kuhakikisha wamarekani hawachoki kwa sababu sakata lilichukua muda mrefu. Zilikuwepo calculations za public relations (PR). Democrats ni chama kilichojaa watu wanaotetea haki za kila kitu unachokijua wewe duniani. Wote walijipeleka Florida. Wanasheria wengi sana Marekani ni democrats hivyo walipanda ndege na kwenda kujitolea tu. Hata yule mwanasheria aliyebobea wa Marekani bwana David Boies alijitolea bila kulipwa kumwakilisha Gore toka mahakama za rufani za Florida mpaka Mahaka kuu ya Marekani. Republicans wao wanafedha.

Hivyo, kwenye TV kambi zote mbili zilikuwa makini kuhakikisha nani anaongea kwa niaba ya nani? Walimuweka Gore na Bush kwenye TV kwa mahesabu ya juu sana. Pia walichagua watu wa kuongea kipindi fulani na wakati fulani. Walikuwa hawaendi hovyo. Suala muhimu hapa, lilikuwa kuhakikisha inner circle ya Bush na inner circle ya Gore hawatokezi kwenye TV. Waliogopa ku-backfire. Kumbuka kwenye kampeni, kambi ya Bush ilishatoa nyeti makusudi kuwa Powel angekuwa waziri wa masuala ya kigeni. Powel ni mmojawapo wa watu ambao hawakwenda Florida na wala hawakutokea kwenye TV kuongelea chochote kuhusu saga lililokuwa linaendela kule Florida.

Kilichokuwa kinaangaliwa ni sheria za Florida zinasema vipi kuhusu utata wote ule. Powel had nothing to do with state laws. Mahakama ya Florida ya ilipoamua kura zihesabiwe upya ambao of course ulikuwa ni ushindi kwa Gore, Bush akakimbilia Mahakama Kuu ya Marekani ambayo iko juu ya vimahakama vya states zote. Alikwenda kule akijua kuwa uwiano wa majaji walioteuliwa na maraisi wa Republicans ni mkubwa kuzidi wa wale walioteuliwa na maraisi wa Democrats. Ni kweli, Bush alishinda uraisi kwa kura moja ya jaji wa mahaka kuu ambayo matokeo yake yalikuwa 5-4. Kura ziligawanyika kutokana na itikadi za majaji na kwa jinsi wlivyoteuliwa na maraisi wa hivi vyama. Hivi ndivyo uamuzi wa mahaka kuu ya Florida wa every vote counts ulivyotenguliwa.

Kweli kama unavosema kuwa Bush alihitaji msaada in order to heal the country ambayo ilikuwa imegawanyika vibaya sana kutokana na lile sakata lililoanza usiku wa uchaguzi na kuisha tarehe 12 mwezi wa kumi na mbili mwaka 2000, when the U.S. Supreme Court overturned a Florida Supreme Court ruling ordering a full statewide hand recount of all undervotes not yet tallied. Mzee ES kadili nilivyokuelewa unadhani umuhimu wa Powel ulikuja katika kipengele cha kuleta umoja wa taifa lililokuwa limegawanyika. Ni kweli kuwa Bush alimteua Powel ili kuonekana ana reach out. Automatically, hiyo ilitakiwa ku-neutralize uchungu wa Florida. Hata hivyo, kabla ya uchaguzi hakuna aliyejua kuwa mahakama kuu ya Marekani ndiyo itamuweka Bush madarakani.

Ingawa Weusi, Waisrael, na Wazungu wa kima cha chini wanaoishi kwenye maeneo niliyoyataja kule Florida ndiyo walionewa kwenye uchaguzi kwa madai ya kura zao kutokuhesabiwa and all sorts of intimidations, lakini kilichokuwa mezani na kilichogawa nchi ni matokeo ya uchaguzi na nani atakwenda kutekeleza sera na kulinda maslai ya nani. Hivyo, nchi haikugawanyika kati ya weusi na weupe au kima cha chini na matajiri. Nchi iligawanyika kati ya kile wanaita Red states and Blue states (majina ya rangi ilitokana na ramani za kwenye TV). Kwa lugha nyepesi ni liberals and conservatives. Mitizamo ya kulia na kushoto. Ukipenda unaweza kusema Democrats na Republicans. Mfano majimbo kama Texas kumchagua Raisi wa democrat ni sawa na kuandika nane kwenye maji. Au state kama New York kumchagua Raisi wa Republican ni kasheshe kwelikweli.

Bush alijaribu kuazima busara za kuiunganisha nchi iliyokuwa imegawanyika kiitikadi na siyo kirangi. Powel ni Republicans –independent thinker ndani ya republican. Kama ulikuwa unataka kutibu kidonda cha democrats, ni sawa na kutia dawa ya chumvi. Utawala wa Clinton ndiyo ulimlazimisha Bush kumtafuta Powel wakati wa Kampeni. Clinton, ukiondoa scandal za wanawake, alikuwa ameiweka nchi ya Marekani katika hali ya kiwango cha juu cha uchumi katika mifuko ya wamarekani. Historia ya wamarekani ni kuwa kama Raisi alifanya kazi nzuri ya kuinua maisha ya wamarekani, basi makamu wake huwa anakuwa na nafasi ya kushinda uraisi. Pia Raisi mwenyewe mara nyingi anashinda awamu ya pili. Ukweli huu huwa unafutwa katika kipindi cha majanga makubwa au nchi ikiwa kwenye vita. Kwa historia tu, Gore alikuwa na nafasi nzuri ya kuiongoza marekani. Watu huwa wanafikiri kuwa makamu wa raisi ataendeleza yale yaliyokuwepo.

Utawala wa Clinton ulimlazimisha vipi Bush kumfuata Powel wakati wa kampenil? Hii ilikuwa muda mrefu kabla ya kupiga kura zilizo zaa saga la Florida. Clinton alikuwa na sera zilizowatetea wanyonge wakiwemo watu weusi. Affirmative action ilitukuzwa kama salamu maria wakati wa Clinton. Hata mfagizi wa Ikulu alikuwa mweusi. Wapishi, wapiga picha, ambosi wa secret service, yule mwana sheria lafiki yake kipenzi Jordan ambako alikuwa anakwenda kupumzika kama unavyosikia Bush anakwenda kupumzika Texas. Clinton hakuwapa vyeo vya juu sana minority, lakini alikuwa na sera zilizowainua kimaisha na wakateuliwa katika nyazifa nyingi throught the country. Unakumbuka hata yule waziri wa mambo ya biashara mweusi ambaye alifia kwenye ajali ya kwenye ndege. Clinton alitoka machozi. Hata wamexicano Clinton alikuwa nao tu. Kama yule ambeye sasa hivi ni gavana wa New Mexico Richardson ambaye inasadikiwa atagombea uraisi mwaka 2008. Wote hao waliingia kwenye ramani ya Marekani kwa sababu ya Clinton

Clinton aliishi na weusi Ikulu na walimfuata sehemu aliko enda. Bush alitaka kupata kura za minority angalau za kutosha. Kumbuka alishinda uraisi kwa kura za Florida kama miasita hivi. Hii ni kadiri ya umamuzi wa mahaka kuu ya Marekni. Pia kumbuka anatoka Texas na alikuwa Gavana. Hakuwa na historia yoyote ya kuwa na minority karibu ingawa Texas wamejaa watu kutoka Mexico. Hata kama alikuwa nao karibu, ni watu matajiri wachache, au wale wasomi kama akina Rice na huyu Attorney General wake ambaye alisomea Rice University na Yale zote moto wa kuotea mbali. Ilimbidi atafute mtu wa kumtetea na kuonyesha kuwa ana reach out.

Mtu huyo alitakiwa apendwe na weusi na apendwe pia na kambi yake Bush. Hakuna mtu zaidi ya Powel. Hata bintie Rice kwa wakati huo asingeweza kuziba lile pengo. Alimtumia Powel kwenye miji iliyojaa weusi kupiga kampeni. Walisimama wote kwenye jukwaa utafikiri Powel ndiye alikuwa anagombea uraisi. Walikuwa Michigan, Pensylovenia, Illinois, na kwingineko. Cha ajabu Powel alikwenda Florida na Bush mara moja kwenye kampeni. Lakini walicheza wote ngoma katika hiyo miji kwa muda wote.

Kwa nini kambi ya Bush ilitoa Leak kwenye vyombo vya habari na Bush mwenyewe akakataa kukanusha au kukubali kuwa Powel atakuwa waziri wake wa masuala ya kigeni kabla ya uchaguzi? Wamarekani wameendelea siyo kama tulivyo sisi. Hata kimawazo weni wao wanaweza gundua janja ya nyani kula mahindi mabichi. Kwa wamarekani weusi, kuwa na rangi nyeusi haimaanishi wewe ni mweusi. You just black in color but not black American. Hakuna mtu mweusi kama Clarence Thomas, a US Supreme court justice. (nawashangaa na ubaguzi wetu, hawa majaji ndiyo waliomuweka Bush madarakani). Huyu jamaa ni mweusi kama mkaa. Hata hivyo, kamuulize mmarekani mweusi yeyote yule. Au kaongee na Maya Angelo, Oprah ma wengineo manake nikisema kamuulize Jesse Jackson utadhani nimevuka mipaka. Hawaamini kuwa ni Mmarekani mweusi hata kidogo. Na yeye anajua. Mtangazaji maarufu wa redio za conservative huko marekani bwana Rush Limbaugh ambaye ni mbaguzi kupindukia. Aliwahi kutangaza kuwa Wamarekani weusi wametoka utumwani mpaka Ikulu. Anaamini kuwa Clinton ni Mmarekani mweusi. Ni kweli, huwezi kuwashawishi weusi wa Marekani kuwa Clinton ni mzungu. Wanaamini kuwa Clinton ni mweusi mwenzao. Hata wazungu wanaamini hivyo. Ndiyo maana walifanya mikasa yote ili kumuondoa pale Ikulu. Kwenye kampeni za uchaguzi 2000, Bush alikuwa na slogan kuwa “we will bring the integrity to the white house”. Watu walidhani anaongelea mambo ya kuchombeza ya Monica. Hapana! Ilikuwa kuwaondoa weusi wote waliokuwa wanafanya kazi Ikulu akiwemo Clinton mwenyewe na kutokubakiza makombo ya akina Gore. Wazungu walikuwa wanaelewa anaongelea nini.

Hivi ndivyo Powel aliingia kumsaidia Bush. Kambi ya Bush walitaka kuonyesha kuwa watamchagua mweusi kushika madaraka makubwa kuliko alivyofanya Clinton na yatakuwa madaraka ya kwanza kufikiwa na mwafrika. Walipingwa na kambi ya Gore kwa kueleza kuwa weusi sio kushika madaraka na kusimamia sera za ukandamizaji. Weusi siyo rangi, bali ni maisha, utamaduni na historia. Walimpenyeza Jesse Jackson kufanya kazi hiyo. Ni kweli kambi ya Gore ilifanikiwa kwa hilo kwani Bush alipata asilimia ndogo ya kura za weusi na ndiyo maana hatambui jumuia zao na hata wakimualika huwa haendi kinyume na maraisi waliopita. Aliposhinda, kwasababu kampeni yake ilishamshikia kidedea Powel, hakuwa na chaguo ila kutimiza zile fununu zilizokuwa zimetapakaa na hata siku moja kule Michigan aliwahi kueleza kwenye jukwaa kuwa mnmuona huyu, hawa ndiyo viongozi tunowataka. Alikuwa anajibu hoja za kambi ya Gore kuwa tunataka sera na viongozi wanaofanana na Marekani (nchi ya mchanganyiko).
 
Mzee Mkandara

Mimi ninachosema ni kuwa Salim ni Mtanzania, yaani Raia wa Tanzania wa kuzaliwa. Hakuna mtu anayeweza kumnyanganya uraia au kumpa. Alipewa na Mungu. Anayo haki ya Uraia kama ilivyoidhinishwa na katiba yetu, Unless something changed in the constitution that I’m not aware of. Tukianza kuvaa majoo ya ubaguzi, tutashindwa kutetea haki nyingine za raia kwa sababu tunajifunga kamba wenyewe.

Mzee ES anasema kuwa haya mabo hayaweza kusemwa hadharani. Siyo kweli. Salim alitolewa kwa sababu ya sifa yake ya uongozi ambayo viongozi wote wa CCM wanaifahamu. Ilikuwa siyo kazi Rahisi kumuondoa Salim kwasababu iko asilimia 25 to 30 ya viongozi wa CCM wanaolitakia taifa mema na hawapendi rushwa na ufisadi ndani ya chama chao. Wewe ushangai Rostam Aziz amejifunga kanga kiunoni kumpinga Salim? Yaani Muhindi ni mzalendo kuliko mwarabu? Yaani Warioba aliyekuwa nyuma ya Salim si Mzalendo ila Rostam aliyekuwa anampinga Salim ni mzalendo.

Haya mambo siyo yenu. Mmeletewa na wanasiasa kwa sababu ya kugombania mlo. Mkapa na Salim walikuwa vinara wa kuuza sera za nchi dunia nzima. Walishirikiana kwa hali na mali. Nakumbuka mkutano wa OAU nchini Lagos Nigeria wakati Salim na Mkapa wanashauri viongozi wa Afrika kukubali uvamizi wa Tanzania nchini Uganda. Pia wakati wa kupinga sera za kibaguzi popote duniani. Salim na Mkapa walikuwa kama mapacha na kilichowaunganisha sio utanzania bali ni zile sera walizokuwa wanatetea. Walikuwa wanajenga hoja zisizopingika kokote duniani. Sasa Mkapa asimwambie Salim wakati huo kuwa mshikaji wangu ni mwarabu, angoje anatoka kwenye madaraka ndipo amwabie? Hapa sio mwarabu au la! Ni nani atalinda kinyesi alichojipaka Mkapa.

Salim raia wan chi gani uarabuni? Watanzania msikubali kununua mafuta ya kujikaanga wenyewe. Msiongopeane kuhusu uarabu mkianza ubaguzi tutaishia kwenye ubaguzi. Mtu unaweza kujiuliza, hivi watu wa Somalia wana uarabu au kabila gani? Mbona wanabaguana na kuuana? Hata kule Bukoba, wale wote si wahaya jamani? Nakumbuka mwaka 1995 wamemkalia kooni yule mbunge kwa tiketi ya CCM bwana Kataraia kuwa ni Mziba yaani ni mhaya lakini kutoka kiziba. Walizoea mbunge wao wa muda mrefu Bwana Luangisa ambaye ni Muyoza. Wewe fikiri jamani, hawa wote ni wahaya. Tofauti ya Muyoza na Mziba ni rafudhi ambayo watu wa Bukoba peke yao ndiyo wanaweza kuitofautisha. Nyerere ndiye alikwenda kule wakati anamuuza Mkapa kuokoa jahazi. Ilibidi awambie wahaya kuacha kupanda mbegu za ubaguzi kwa sababu ya kugombania madaraka.

Kibaya zaidi wanaopanda mbegu za ubaguzi siyo wananchi. Ni viongozi. Wananchi tunanunua tu. Viongozi wa siasa wanatumia njia zozote zile kupata madaraka bila kuangalia madhara kwa taifa. Nikama unavyoona suala la rushwa au takrima. Siku hizi rushwa imetawala. Wajumbe wa vikao vya uteuzi wa wagombea udiwani, ubunge na hata urais wanafuatwa wanakoishi na kuhongwa. Hongo inaendelea hata kwenye mikutano ya uteuzi na mara nyingi uteuzi unafanywa kutegemea kiwango cha hongo.

Kwenye kampeni kuna hongo na takrima. Katika hali ya umasikini uliokithiri watu wanapokea hongo na kuchagua viongozi kwa msingi wa fedha. Watu wenye uwezo na hulka ya siasa ni wengi na wakitengwa kwa msingi wa kutokuwa na uwezo wa fedha wanaweza baadaye kuwa chanzo cha kujenga chuki ndani ya jamii. Hata watu wanaoenguliwa kwa misingi ya rangi, kabila, dini, ukanda, na mengineyo mengi watakuwa chanzo cha chuki na tutafika taratibu kwenye mauaji.

Tuwapinge viongozi wetu wanapotuletea mambo yasiyotusaidia na kuyapa kipaumbele katika kampeni. Hasa pale yanapopinga haki na uhuru wa raia yeyote. Angalia kule Zanzibar, kuna masharti ambayo yanaingilia kwa kiwango fulani haki na uhuru wa mpiga kura. Mtu anatakiwa awe ameishi kwa muda maalumu katika jimbo ili aweze kujiandikisha kama mpiga kura. Sharti hili linaingilia haki ya mtu kuhama sehemu moja ya nchi na kwenda sehemu nyingine. Hakuna sababu ya msingi kwa nini mtu aliyehamia Makunduchi kutoka Mjini Magharibi azuiwe kujiandikisha mahali alipo kwa sababu tu hajaishi hapo kwa muda maalumu.

Baya zaidi ni kuzuia watu wenye asili ya Bara wasipige kura. Mtu anayeishi na kufanya biashara Zanzibar atalazimika kufuata sheria na uongozi wa mji wa Zanzibar. Vivyo hivyo mtu anayeishi Dar es Salaam ni lazima azingatie sheria na uongozi wa jjji hilo. Raia yeyote anayeishi Dar es Salaam ana haki ya kushiriki katika uchaguzi wa madiwani lakini si raia wote wana haki ya kushiriki katika uchaguzi wa madiwani katika mji wa Zanzibar. Utaratibu huu una msingi wa kuwagawa raia na unaweza kuathiri umoja wa taifa.

Mwanzoni kila raia alikuwa na haki ya kuchaguliwa kama mwakilishi. Lakini haki hii iliwekewa sharti mwaka 1992, kwamba mgombea yeyote lazima apendekezwe na chama cha siasa. Sharti hili limemnyang'anya raia haki yake ya msingi ya kuchaguliwa kama mwakilishi. Haya yote siyo matakwa ya wananchi. Ni matakwa ya viongozi ili waendelee kukaa madarakani. Kuibuka kwa ukabila, udini, ukanda na ubaguzi wa jinsia na rangi kunachochewa au kuvumiliwa na vyama vya siasa. Mambo haya yanavuma zaidi wakati wa kampeni za uchaguzi. Badala ya kuyakemea viongozi wanatumia ukabila, dini, kanda, rangi na jinsia ili kupata kura.

Kila nchi au taifa lina mambo yake ya msingi na utaratibu wa kuyasimamia. Kila chama kinapaswa kuzingatia mambo hayo na kuyatetea. Lakini katika nchi yetu kuna malumbano mengi hata kwenye mambo ya msingi. Kwa mfano vitisho ambavyo wanapata wananchi wa asili ya Bara huko Zanzibar ni jambo ambalo lingekemewa kwa sauti moja na vyama vyote. Badala yake vinalumbana

Mzee Mkandra, Lazima tutambue kuwa umoja, mshikamano, maelewano na amani yetu ni matokeo ya juhudi za Watanzania wakiongozwa na watu waliokuwa wanalitakia mema taifa letu. Ni jukumu la vyama vya siasa, viongozi na Serikali kusimamia utekelezaji wa sera ambazo zinalinda mafanikio tuliyokuwa nayo ambayo yanaaza kupotea. Tanzania ni nchi ambayo kwa kiwango kikubwa imejenga muafaka wa kitaifa. Msingi wa muafaka huu ni jitihada za makusudi zilizofanywa kuleta usawa kwa msingi wa utu, kukataa ubaguzi wa aina yoyote, kutumia lugha moja, kuondoa mila mbaya za makabila zilizowagawa wananchi, kuendeleza mila nzuri, kuwashirikisha wananchi katika shughuli za nchi na kuwa na sera zinazowalenga wananchi. Suala sasa si ujenzi wa muafaka. Suala ni kulinda na kuimarisha muafaka.

Ili kulinda na kuimarisha muafaka huu ni lazima tutambue na kupiga vita vitendo vyote vilivyo kinyume na mafanikio yaliyopatikana. Mambo ambayo yameanza kujitokeza ni ubaguzi kwa msingi wa kabila, dini, kanda na jinsia. Ubaguzi wa Bara na Visiwani nao ni lazima upigwe vita. Wananchi washirikishwe zaidi katika shughuli la nchi yao na demokrasia iimarishwe zaidi kwa kuzingatia haki za wananchi. Tusipofanya hivyo muafaka wa sasa utapotea. Mwisho tutachinjana. Hii ndiyo historia ya mwanadamu
 
Mzee Kyoma,

Man I cannot read the whole thing, ninafikiri at this point tunahitaji kukubali kutofautiana, kwa sababu msimamo wangu kama mshiriki wa hizo kampeni katika kambi moja, ni kwamba Salim alinyimwa kutokana na rangi yake, kwani sijui record yoyote ya JK iliyokuwa so convincing kuliko ya Salim,

Na kukuhakishia ni kuwa kuwa Salim alikuwa so relaxed and confodent na uchaguz, kiasi kwamba hakutumia hela nyingi kwa uchaguzi zaidi tu ya kumnunulia gari la SUV mzee Ndejembi aliyekuwa akizunguka nchi nzima kumpigia kampeni, aliamini kuwa yeye akishindwa basi JM atakuwa ambaye ni rafiki yake kwa hiyo hakitaharibika kitu,

Mpaka siku ya siku ilipofika ndipo akagundua kuwa viongozi wengi walikuwa siku zote wamevaa ngozi za kondoo, anyway sina mpango wa kukubadili msimamo wako wa kwamba Salim alinyimwa kutokana na record,

kwa sababu personal ninasubiri the day kiongozi wa bongo atakapochaguliwa au kunyimwa kwa kutumia record, great debate bro lakini no siwezi kusoma yote ili kuendelea na hii mada!
 
Last edited by a moderator:
Mzee ES

Nashukuru kwa kukubali kutokukubaliana. Na mimi naona nibwage manyanga kwa hili. Kumbuka nyuma umeandika kuwa Salim ingawa alifuatwa Addis A. na kuombwa kugombea uraisi na wale waliojiita vijana mwaka 1995, alikataa kwa sababu alitaka CCM wamuombe rasmi. Mara nyingi, watu wanoweza kuongoza hawakimbilii madaraka kwa udi na uvumba.

Pili umeandika kuwa hujui record yoyote ya JK iliyokuwa so convincing kuliko ya Salim. Ninachoweza kukwambia hapa ni kuwa hata mimi ningeshangaa kama kuna anayeamini kuwa JK ana records kumzidi SAS. Kwanza toka lini CCM wakakuchagua kwa records?

Nashukuru na mimi nakubali ombi lako la kukubali kutokukubaliana. Tutakutana kwenye mada nyingine.
 
duh! enzi hizo kulikuwa na magreat thinker JF,yaani thread inachangiwa na watu wachache na mawazo yaliyoshiba!
 
Last edited by a moderator:
Mzee ES
...Kilichokuwa kinaangaliwa ni sheria za Florida zinasema vipi kuhusu utata wote ule. Powel had nothing to do with state laws. Mahakama ya Florida ya ilipoamua kura zihesabiwe upya ambao of course ulikuwa ni ushindi kwa Gore, Bush akakimbilia Mahakama Kuu ya Marekani ambayo iko juu ya vimahakama vya states zote. Alikwenda kule akijua kuwa uwiano wa majaji walioteuliwa na maraisi wa Republicans ni mkubwa kuzidi wa wale walioteuliwa na maraisi wa Democrats. Ni kweli, Bush alishinda uraisi kwa kura moja ya jaji wa mahaka kuu ambayo matokeo yake yalikuwa 5-4. Kura ziligawanyika kutokana na itikadi za majaji na kwa jinsi wlivyoteuliwa na maraisi wa hivi vyama. Hivi ndivyo uamuzi wa mahaka kuu ya Florida wa every vote counts ulivyotenguliwa...
Halafu tunadanganywa mahakama zao ni huru!
 
Ndugu Mugwishage,
Amir Jamal alisekuwa waziri wa fedha tanzania alizikwa Canada. Amerika ya kaskazini na siyo AFRICA.

Unajua wahindi wa tanzania bado wanaona kuwa ni bora walete watu toka Pakistani kuja kufanya kazi za ulinzi kwenye godowns zao kuliko kuajiri mtanzania mweusi.

Wahindi hawa hawa wanaajiri graduate watanzania kwa shilling 60000/= kwa mwezi halafu anamuajri mhindi form six anamlipa laki tatu! Mfano Manji ninasikia watu wananyanyaswa huko quality group! etc pia wahindi huajiri watu bila qualification. Hakika vijiwanda vyao vikipitiwa kuna ajira kibao zitapatikana huko(mfani store keeps, wahasibu makarani nk) ! Lakini zamani walikuwa wanajigamba kuwa wana simu ya kila waziri.

Sasa kama wao hawako tayari kututuambua kwenye urais ndiyo watatuatambua! tusjie tukapa aibu siku nyingine tututakuwa na rais Mhindi halafu akifa mwili wake ukaenda kuzikwa canada!

Mwili ni kasha hata wwe ukitaka kuzikwa Canada ni pesa yako tu.Muhimu anaweza kutufusha,tuna haja sasa tuwape nafasi ya uraisi watz wengine wasio na rangi nyeusi ili tupate balance.
 
Eti mzee kuna ajabu ya vijana wa kibongo kuiba?

Ala hawa mabalozi kina Mahalu nao vipi? mbona wameiba?
Na huko majuu hao kina Ken Lay ambao wamewaibia watu mpaka viinua mgongo vyao huko ma-Enron, sasa hao mzee unasemaje na wao ni vijana wa kibongo?

Swali ni kwamba someone needs to explain, mwananchi aliyefikia hatua hata ya kuwa waziri anapokwenda kuzikiwa Canada nje ya nchi yetu je mawaziri wa ngapi wa nchi zingine wamezikiwa bongo?

Je huyu mtu alipokuwa hai, mnawezaje kutuhakikishia kuwa hakuwa kibaraka? vijana hii issue ni nzito mno kuliko mnavyoiangalia I mean how yaani tunawezaje as taifa kuruhusu mambo kama haya na ukizingatia kuwa the man mwishoni alikuwa balozi wetu kwenye sehemu nyeti kama ya ubalozi wa Geneva, jawabu ni kwamba zilikuwa enzi za Mwalimu ndio maana tulikuwa tunaogopa, ndio maana sasa kina Salim ndio hivyo haturudii tena makosa, hakuna excuse ya kiongozi wa nchi yetu ngazi ya uwaziri kuzikiwa nje ya nchi yetu hiyo ni dhana potofu kwa wale mnaoitetea tusijeruhsu kutokea tena!
Balali alizikwa wapi?
 
Back
Top Bottom