My Son drink water
JF-Expert Member
- Nov 30, 2016
- 4,930
- 13,335
Nicolai Cesse cue wa Romania alikuwa na akili kama za jiwe,aliwatesa wananchi wake kwa miaka mingi sana,kila wakitaka kuandamana anawatisha,binadamu hufikia mwisho wa uvumilivu.Hakuna utawala usiofuata misingi ya sheria na haki za raia utaoweza kutawala milele.
Anguko lake huwa ni kubwa sana kiasi kwamba kishindo chake kinaweza kuwafanya viziwi wale ambao hawakutarajia.
Wananchi wakaamua sasa tunaandamana,liwalo na liwe,ilikuwa ni Dec mwaka 1989,wananchi wakaingia mitaani ,kama kawaida jeshi la police likaingia kazini kuwapiga kuwatawanya na kuwakamata,hiyo haikusaidia.
Kila mshale wa saa ulipokuwa ukigonga ndo idadi ya watu kuingia mitaani ilizidi kuongeza,police walianza kuua,mkuu mimi nilikuwa Romania kipindi hicho haya niliyaona kwa macho yangu,nilikuwa na miaka 14,nilikuwa nimeenda huko nikiambatana na raia wa Australia waliokuwa wamenichukua kunisomesha,waliamua mwezi huo kula Xmas na mwaka mpya Romania, nitakuja kuweka thread maalumu humu kuhusiana na tukio lote nilivyoshuhudia Bucharest.
Police walizidiwa,wanajeshi nao wakaingia kazini,kufumba na kufumbua Romania ikaanza kunuka harufu ya mauti,maiti zilitapakaa kila kona,kila sehemu,risasi zilikuwa zinaua watu zikitoka kila sehemu,snipers,walikuwa wengi juu ya maghorofa,waliuliwa kama sisimizi.
Kilichonishangaza idadi ya watu haikupungua mitaani,ndo ilikuwa inazidi kuongezeka,vifaru vilitapakaa mitaani,mwisho wanajeshi wakaanza kurudisha silaha kambini na kuanza kuungana na wananchi kuandamana.
Nicolai na mkewe Helena wakakimbia kutumia Helicopter, bahati mbaya ilipofika mji wa Targovista ikaharibika,ikabidi walinzi wao wateke Taxi ili kutoroka nayo,walienda kama km 10 tu ikaishiwa mafuta,naam,walikamatwa na jeshi na kuchinjwa kwa risasi,