Ameondoka nyumbani

Ameondoka nyumbani

joda

Member
Joined
Apr 7, 2012
Posts
45
Reaction score
12
Mume ameniacha, kaenda kupanga nyumba sehemu nyingine, ananiambia tuachane sababu hatufanani.

Mbaya ananitumia meseji kila siku usiku akiniambia jinsi gani ananimiss na kuwa ni jinsi gani moyo wake unamuuma kwa kuniacha ila inambidi aniache tu.

simjibu. Anaamini baada ya muda haya maumivu yatatuisha na tutaanza upya.

Ananiombea nipate mume mwingine and it is a strong christian marriage.

Nimeumia sana ila sasa naona moyo umeanza kuchukulia kwamba ndiyo hali halisi, ila nimefedheheka sana kujua I married a person mwenye akili za aina yake.

Nilikuwa naamini ana akili njema sana.

Sijui nani kamloga baba mtoto.
 
Point of correction: hiyo sio strong marriage tena, ishavunjika. Maumivu lazima yawepo, kurudi kwenye itafutaji tena na magarasa yalivyo mengi???

Pumzika kwanza, angalia maisha yako kwanza, mapenzi yatajipanga huko mbele kwa mbele.
 
Kama nindoa ya Christianity bado wewe ni mke wake apende asipende
 
Usihofu hata mwana mpotevu alichukua urithi wake akaenda nchi ya mbali kula maisha lakini baadaye akarudi nyumbani ni mwana mpotevu atarudi tu,tulia vumilia atarudi naam atarudi.
 
Makubwaaaaa! Pole mwaya!

DONT GIVE UP YOUR PERSUIT OF YOUR HAPPINESS! DONT LET THE UNGRATEFULL WORLD TURN YOU TO SOMETHING YOU ARE NOT!

It aint your fault shit just happens someyimes!
 
Aliamka tu asubuhi akaondoka? au kuna kitu kilitokea? Ndoa yenu ina muda gani?
 
kuna kitu kinamisss….yaani ahame tu haingii akilini….aidha kuna kitu umemtenda au kapata mwengine….
 
Nenda kwa paroko au mchungaji aliewafungisha ndoa,aitwe,aulizwe,wape taarifa wasimamizi wa ndoa na wazazi,kama atagoma kuwaskiliza,dai talaka yako,iwemahakamani au vyovyote,mkishaachana piga moyo konde anza maisha upya,ili yakimshinda huko,au akiokota magonjwa kwaoooooo na sio kwako,asipokupa talaka akiokota ukimwi wake atarudi kwa mke wake ili umuuguze,kataa hyo kitu mapema,c kakuona hufai atakukumbuka!
 
Miaka 6. hapana alianza drama mbalimbali ambazo hazina sababu ya maana hasa. Alikuwa ananitafutia sababu naona, lakini ni ngumu sana kuipata kwangu. basi akaamua akaondoka, akachukua baadhi ya nguo zake akaenda kuanza new life. every after few days anakuja kwa kigezo cha kumsalimu baby. namuangalia tu.
 
^^
Katika mapenzi, kuna wapenzi wanaitwa rebels! Hawa hawapendi kunyimwa uhuru wao, hawapendi kurudia mambo yale yale nyakati zote, ni wavumilivu wa tabia zinazobadilika. Inapotokea hawaoni mabadiliko kwa wenza wao, huamua kuasi. Huondoka. Huutafuta uhuru wao uliopotea, na huaga! Hilo ndilo lililokupata mleta mada. Kifupi, kwa hulka na silika zao, si rahisi kurudiana. Tafuta mwingine.
^^
 
Pole sana mdada, isije ikawa ulimwambia hakufikishi Mawenzi!
 
Nenda kwa paroko au mchungaji aliewafungisha ndoa,aitwe,aulizwe,wape taarifa wasimamizi wa ndoa na wazazi,kama atagoma kuwaskiliza,dai talaka yako,iwemahakamani au vyovyote,mkishaachana piga moyo konde anza maisha upya,ili yakimshinda huko,au akiokota magonjwa kwaoooooo na sio kwako,asipokupa talaka akiokota ukimwi wake atarudi kwa mke wake ili umuuguze,kataa hyo kitu mapema,c kakuona hufai atakukumbuka!

nakubaliana na wewe, lakini this is a christian marriage, nataka niwe kwenye position nzuri ili hata nikitaka kuquit natoka bila lawama yoyote, and if nikitaka kufanya maamuzi mengine ya mapenzi nisifungwe na kanisa. wazazi, wadhamini wanajua lakini naona wote wamepigwa na butwaa.mchungaji anajua pia nadhani atachukua hatua.ila sijui.. Ukimwi mmmh atajiuguza alipoupata and i wont share his viruses.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom