amenisihi nisiseme, lakini roho inaniuma

amenisihi nisiseme, lakini roho inaniuma

hizi statement zinasuggest kwamba mama hajui mume anaenda nje



on topic: nimeona wanaume wengi tunashauri kijana akae kimya na tunaona its okay dad ku-cheat because ni mzazi wa kiume, Je if the situation was reversed mngeshauri the same??

Na mimi nimejitahidi kufikiria nimesa jibu. Na nimepata majibu mengine kwamba wanaume wengi wa kitanzania kufanya ngono nje ya ndoa zao ni sifa mojawapo and they are proud of it. Na wengine wamenitia uzuni kulinganisha uzinzi wa baba na mtoto kuwa sawa...Swali wanaume mliochangia humu mlianza ngono mkiwa kwenye ndoa? I real hate hypocracy duh mmezidi. Kijana usimwambie mama lakini hakikisha baba anapata fundisho na wewe jifunze makosa kutoka kwa baba yako HIV/AIDS ipo inasubiri wadau.
 
We mwambie dingi asilete maukimwi home tu hayo mengine uchune!
 
MUNGU kakuweka kwenye hio familia uwe msaidiz wa wazaz na ww pia ndo mpatanish kama vp simamia haki na uutetee uovu koz mamako akijua hukumshtua hata kuamin teeeeeena
 
Dr umenchekesha!
Kwani hata mama akimconfront ndo mzee ataacha kabisa uzinzi?( manake hapo lazma aruke futi 100)
wangapi wanafumaniwa na wanaruka futi mia. Na mwisho.wa siku anahamia pengine?
Dawa hapo dogo amchimbe mkwara dingi kuhusu hiv, na kutunza heshma ya familia. Na ahame home manake.anakula ugali.wa.shkamoo anaafford kulipia ngono gesti.
Sasa siku moja mama yenu anawaita wanae wote...kisha anwaambia wanangu nimetoka hospitali leo, nimepima nimekuwa nimeambukiwa VVU (HIV)! If you can live with that, usimwambie...lakini jua kwa kutom'warn mama, unamchimbia kaburi!
 
Huna haja ya kuumia. Mwendee baba yako umwambie unavyojisikia na kumshauri aache usharobaro maana kwa umri wake anaweza kuleta miwaya na talaka bila sababu na famili aikaathirika.
 
Nimetfakari sana, nakuona kama si utoto basi ufahamu wako ni mdogo sana. Je, siku utakayomuona mama yako naye utafanyaje?
Akimuona mama yake atamwambia uchune kwani yule sio baba yako mzazi nilimsingizia kuwa wewe mwanae
Kizazi cha zinaa kitakuwa zinaa,Isije kuwa iko kishitobe chenyewe ni dada yake(Hizo ndio faida za kupiga nje)
 
dah mwana umepata leverage kubwa sana hapo...sasa mdingi atakuwa mtumwa kwako. wewe usimwambie maza. kuna siku utatumia hiyo infomation kupata kitu....ata ikiwezekana unaweza mwambia na mie nataka kuonja K ya yule mwanamke lah sivyo namwambia maza

Mkuu hapo kwenye nyekundu nimecheka hadi nikataka kumeza monita lol...........Wewe ni kiboko, kwamba dogo anaeza akataka kupita alipopita mdingi wake hahahahahhaaa.
 
We funga kidomo domo hicho, kwanza huyo faza wako ni karne gani??? Eti anakukuta dogo gesti halafu anaomba msamaha!!! Chezeya wazee wa dizaini ya baba yangu wewe, yaani kwenye situation kama hiyo kwa baba yangu wewe mtoto ndiyo ingekula kwako mbaya. Eti umwambie mama, ili???????
 
Habari za leo wana JF,
naombeni ushauri nifanyeje katika hili, maana linanikosesha raha kabisa.
ni Jmosi ya juzi baada ya mim kupata vihela vya tempo ninayopiga kiaina, ikabidi nitoke kidogo na shemeji/wifi yenu mitaa fulan hapa DSM. mie ndo nimemaliza chuo na yeye ndo anaingia 3rd yr. mida ya kama saa mbili hivi baada ya kumaliza starehe zetu, natoka tu kunako nyumba ya wageni namuona dingi laivu nae akitoka the opposite room na mwanamke ambaye simfahamu.
tukaonana uso kwa uso na mshua, akapigwa na butwaa. sikusema kitu nikasepa fasta na kuondoka na girl wangu.
bado naishi home, si unajua mambo hayajakaa sawa kuweza kupata apartment yangu, nilifika home mida ya saa 4 hivi nilimkuta dingi keshafika. nilifika na kuingia chumbani kwangu, dingi naye akaja fasta na kuniambia nisiseme kitu kwani mie nishakua na hayo ni mambo ya kawaida.

sasa namuonea huruma mama yangu, naona kama simtendei haki.., mimi kujua upuuzi wa baba nisimwambie inanuima sana,.
kwa upande mwingine naona nikisema italeta ugomvi mkubwa na mimi kwa namna moja au nyingine, nitakuwa chanzo cha ugomvi huo.
leo hata sijapanda gari lake, maana nasikia hasira hata kuongea nae.
naombeni ushauri wadau....,

he wewe vipi bado hujakua na kuwa na familia
ukikua utaona kuwa hivo ni vijimambo tu vya ukubwani
we uchune bana mtoto wa kiume unatakiwa uwe nakifua na kuhimili mambo
ina maana wewe hujawahi kucheat??
 
Habari za leo wana JF,
naombeni ushauri nifanyeje katika hili, maana linanikosesha raha kabisa.
ni Jmosi ya juzi baada ya mim kupata vihela vya tempo ninayopiga kiaina, ikabidi nitoke kidogo na shemeji/wifi yenu mitaa fulan hapa DSM. mie ndo nimemaliza chuo na yeye ndo anaingia 3rd yr. mida ya kama saa mbili hivi baada ya kumaliza starehe zetu, natoka tu kunako nyumba ya wageni namuona dingi laivu nae akitoka the opposite room na mwanamke ambaye simfahamu.
tukaonana uso kwa uso na mshua, akapigwa na butwaa. sikusema kitu nikasepa fasta na kuondoka na girl wangu.
bado naishi home, si unajua mambo hayajakaa sawa kuweza kupata apartment yangu, nilifika home mida ya saa 4 hivi nilimkuta dingi keshafika. nilifika na kuingia chumbani kwangu, dingi naye akaja fasta na kuniambia nisiseme kitu kwani mie nishakua na hayo ni mambo ya kawaida.

sasa namuonea huruma mama yangu, naona kama simtendei haki.., mimi kujua upuuzi wa baba nisimwambie inanuima sana,.
kwa upande mwingine naona nikisema italeta ugomvi mkubwa na mimi kwa namna moja au nyingine, nitakuwa chanzo cha ugomvi huo.
leo hata sijapanda gari lake, maana nasikia hasira hata kuongea nae.
naombeni ushauri wadau....,

Poleni sana! wewe unafikiri mama yako hajui? wanawake wana akili acha kabisa, mama yako anajua kabisa, huna haja ya kumwambia, kwani unaweza kuleta matatizo makubwa sana. Cha msingi jipange uhame home.
Kweli mtoto wa nyoka ni nyoka.
 
nashukuru sana wana JF kwa ushauri wenu. walio wengi wamenishauri kukaa kimya, na kuongea na baba yangu aachane na tabia hiyo. nazingatia ushauri wenu kwa dhati kabisa, chuki dhidi ya mshua imepungua saiv japo haijaisha kabisa.
nitajitahidi niserve pesa nipange walau chumba kimoja mitaa tofauti na home, then nitasema na mshua kuhusu tabia ile.
 
iko siku wote mtakutwa na ukimwi halafu tutasubiri nani anaanza na nani anafuatia,hata hivyo pole kwa stress.
 
Dogo acha kupanick wewe...huoni kama unafuata nyayo za babako?...wewe hujao na unaishi kwa babako na unaenda guest house kugonga...matokeo yake umekutana na mshua....like father like son.

Kuhusu kusema kwa mama au kutokusema kwa baba unaweza kusikiliza wimbo wa dogo asley na kufuatilia video yake naamini utauacha umasikini soon... Mchimbe mkwara mshua kuwa unaenda kusema kwa mama uone utavyokuwa unasikizwa na kupewa pesa zisizokuwa na sababu ya msingi.

pia unaweza kujiongeza ki-busara na kumface mamako na kumsisitiza awekaribu na mshua na asimpe nafasi ya kujivinjari mwenyewe maana "umesikia wanawake wa mtaani kwenu na vibinti vinanyatia babako kisa eti ni handsome mpaka anazeeka na u-handsome wake" .. Bi mkubwa atakuelewa na ataanza kukaba ipasavyo na penzi lao litarudi kama zamani.

ila za mbayuwayu..changanya na za kwakoooo
 
Na swali huyu mzee akileta ukimwi au hawara wa pembeni wakirudisha nyuma maendeleo ya nyumbani kwao??? Maisha ya zamani ni historia siku hizi kuna magonjwa hatari siyo kama enzi hizo, naandika hivi nikifahamu wanaume ndani ya ndoa wana cheat tena sana lakini lazima mkumbuke huyu ni dogo na anakuwa affected kisakolojia kwa hivyo hili suala siyo la kutoa majibu juu kwa juu.

PS: Hadi namaliza kuandika hapa nakiri sina jibu sahii la kumpa huyu dogo wa chuo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom