Ameni-dump kwa mara ya pili

Ameni-dump kwa mara ya pili

Halafu watu cjui hawaelewi au nivipi ukweli nihuu Mapenzi yakweli niyale ya mwanzo lkn mkipoteana then mkutane uctegemee kuwa km zamani huwa naangaliaga hata ushauri mwingi unaotolewa humu khs watu waliotemana Kuwaambia warudiane fyn mnaweza kurudiana lkn hakuta Kuwa na mapenz mtaishi kwa mazoea tu,,nakuckitikia ww mdada hata km huyo jamaa angekurudia kweli lkn ucngefurahia mapenzi Mapenz yanakuwaga matam pale ambapo kila mmoja hajui mapungufu ya mwenzie

Maneno yana ukweli Fulani.
 
amechezeaje moyo wako sasa, au umejichezea mwenyewe kwa akili zako
 
Maneno yana ukweli Fulani.

Nashukuru km umepata kitu hapo Ninachowakubali nyie wanawake hamnaga chakuogopa kupima nenda kachek Afya then endelea na Maisha ucpoteze muda kumfikiria huyo mwadamu atakutaabisha nafsi hadi ujute kwanini umemfahamu
 
Pole dada, acha kujilaumu kwa yaliyotokea ila uwe makini na mwangalifu katika haya mambo ya mahusiano hasa unapokutana na mpenzi wa zamani.

Naona tatizo hapa katika mtazamo wa wasichana wengi.

1. Mahusiano hufikia mwisho ; watu wengi wamekwama kwenye imani kwamba mahusiano hayana mwisho, ukweli ni kuwa mahusiano hufikia mwisho kwa sababu nyingi tu bila kujali kama upo tayari kuona mahusiano yakifa au la. Na ni ngume sana kurudisha mahusiano baada ya miaka mingi kiasi hicho.

2. Kufanya tendo la ndoa sio tiketi ya kurudisha mahusiano; kwa sisi wanaume unapokutana na mpenzi wa zamani kitu cha kwanza kinachokuja akilini ni kumbukumbu za ngono. Hapa haijalishi yupo kwenye mahusiano mapya au la, mwanaume akikwambia ''I miss u'' ni sawa tu na kukwambia ''nahitaji tukumbushie mambo yetu yaleeee''..

3. Chukua tahadhali Mwananume anapokuonyesha kujali na kukupenda baada ya kuachana naye kwa muda mrefu;
Wanaume ni watu wa mipango sana, kama tunahitaji kitu kwa mwanamke hasa mpenzi wa zamani huwa tupo tayari ku-pretend kwa kiwango cha juu. Kama nipo nje ya nchi naweza kukuletea hata zawadi ya thamani sana ili tu nitimize lengo na nia yangu.

4. Wanaume hatuwaamini sana wapenzi wetu wa zamani, mkiisha achana na mwanaume basi kaa ukijua kuwa huwa hawana mpango tena wa mahusiano mengine ya kudumu pamoja nawe.

 
"Nimejiona mpumbavu sana kumruhusu binadamu huyu kuchezea moyo wangu kwa mara ya pili"

mi nimenote hii tu
 
Back
Top Bottom