Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 58,636
- 220,350
Amenidump kwa mara ya pili. Nilikiuwa na mahusiano na mwanaume huyu kwa miaka mitano kabla hajaniacha na kwenda kuoa. Nilipoteza mawasiliano nae kabisa na kumfuta kwenye moyo wangu. Ndoa yake ilisambaratika akaanza kunitafuta tena, alirudi mwaka 2010 lakini moyo wangu ulisita kumpokea tena.
Yeye anaishi Songea ndio anakofanyia kazi, katiak hali ya kibinadamu nilisema nisiweke kinyongo rohoni, nikawa ninachat nae. Wiki mbili zilizopita alinitaarifu kuwa anakuja kwenye mkutano DSM na angependa tuonane. Nilionana nae, tuliongea sana, mwisho wa siku nilikuwa ninalala kwenye hoteli aliyofikia, asubuhi ninakwenda kibaruani kwangu.
Mkutano ulikuwa ni wa wiki moja, nikajua tunafungua ukurasa mpya wa maisha, tuliongea, nikamwonyesha sehemu mpya za maraha ya jiji. Baada ya mkutano kwisha, amerudi Songea amekuwa mvivu wa kuchat, nikipiga simu, hapokei, mwisho wa siku amenitolea uvivu kuniambia anauhusiano mwingine huko kwahiyo hataweza kuwa na uhusiano mwingine na mimi.
Nimejiona mpumbavu sana kumruhusu binadamu huyu kuchezea moyo wangu kwa mara ya pili.
Yeye anaishi Songea ndio anakofanyia kazi, katiak hali ya kibinadamu nilisema nisiweke kinyongo rohoni, nikawa ninachat nae. Wiki mbili zilizopita alinitaarifu kuwa anakuja kwenye mkutano DSM na angependa tuonane. Nilionana nae, tuliongea sana, mwisho wa siku nilikuwa ninalala kwenye hoteli aliyofikia, asubuhi ninakwenda kibaruani kwangu.
Mkutano ulikuwa ni wa wiki moja, nikajua tunafungua ukurasa mpya wa maisha, tuliongea, nikamwonyesha sehemu mpya za maraha ya jiji. Baada ya mkutano kwisha, amerudi Songea amekuwa mvivu wa kuchat, nikipiga simu, hapokei, mwisho wa siku amenitolea uvivu kuniambia anauhusiano mwingine huko kwahiyo hataweza kuwa na uhusiano mwingine na mimi.
Nimejiona mpumbavu sana kumruhusu binadamu huyu kuchezea moyo wangu kwa mara ya pili.