Ally Salum Hapi, Ukweli huishi milele daima kaka.!

Ally Salum Hapi, Ukweli huishi milele daima kaka.!

Mna ifahamu katiba ya urusi!!?
Mna ifahamu katiba ya Saudi Arabia!!?
Unafamu katiba ya Rwanda!!?

Zote hizo zili pitishwa na wananchi na bado zinapo fuatwa , watu wanao tumia maana ya Liberal democracy wanaona hakuna demokrasia kwenye nchi hzo
Ndio maana nika waambia huwezi kusema kuna maana moja tuu ya demokrasia
Ni dhana pana kuliko mnavyo ifahamu
Mkuu katiba za hao watu hazina demokrasia yeyote, hawa watawala hutumia mabavu kushawishi watu kujitengenezea katiba. Kwa maana halisi ya demokrasia tafsiri iko wazi. Huwezi kunukuu maneno ya Mwanamfalme wa Saudia au Kagame wa Rwanda ukaridhika ukasema kweli hii ndio maana halisi ya demokrasia. Lakini tizama wamarekani, Wajerumani na Waingereza halafu tafsiri maana halisi ya demokrasia kwa ujumla wake.
 
Ipo siku yatakwisha kwani kila lenye mwanzo lina mwisho
 
Definition hiyo hutumiwa kwa maana ya kutambuliwa, ila haitumiwi kama definition pekee au definition sahihi zaid ya democracy kuwahi kuwepo duniani

Ila nna i credit kwa kutoa definition ya mtazamo wa ki liberali katika demokrasia, japo bado ina ombwe kubwa tuu la kimantiki hata hivo
Sio kwa maana ya kutambuliwa tu bali ndiyo akisi ya maana na ndio ukweli wenyewe. Hizi maana zingine watu wanajiundia tu kujihalalishia haramu.
 
Jambo kubwa kuliko ni kuwa watoto wanasikia na kuamini Tv zaidi kuliko hata vitabu. Sasa kama ataulizwa swali juu ya maaana ya demokrasia na akatumia jibu la uwongo lililotolewa na kiongozi wake kama Ally Happy kwenye Tv itakuwa sahihi kumlaumu mwalimu au kiongozi na wanasiasa kama huyu?
 
Mkuu katiba za hao watu hazina demokrasia yeyote, hawa watawala hutumia mabavu kushawishi watu kujitengenezea katiba. Kwa maana halisi ya demokrasia tafsiri iko wazi. Huwezi kunukuu maneno ya Mwanamfalme wa Saudia au Kagame wa Rwanda ukaridhika ukasema kweli hii ndio maana halisi ya demokrasia. Lakini tizama wamarekani, Wajerumani na Waingereza halafu tafsiri maana halisi ya demokrasia kwa ujumla wake.
Hapo ndo unapo kosea katiba ya Rwanda ilipitishwa na wana nchi tena kwa zaidi ya asilimia 90, na wewe ulisena kufuatwa kwa matakwa ya watu na katiba kwa definition yako kagame ata angukia hapo.

Demokrasia ilianzia ugiriki, lakini hata kina Aristotle na Plato wana onesha kuwa hakuna aina moja ya demokrasia na demokrasia siku zote ime kuwa na tabia moja tunaiita "Exclusionism" hii ipo kote
Kwa hiyo dhana ya ki demokrasia ya Uingereza na Marekani ni moja tuu ya dhana hizo ila si dhana pekee.

Msome jamaa anaitwa Barker Ernest kaandika Kitabu kizuri cha mawazo ya Aristotsle na Plato
 
Ni kama zile akili mbovu za watu flani ambao huwaambia wake zao wasiende popote wala wasihoji lolote kwa kisingizio kwamba, kula unakula vizuri, unavaa vizuri, watoto nakuzalisha, sasa unataka nikupendeje, ndivyo maccm yalivyo, yanadhania kula kuvaa na kulala ndo demokrasia.
 
Sio kwa maana ya kutambuliwa tu bali ndiyo akisi ya maana na ndio ukweli wenyewe. Hizi maana zingine watu wanajiundia tu kujihalalishia haramu.
Nakubalina na wewe kwa fikra zako za demokrasia
Lakini nakubaliana pia na happi kwa fikra zake .wote mko sahihi inategemea tuu mitazamo yenu ine egemea wapi, basi

Na ndo kaz yetu sisi tunao waangalia nyie mlio kwenyw shule mbali mbali za fikra, mwisho tuna stay neutral

BAK
 
Kwa kweli nami nilikitazama hiko kipindi kwa kweli nilishangaa sana. Sijui watu wanaogopa sema ukweli hata Kama wanaujua au wanalinda nafasi zao
Ugali wake mweeeeh
 
Aibu hii itawala milele mana siku zinakuja ambapo upotoshaji huu utatumiwa kama reference kuonyesha namna tabaka tawala linavyotumia madaraka yake kupotodha umma ambao majority ni illiterate
 
Demokrasia ni dhana ambayo haina tafsiri moja, na hakuna maana moja ya demokrasia inayo kubalika na dunia nzima
Labda useme ulitaka aongelee demokrasia kwa mtazamo wa ki magharibi, hapo uta kuwa sahihi.
Tafsiri ya Gaddafi ilikuwa ina mashiko yake lakini, ilikosa vinasaba vya u magharibi na watu wake ndio walitaka wawe na demokrasia kama hiyo ndio waka mtoa.
Hapi alikuwa sahihi ila si kwa mtazamo wa ki magharibi. Na wewe uko sahihi ila si kwa mtazamo wa ki jamaa, na ki dhahania nyingine za demokrasia
Jifunze kuweka point mwanzoni, uko vizuri mkuu.
 
Usikubali kupotoshwa na hawa wahuni wa CCM ambao hawataki katiba mpya ya rasimu ya Warioba kwa kuhofia kwamba ndiyo itakuwa mwisho wa uhai wao katika anga za siasa nchini, hawataki Tume huru ya uchaguzi kwa kuhofia kushindwa kuiba chaguzi nchini kama wanavyofanya sasa bara na visiwani na hivyo kuja na definition yao uchwara kwa sababu tu inakidhi matakwa yao ya kukwepa katiba mpya ya rasimu ya Warioba na tume huru ya uchaguzi ambayo itafanya maamuzi yake ikiwa huru bila ya kuingiliwa na yeyote yule kwa kuhofia uteuzi wao kutenguliwa (kutumbuliwa)

Nakubalina na wewe kwa fikra zako za demokrasia
Lakini nakubaliana pia na happi kwa fikra zake .wote mko sahihi inategemea tuu mitazamo yenu ine egemea wapi, basi

Na ndo kaz yetu sisi tunao waangalia nyie mlio kwenyw shule mbali mbali za fikra, mwisho tuna stay neutral

BAK
 
Madaraka hulevya .
Ndugu zangu nimeona watu wengi wanamshambulia huyu kijana ambaye kwa kweli ameeleza vizuri maana ya demokrasia anayoielewa yeye sasa kosa lipo wapi? Tafsiri ya demokrasia haipo moja, ukisoma vitabu mbalimbali vya social science, community development, human resources, politics, livelihood na vingine vingi kila kimoja na kwa waandishi mbalimbali wana tafsiri tofauti. Demokrasia haina tafsiri moja, zipo nyingi inategemea wewe unaiamini ipi!!!
 
Si ajabu mtu akiibuka na kusema awamu hii imeua wasomi wetu au ina mpango wa kuchukua kile walichonacho kichwani

Ukiniita mchochezi mimi siujui uchochezi
 
Huwezi KAMWE ukamwambia mwananchi wa nchi yoyote ile mimi nakupatia huduma zako muhimu zote uzitakazo lakini huna haki ya kuandamana, kukutana na wananchi wenzio wa vyama tofauti na chama A, kuchagua viongozi uwatakao kwa kuwa chama A kitafanya kila hila kuiba chaguzi na hivyo kumnyang'anya huyo mwananchi haki yake ya kuwachagua viongozi awatakao, na kuwepo katiba ambayo inalinda maovu yote ya viongozi wa chama A, halafu ukaita hiyo nayo ni demokrasi.

Waandishi wa vitabu kwa kutaka kujinufaisha hupindisha maana halisi ya neno demokrasi kwa kujua fika kwamba kuna soko la kuuza vitabu vyao ambavyo vimepotosha maana halisi ya neno hilo.

Ndugu zangu nimeona watu wengi wanamshambulia huyu kijana ambaye kwa kweli ameeleza vizuri maana ya demokrasia anayoielewa yeye sasa kosa lipo wapi? Tafsiri ya demokrasia haipo moja, ukisoma vitabu mbalimbali vya social science, community development, human resources, politics, livelihood na vingine vingi kila kimoja na kwa waandishi mbalimbali wana tafsiri tofauti. Demokrasia haina tafsiri moja, zipo nyingi inategemea wewe unaiamini ipi!!!
 
Tafsir ya abraham lincolin ni tafsir iliyobase kwenye ideas za kibepar ie ndani yake ilikuwa nasura ya vita baridi.

Wajamaa nao walijiita wanademokrasia kwamtazamo wakiuchumi kwakuwa wao walikuwa wanatengeneza usawa ktk umiliki.
##dhana ya demokrasia nisawa nashimo lisilojulikana uhalisia wake wa ndani,ukiingia utakutana na moto mkali##
 
Demokrasia ni dhana ambayo haina tafsiri moja, na hakuna maana moja ya demokrasia inayo kubalika na dunia nzima
Labda useme ulitaka aongelee demokrasia kwa mtazamo wa ki magharibi, hapo uta kuwa sahihi.
Tafsiri ya Gaddafi ilikuwa ina mashiko yake lakini, ilikosa vinasaba vya u magharibi na watu wake ndio walitaka wawe na demokrasia kama hiyo ndio waka mtoa.
Hapi alikuwa sahihi ila si kwa mtazamo wa ki magharibi. Na wewe uko sahihi ila si kwa mtazamo wa ki jamaa, na ki dhahania nyingine za demokrasia
Upotoshaji wa makusudi!! unajichetua au huelewi?
 
Mtu anaeleta mfano wa gadafi huwa naona kama halewi ulimwengu unavyokwenda
 
Back
Top Bottom