Mwizukulu wa Buganda
JF-Expert Member
- Nov 19, 2024
- 810
- 2,039
Kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania na majukumu ya Bunge, mbunge hana mamlaka ya kukusanya kodi, kuidhinisha matumizi ya fedha moja kwa moja, kuajiri watendaji au kutekeleza miradi. Majukumu yake makuu ni:
Je, kauli za viongozi hawa ziko sahihi?
1. Kauli ya Hayati Magufuli:
"Mkichagua upinzani sitoleta maendeleo"
Kikatiba, utekelezaji wa maendeleo ni jukumu la Serikali kupitia bajeti, wizara, taasisi za umma na mamlaka za serikali za mitaa. Hivyo maendeleo hayapaswi kutegemea chama cha mbunge aliyeshinda eneo husika. Kimsingi wananchi wote wanastahili huduma za serikali bila kujali chama walichokichagua.
2. Kauli ya John Heche:
"Kazi ya mbunge si kuleta maendeleo, hakusanyi kodi"
Kauli hii ina ukweli lakini tutambue kuwa Mbunge si mtendaji wa Serikali wala mkusanyaji wa kodi. Barabara, hospitali, maji na shule hujengwa na Serikali kupitia fedha za walipa kodi. Mbunge hana bajeti ya kutekeleza miradi hiyo moja kwa moja.
3. Kauli ya Ali Hapi:
Kazi ya mbunge ni kuleta maendeleo kwa kutumia nafasi zake bungeni kuwasilisha mahitaji ya wananchi
Zaidi soma Ally Hapi: Heche hajui wajibu wa mbunge, CHADEMA ni waongo, hawajui wajibu wao, hawajui sheria, hawajui taratibu za nchi
Hii pia ina ukweli. Ingawa mbunge hajengi mradi mwenyewe, ana wajibu wa kupigania mahitaji ya jimbo lake kwa kuhoji serikali, kushawishi mgao wa fedha, kujadili bajeti na kufuatilia utekelezaji wa miradi. Lakini ataweza vipi kuleta maendeleo ikiwa Serikali itaamua kutopeleka maendeleo eneo lake. Hii changamoto hasa imekuwa ikiwakuta wanabunge wanaotoka vyama pinzani ikiwa ni namna ya kuwakomoa ili wasiaminiwe na wananchi uchaguzi ujao.
Hivyo, kiuliza nani "analeta maendeleo", jibu sahihi zaidi ni Serikali kwani ndiyo mtekelezaji mkuu wa maendeleo. Mbunge ni mwakilishi na msimamizi anayepaswa kuyapigania na kuyafuatilia. Chama tawala huathiri maendeleo kupitia sera zake kwa kuwa ndicho kinachounda serikali.
- Kuwakilisha wananchi;
- Kutunga sheria;
- Kuisimamia na kuishauri Serikali;
- Kushiriki kujadili na kuidhinisha bajeti na mipango ya maendeleo.
Je, kauli za viongozi hawa ziko sahihi?
1. Kauli ya Hayati Magufuli:
"Mkichagua upinzani sitoleta maendeleo"
Kikatiba, utekelezaji wa maendeleo ni jukumu la Serikali kupitia bajeti, wizara, taasisi za umma na mamlaka za serikali za mitaa. Hivyo maendeleo hayapaswi kutegemea chama cha mbunge aliyeshinda eneo husika. Kimsingi wananchi wote wanastahili huduma za serikali bila kujali chama walichokichagua.
2. Kauli ya John Heche:
"Kazi ya mbunge si kuleta maendeleo, hakusanyi kodi"
Kauli hii ina ukweli lakini tutambue kuwa Mbunge si mtendaji wa Serikali wala mkusanyaji wa kodi. Barabara, hospitali, maji na shule hujengwa na Serikali kupitia fedha za walipa kodi. Mbunge hana bajeti ya kutekeleza miradi hiyo moja kwa moja.
3. Kauli ya Ali Hapi:
Kazi ya mbunge ni kuleta maendeleo kwa kutumia nafasi zake bungeni kuwasilisha mahitaji ya wananchi
Zaidi soma Ally Hapi: Heche hajui wajibu wa mbunge, CHADEMA ni waongo, hawajui wajibu wao, hawajui sheria, hawajui taratibu za nchi
Hii pia ina ukweli. Ingawa mbunge hajengi mradi mwenyewe, ana wajibu wa kupigania mahitaji ya jimbo lake kwa kuhoji serikali, kushawishi mgao wa fedha, kujadili bajeti na kufuatilia utekelezaji wa miradi. Lakini ataweza vipi kuleta maendeleo ikiwa Serikali itaamua kutopeleka maendeleo eneo lake. Hii changamoto hasa imekuwa ikiwakuta wanabunge wanaotoka vyama pinzani ikiwa ni namna ya kuwakomoa ili wasiaminiwe na wananchi uchaguzi ujao.
Hivyo, kiuliza nani "analeta maendeleo", jibu sahihi zaidi ni Serikali kwani ndiyo mtekelezaji mkuu wa maendeleo. Mbunge ni mwakilishi na msimamizi anayepaswa kuyapigania na kuyafuatilia. Chama tawala huathiri maendeleo kupitia sera zake kwa kuwa ndicho kinachounda serikali.