ALJazeera USA, iwe fundisho kwetu!

ALJazeera USA, iwe fundisho kwetu!

Mleta mada hii kwanza ungeangalia historia ya Al Jazeera maana hao Al Jazeera walianza na vipindi vyao vya kiarabu wakiwa Emirates na walikuwa wanarusha udhalimu wanaoufanya waisrael kwa wapalestine na habari zilikuwa ni mbaya mpaka wakalipua kituo chao cha utangazaji. Ndipo wakahamia Doha.

Baadae wakaomba wapatiwe leseni ya matangazo kwa lugha ya kingereza lakini walipewa masharti mengi yakiwemo ya kutokuweka matokeo live ya mateso ya Palestinians.
Ilikuwa wakati huo walikuwa wanaweka askari wa Israel wanawavunja mikono kwa tofali watoto wa kiarabu na wanaweka live lakini ilikuwa kwa kiarabu walipopewa kurusha kiingereza ikawa hakuna tena ila habari wanazotaka wao wazungu
 
Ila ukweli mjue kua hakuna media house hata moja duniani,narudia tena HATA MOJA duniani iliyo neutral kwenye ajenda zakr.kila media iko biased kwa upande flani chunguza utaona.

Hapo uko sahihi, hawa wote hata CNN, BBC n.k. ni wanafiki tu.
 
Watanzania ila tumezidi, mimi huwa naenda hapo jirani tu Kenya, huwezi kuta mkenya anatzama sijui StarTV, itv , au EATV, hata hiyo EATV ina jila la kiafrica mashariki but ukienda Kenya na uganda hakuna mtu anaye tazama. sasa njoo Bongo, Watanzania wengi sana wanatazama TV za kenya, na hata magazeti ya kenya yanauzwa sana Tanzania but nenda Nairobi kama utakuta hata The Guardian,
 
Pamoja na kutokuwa na uhuru wa vyombo vya habari,tunaweza kuwa na stesheni kama aljazeera ambazo zinatoa taswira ya dunia kwa maono ya mwaraabu? BBC inatoa taswira ya dunia kwa macho ya mwingereza,vilevile DW kwa wajerumani.


Think about it.
 
Back
Top Bottom