TANZIA Aliyewahi kuwa Waziri na Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL, Omary Nundu amefariki dunia

Tunaoamini katika ufufuko halisi.. Tunaamini kuna siku atafufuka na kujumuika na wafu wengine waliofufuka katika Kristo... Rip brother.. Until we meet again
 
Hapana hajawai kua mkuu wa mkoa. Amefanya kazi nchini miaka ya zamani baadae akaenda nje mpaka 2010 aliporudi na kugombea ubunge tanga mjini baadae akawa waziri wa uchukuzi na alipoondolewa alibaki kua mbunge mpaka 2015 aliposhindwa uchaguzi mkuu. Wakat wa awamu ya tano aliteuliwa kua mwenyekiti wa bodi ya TTCL baadae akateuliwa tena kua mwenyekiti wa bodi ya Aitel.
Aliwahi kuwa mkuu wa mkoa wa tanga miaka ya 2010
 
Ni yupi kati ya hawa

omar.JPG


nundu.jpg
 
Huyu ndie aliyetudanganya na kutuaaminisha kuwa Airtel ni mali ya Serikali kumbe muongo mkubwa. Walikuja wahindi wenye kampuni yao, sijui porojo zake ziliishia wapi?
Kweli mawazo ya kuwa AIRTEL ni mali ya Serikali na toka 2017 ameshindwa kuprove hivyo yanaweza kuwa yalimletea sonona (depression). RIP Nundu
 
Inna lillah wainna ilaih rajiun. Allaah akupe kauli thabit babu yetu, na akufanyie kaburi lako kuwa bustani miongoni mwa bustani za peponi.
 
Waziri wa zamani nchini Tanzania, Omary Nundu amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Hospitali hiyo imethibitisha.

> Mnamo tarehe 27 February 2017 Rais Magufuli alimteua Omary Nundu kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la TTCL.

> Nundu aliwahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Tanga kuanzia mwaka 2010 hadi 2015

Historia Ya Marehemu, Omary Nundu

Omari Rashid Nundu, alizaliwa Tanga, Tanzania mwaka 1948 na huko ndiko alikopata elimu yake ya shule kabla ya kujiunga na Chuo Kikuu cha Glasgow, Scotland mwaka 1971 kusomea uhandisi na sayansi ya vyombo vya anga (Aeronautical Engineering); na baadaye kuendelea na shahada za juu na utafiti vyuo vikuu vya Cranfield, England na Concordia, Canada.

Omari amebahatika kufanya kazi kwenye taasisi mbalimbali duniani katika kuitendea haki taaluma hiyo aliyoisomea na anayoipenda. Kwa nyakati mbalimbali alikuwa mhandisi na mkurugenzi kwenye mashirika ya ndege, alikuwa mshauri na mhadhiri kwenye vyuo vya kimataifa, na pia alikuwa mkuu wa vitengo vya usafiri wa anga katika jumuia za kimataifa.

Kabla ya kurejea Tanzania na kuwa mbunge wa Tanga na pia Waziri wa Uchukuzi katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alikuwa Rais wa jopo la kimataifa la magwiji wa taaluma ya Usafiri wa Anga Duniani (Air Navigation Commission) kwa miaka miwili mfululizo

Ingawa ni mhandisi na mwana sayansi aliyebobea, Omari anapenda kuongea lugha mbalimbali lakini ana mapenzi ya dhati kwa lugha ya Kiswahili ambayo ndiyo iliyomkuza. Hivyo basi kuwa yeye ni malenga wa mashairi halishangazi. Utenzi uliomo mwenye kitabu hiki unajaribu kusimulia maisha na mwenendo wa Dunia kwa kadri alivyoyashuhudia mhandisi huyu hadi mwaka 2015.
Apumzike kwa amani Mzee wetu Omary ibn Nundu. Namkumbuka wakati akiwa Waziri wa Uchukuzi na jinsi alivyopambana na Naibu Waziri wake Eng. Mfutakamba baada ya kuwa Naibu Waziri anamzunguka mkuu wake. Mzee alitoka hadharani na kukemea; alithubutu
 
Inawezekana kweli kulikuwa upigaji hela za matibabu ya nje lakini si vizuri kusema Watanzania wote watatibiwa hapa hapa. Hili wimbi la viongozi au wake wa viongozi kufariki mikononi mwa madaktari wetu limekuwa kubwa.

Hivi kweli huyu Dr Harrison Mwakyembe na Prof Mwandosya wangekuwa wameugua kipindi hiki cha Meko wangepona na kurejea kwwnye afya walizonazo leo kwa huduma za MNH? Last month mke wa AG Killangi alikufa pia.

Ikibidi kiongozi aende nje kwa matibabu nashauri aende tu, ila kama kuna mtu anataka kupiga hela, adhibitiwe mbona mifumo ipo.
 
Back
Top Bottom