Aliyewahi kuutesa moyo wangu ananitaka

Kwa kweli mke wangu nampenda sana na ndiye hasa alinifanya nisahau machungu ya huyo wa uropa. Sijisikii raha hata kidogo kuumiza moyo wake kwani naye ananipenda kwa dhati na kuniheshimu sana na sikosi chochote kwake.

ewaaa..nimefurahi kuckia hayo! sasa ucmpe nafac tena huyo hta ya dk 2...tunza familia yako.
 
vituko, vituko na dharau zako,
ukahadaika na mpita njia,
sasa unataka kwangu kurejea,

i am sorry, kwangu kumejaa,
urudi huko huko, ume expire,
zamu yako imekwishaaaaaaaaaaaaaa
 
aaahh bana, acha kumtisha mwenzako bana. Anasema anamjua tangia 'primary', sasa wewe unaleta mambo ya kutishiana shetani, aaaarrggghhh
Hatujajua upande wa pili wa shillingi kwa nini mdada alisepa hapo awali...

Msome tena Mheshimiwa balozi alivyokua excited;

  • mdada karudi 'fresh!'
  • mdada alikoipata cellular number yake,
  • mdada alivyozidi 'kunona'
  • mdada haoni wala hasikii!
Teh teh teh! Mheshimiwa Mbu nadhani nilishangaa kuliko nilivyokuwa excited!
 
Umekumbusha ule wimbo wa Mwanameka wa Marijani Rajabu (RIP)!
 
vituko, vituko na dharau zako,
ukahadaika na mpita njia,
sasa unataka kwangu kurejea,

i am sorry, kwangu kumejaa,
urudi huko huko, ume expire,
zamu yako imekwishaaaaaaaaaaaaaa
Safi sana hii nimeipenda watu wengi huwa wanatema bigjii kwa karanga za kuonjeshwa
mwambie hakuna nafasi tena
 
Teh teh teh! Shemeji yako akikusikia atakumind kweli Fidel80! Spare tyre nyingine hazifai.
 
,...hehehehe...duuuh, sasa hii kufuru! njozi nyingine tamu jamani.
Huoni bibie pamoja na kukaa kote ughaibuni breki ya kwanza kwa mheshimiwa balozi?
Hilo hasa ndo linanisumbua akili. Mimi nahisi atakuwa kaambiwa tu balozi yupo na sasa hivi ana familia na anataka adhihirishe kwamba huenda yeye ni bora kuliko hiyo familia.
 
na mtu kashamwambia ana familia lakini bado tu anataka kujichomeka, wakionjwa na kuachwa wanalalama mwanaume kamtenda kumbe mengine wanajitakia.
kwa kweli wakati mwingine haya matatizo tunajitafutia. lakini huyo sidhani kama anajali kuachwa, ana uhakika kabisa akishaanzana na jamaa tu kinachofwatia atakayeachwa ni mama mwenye nyumba (poor her! (isije ikawa ndo mimi; God Forbid))
Hapo cha maana ni mkaka kuwa na msimamo, ailinde ndoa yake kama kweli anamjua Mungu.
 
Hilo hasa ndo linanisumbua akili. Mimi nahisi atakuwa kaambiwa tu balozi yupo na sasa hivi ana familia na anataka adhihirishe kwamba huenda yeye ni bora kuliko hiyo familia.

...unaona sasa? wewe mbwage tu huyo. Hakufai hata kidogo!
 
kwa kweli wakati mwingine haya matatizo tunajitafutia. lakini huyo sidhani kama anajali kuachwa, ana uhakika kabisa akishaanzana na jamaa tu kinachofwatia atakayeachwa ni mama mwenye nyumba (poor her! (isije ikawa ndo mimi; God Forbid))
Hapo cha maana ni mkaka kuwa na msimamo, ailinde ndoa yake kama kweli anamjua Mungu.


hilo ndio tatizo hapa, na mdada kashajiandaa/jipanga...na hawa wanaume zetu wakishaokota huko nje hukawii kuona mabadiliko...yaani jamani! lakini mie mpaka nimueachie mwanamke mwenzangu huyu kichwa maji wangu kweli atakuwa kapambana haswa, na nitamuachia nikijickia kumuachia...ile diziani unaona mr kama nae karidhika fulani hivi....
 
Huyo mdada hana nia nzuri nawe, na anachokitaka ni kuvunja ndoa yako tu.
kwa ushauri tu ni kwamba usimu-intertain kabisaaaaa, mwambie ukweli kuwa ulimpenda sana na sasa humpendi kabisa na una mke, na huwezi kuanzisha uhusiano na mtu ambaye humpendi. kwa vile ana namba yako ni wazi atakusumbua sana, jitahidi kwa kadiri ya uwezo wako usiwe unajibu sms zake wala usimpigie simu, kwa ninavyofahamu one way communication huwa hai-last longer.
wadada wengine bwana, hivi unajipelekaje sehemu kuwa n.k?
Thanks FP, in fact nilimueleza hayo hayo unayosema na kumsihi asinipigie simu. Anadai hawezi kunisumbua wakati niko na familia lakini mimi nimemueleza hawezi kujua wakati gani niko na familia. Muda mfupi uliopita kanipigia simu sikupokea, matokeo yake kanitumia sms tukutane "pale pa jana" nikupe zawadi zako. Sijajibu sms yake na nimefunga simu. Naanza kuhisi usumbufu fulani.
 
hilo ndio tatizo hapa, na mdada kashajiandaa/jipanga...na hawa wanaume zetu wakishaokota huko nje hukawii kuona mabadiliko...yaani jamani! lakini mie mpaka nimueachie mwanamke mwenzangu huyu kichwa maji wangu kweli atakuwa kapambana haswa, na nitamuachia nikijickia kumuachia...ile diziani unaona mr kama nae karidhika fulani hivi....

ha haaaaaaaaaaaaaaa, umenichekesha sana Nyamayao. Ni kweli unatakiwa kupigania chako. lakini mimi kasheria nilikojiwekea ni ka kupambana na mr sio na huyo wa nje ambaye hanihusu. kama mr akinihakikishia kuwa huyo ndo zaidi basi unakuwa huna la kufanya. ila sijui huyo nje huko hatasikia hata sauti yangu, hata akinifwata nyumbani kwangu
 
Pole Ambassador huyo kaja ki-Commando zaidi kuvuruga ndoa yako..Ni mharibifu hana lolote la maana
Mwambie kwa sasa ur not reachable
 
Back
Top Bottom