Aliyechora ramani ya dunia msaada

Aliyechora ramani ya dunia msaada

KIBURUDISHO

JF-Expert Member
Joined
Mar 28, 2011
Posts
1,002
Reaction score
278
Habari za asubuhi humu jamvini natumai mko poa,Nasumbuliwa na hili swali hivi aliyechora ramani ya dunia alitumia nini na teknolojia gani kuichora ramani ya dunia? Na alikuwa amesimama wapi wakati anachora ramani hiyo?
Nawasilisha swali hili mbele yenu.
 
Kujua sawasawa dunia ilivyo kulitokana na safari za uvumbuzi/utafiti (exploration) za watu kadhaa miaka ya zamani - Rejea masomo ya maarifa shule za msingi/sekondari. Mfano moja kati ya wengi alikuwa Vasco Da Gama. Pia ugunduzi wa zana kadhaa kama telescope, nk ulisaidia sana kutafiti dunia ilivyo. Utakuwa umewasikia watu kama akina Galileo. Kuchora ramani kulikofuata hakukuhitaji mtu atoke duniani.
 
Habari za asubuhi humu jamvini natumai mko poa,Nasumbuliwa na hili swali hivi aliyechora ramani ya dunia alitumia nini na teknolojia gani kuichora ramani ya dunia? Na alikuwa amesimama wapi wakati anachora ramani hiyo?
Nawasilisha swali hili mbele yenu.

Mkuu kwani we huwezi kuchora ramani ya sebule yako ukiwa ndani ya sebule?
 
Naomba kukuliza swali, unapouliza kuwa huyu aliyechora ramani ya dunia alikuwa amesimama wapi unamaanisha nini?
 
mkuu kila kitu kinaanza kidogo kidogo mpaka kinafanikiwa.

-mwanzo watu walikua wanajua dunia ni tambarare yani unatembea wee mpaka unafika mwisho wa dunia baadae wakagundua ipo duara (japo ni uwongo mababu zetu walikua wanajua)

-then watu wakaanza kuchora try and error ramani zilikua na makosa mengi

-kadri muda unavyoenda na technology inaongezeka hadi tumepata vitu kama satelite ambavyo vinatoa details sahihi
 
Habari za asubuhi humu jamvini natumai mko poa,Nasumbuliwa na hili swali hivi aliyechora ramani ya dunia alitumia nini na teknolojia gani kuichora ramani ya dunia? Na alikuwa amesimama wapi wakati anachora ramani hiyo?
Nawasilisha swali hili mbele yenu.

mulugo type
 
Zamani ilikuwa kwa kuobserve kwa macho na kuchukua vipimo manualy kama walivyosema wadau, jaribu mwenyewe kujichorea ramani ya mitaa yako, same principle ila unachukua ramani za wengi na kuziunga.

Zikaja picha za ndege, tangu miaka ya 50 kuna satelite imagery na vitu kama gps kuongeza accuracy.
 
Habari za asubuhi humu jamvini natumai mko poa,Nasumbuliwa na hili swali hivi aliyechora ramani ya dunia alitumia nini na teknolojia gani kuichora ramani ya dunia? Na alikuwa amesimama wapi wakati anachora ramani hiyo?
Nawasilisha swali hili mbele yenu.

Ramani ya dunia ilipatikana baada ya combination ya mambo mengi ikijumuisha maoni ya uncle pmwasyoke. It is illogical kusema kuwa: 'aliyechora ramani ya dunia'. Hivi kweli mtu mmoja tu angeweza vipi kuchora ramani ya dunia? Zoezi la kuchora ramani ya dunia si jambo jepesi kama vile unavyoweza kusimama ktk kichuguu na kuanza kuchora ramani .
 
Last edited by a moderator:
Ramani ya dunia ilipatikana baada ya combination ya mambo mengi ikijumuisha maoni ya uncle pmwasyoke. It is illogical kusema kuwa: 'aliyechora ramani ya dunia'. Hivi kweli mtu mmoja tu angeweza vipi kuchora ramani ya dunia? Zoezi la kuchora ramani ya dunia si jambo jepesi kama vile unavyoweza kusimama ktk kichuguu na kuanza kuchora ramani .
Kichuguu hahahaaa!:bored:
 
Last edited by a moderator:
Habari za asubuhi humu jamvini natumai mko poa,Nasumbuliwa na hili swali hivi aliyechora ramani ya dunia alitumia nini na teknolojia gani kuichora ramani ya dunia? Na alikuwa amesimama wapi wakati anachora ramani hiyo?
Nawasilisha swali hili mbele yenu.

JF imeingiliwa na vitoto vidogo vingi sana mpaka inakirihisha.
 
Naomba kukuliza swali, unapouliza kuwa huyu aliyechora ramani ya dunia alikuwa amesimama wapi unamaanisha nini?

Haki ya mama umenichekesha saana!

Yaani wewe ni mbongo halisi!!

Manake mbongo ukimuuliza swali gumu!
Kwa kukosa la kukujibu basi na yeye anakuuliza swali!
Yaani lzm upate kuchanganyikiwa kwanza!

Teh teh teh teh teh!
 
Habari za asubuhi humu jamvini natumai mko poa,Nasumbuliwa na hili swali hivi aliyechora ramani ya dunia alitumia nini na teknolojia gani kuichora ramani ya dunia? Na alikuwa amesimama wapi wakati anachora ramani hiyo?
Nawasilisha swali hili mbele yenu.
KIBURUDISHO swali lako ni muhimu saana!
Japo watu wasio jua jibu wanaleta mzaha na kejeli kwako!

Jibu ni kuwa.

Ramani ya dunia imechorwa kutoka na jitihada ya wavumbuzi mbalimbali ambao wametembea kuzunguka dunia.
Na wakusanyaji mbalimbali wa ramani za nchi tofauti na mipaka yake.
Ilichukua miaka miiingi sana kuipata ramani tulionayo leo.

Kama utarejea kwenya geographic maps za awali kabla ya ugunduzi wa kamera na upaaji wa angani! Basi ramani zile zilikuwa na ulakini mwingi! Na kasoro nyingi mno,
Na zimefanyiwa maregebisho mengi sana!

Baada ya uvumbuzi wa kamera na uwezo wa mwanadamu kupaa angani kwa kutumia vyombo mbalimbali

Hapo ndipo tulipoweza kupiga picha ya mkoa kwa mkoa. Nchi kwa nchi. Bara kwa bara.
Na hatimae kuziweka pamoja na kupata ramani tulionayo leo.

Asante kwa kuuliza

Na kama kuna lingine uliza usione aibu!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom