Aliyebuni mfumo wa namba za Magari alikosea

Aliyebuni mfumo wa namba za Magari alikosea

Unapo Fanya uchambuzi wa mfumo gani utumike (Identification Code) lazima uhakikishe vitu hivi unavizingati.

1. Mfumo wako unataka uwe na muda gani bila namba kujirudia.

2. Mfumo wako lazima ubebe taarifa , mfano nikisoma namba ya gari nipate taarifa Fulani za gari, sisi hapa utakuta rangi ndio zinatumika.

na mengine mengi.

nikianza na hill kwanza , nimeshtuka sana kuona hadi sasa tumesha anza kutumia namba za DKX XXX INA maana miaka michache ijayo itabidi tunaanze upya maana namba zitakua zote zimesha tumika.

Je aliyependekeza mfumo wa namba za magari alikua anafikiria jambo hili?
Unatoa lawama na kukosoa huku ukiwa huna taarifa sahihi za mfumo.
Ukiingiza namba kwenye system inasoma Tin,na taarifa zote za mmiliki pamoja na MV licence.
Ambao wapo kwenye mfumo wa usalama,ndio wana access ya hiyo program,huwezi kupewa wewe au ulitaka namba zikuoneshe kabisa kuwa hii ni gari ya fulani?
 
Yahani hiyo namba kwa utaalamu uliopo hadi namba ya simu ya mmiliki ipo ndani yake. Si hilo tu mtaa na taarifa muhimu za gari na mmiliki wake. Ukibisha fanya kosa uone
 
we utakuwa bado kijana mdogo,kabla ya mfumo huu kulikuwa na TZA XXXX MPAKA TZ Z XXXX hapo nyuma kulikuwa na mfumo wa TZ XXXXX,Kabla kukawa na mfumo wa mkoa namba ziliposajiliwa,huu mfumo wa sasa mpaka namba zijae kizazi hiki huenda kikawa kimeshatoweka watakaokuwepo watajua watumie mfumo gani,kama umesoma hesabu za probability utaelewa mfumo huu unahost magari mangapi?ni mengi sana so hofu ondoa
This is what they call'permutation"in staki staki'
 
Faida ya kujua hesabu,,,permutations and combinations.. Eti zitaisha tutaanza upya hahah
ADF, ZZZ plus 0,1,2,....9,
Kuisha sio kitoto
Kuna AAAA, ZZZZ Plus 0 to 9..
 
Tumia hesabu za 'Permutation and Combinations' mlizosoma A-Level na vyuoni. Hesabu ni kama ifuatavyo:

Tnnnlll ndo mfumo wa namba za gari.

nnn ni namba ambazo zinaweza zikajirudia:
  • Kama namba ya kwanza haitakuwa 0, yaan mfano 099; basi kuna namba tofauti 9 zinazoweza kutumika. Hapa tunataka kuepuka namba kama 000, 011,030 ambazo zinaweza zisiwe na maana kimahesabu na kimazoea(030=30,000=0).
  • Nafasi ya pili na ya tatu zina namba(digits) 10 tofauti zinazweza kutumika (0,1,2,3,4,5,6,7,8,9)
  • Hivyo kuna namba tofauti 9*10*10=900
lll inasimama badala ya alphabet(A-Z), hapa kuna alama(characters) 26.
  • nafasi ya kwanza inaweza kuchukuliwa na alama 26 tofauti
  • kwakuwa kurudia alama sio tatizo (mfano T234AAA) basi kuna alama 26 kwa nafasi ya pili, 26 tena kwa nafasi ya tatu
  • Hivyo kuna miundo 26*26*26 ya alama tofauti. Of course hapa unaweza ukatoa maneno yenye maana mbaya kama ASS, UKE, MBO,nk, so let say yako 100, hivyo ni 26*26*26-100
Jumla ya namba tofauti zinazoweza kugawiwa ni 900*26*26*26-100=15,818,300 (takribani milioni 16)

Nina uhakika idadi ya magari na pikipiki Tanzania haifiki hata milioni 5. Hivyo hakuna wasiwasi, na hata tukifikia hiyo namba, kuna option ya kugawa namba kikanda-hivyo ukiongeza herufi nyingine kuwakilisha kanda basi kila kanda itakuwa na namba tofauti milion 15 na laki 8.

Nyongeza:
Kila herufi mpya inapoanza kutumika (Mfano T111PAA) inakuwa na namba tofauti 9*10*10*1*26*26=608,400
 
miaka 20 ijayo haifiki tutakua tumesha maliza.
Hesabu hiyo ni rahisi ukijua yafuatayo:
  1. TRA wanaandikisha magari mangapi kwa mwaka?
  2. Kuna magari mangapi Tanzania nzima kwa sasa?
  3. Magari mangapi yanakuwa de-registered kwa sababu ya ajali, spea, nk?
  4. Umiliki wa magari unakuwa kwa asilimia ngapi?
Kwa mfumo uliopo, tunaweza tukaandikisha magari milion 15.8 (angalia post namba 106 kwa mahesabu).

Let's say kuna magari milion 5 yameshaandikishwa tayari, basi tunabakiwa na namba milioni 10.8. Kama TRA wanaandikisha wastani wa magari laki moja kwa mwaka, basi kwa mfumo wa sasa namba zitaisha baada ya miaka 10,800,000/100,000=miaka 108. Hata kama idadi ya magari inayoandikishwa kwa mwaka itaongezeka, namba zitaisha wakati mimi na wewe tumeshatangulia mbele za haki😀
 
Ili upate ni magari mangapi
10x10x9x26x26x26 = 15818400
 
Let me implement my very limited knowledge of mathematics.
The format is T 999 XXX

Tuna possibility ya kuwa na namba 100 - 999. Sijawahi kuona T 099 XXX. I stand to be corrected.
Hivyo kimahesabu tuna namba tofauti 999 - 100 = 899

X stands for alphabetic characters except O and I -> 24 letters
Out of the 24 letters, 3 can be arranged in format XXX.
Kupata the total possible number of XXX arrangement ni 24*24*24
The result: 13,824 arrangements (from AAA to ZZZ)

Kwa kila namba kati ya 100-999 tuna combinations za herufi 13,824.
Kwahiyo total number of T 999 XXX combinations ni 899 * 13,824 = 12,427,776

Hivyo basi, mfumo huu wa usajili unaweza kuhandle jumla ya vyombo 12,427,776 (Milioni kumi na mbili laki nne ishirini na saba elfu mia saba sabini na sita).

Tangu mfumo huu uanze kutumika mnamo mwaka 2005 tumekwisha exhaust combinations through T 999 DZZ (Assumption). Tujaribu kuangalia ni vyombo vingapi vimekwisha sajiliwa.

Arrangements kati ya AAA - DZZ. Hi ni A(AA-ZZ) B(AA-ZZ) C(AA-ZZ) D(AA-ZZ).
Kila (AA-ZZ) combo ina possibilities 24*24 = 576
Hivyo kwa A mpaka D ni A(552) + B(552) + C(552) + D(552) = 4 * 576 = 2,304
Jumla ya vyombo = 899 * 2304 = 2,071,296

Hivyo nasi, kuanzia T 100 AAA mpaka T 999 DZZ vyombo 2,071,296 vimekwisha sajiliwa. Mind you kuna pikipiki na bajaji zilizokuwa zinakimbiza sana namba.
Hii ina maana kuanzia T 100 EAA mpaka mwisho wa mfumo, magari 10,356,480 yanaweza kusajiliwa.

Imetuchukua miaka 12 kusajili vyombo 2,071,296. Je, tukitoa pikipiki na bajaji, itatuchukua miaka mingapi kusajili vyombo 10,356,480?? Data zaidi zinatakiwa. Kama kuna mwenye gari DAA atuambie ilisajiliwa mwaka gani tujue ni muda gani umepita.

N.B Wataalamu wa hesabu tafadhalini sahihisheni logic yangu. Jibu hili sio definitive.
UPo sahihi japo marekebisho kidogo
100 hadi 999 kuna namba 900 na siyo 899. Hivyo
9*10*10 = 900
24*24*24=13824
900*13824=12,441,600. kwa hiyo kwa huo mfumo unaweza kusajili magari 12,441,600
 
Tumia hesabu za 'Permutation and Combinations' mlizosoma A-Level na vyuoni. Hesabu ni kama ifuatavyo:

Tnnnlll ndo mfumo wa namba za gari.

nnn ni namba ambazo zinaweza zikajirudia:
  • Kama namba ya kwanza haitakuwa 0, yaan mfano 099; basi kuna namba tofauti 9 zinazoweza kutumika. Hapa tunataka kuepuka namba kama 000, 011,030 ambazo zinaweza zisiwe na maana kimahesabu na kimazoea(030=30,000=0).
  • Nafasi ya pili na ya tatu zina namba(digits) 10 tofauti zinazweza kutumika (0,1,2,3,4,5,6,7,8,9)
  • Hivyo kuna namba tofauti 9*10*10=900
lll inasimama badala ya alphabet(A-Z), hapa kuna alama(characters) 26.
  • nafasi ya kwanza inaweza kuchukuliwa na alama 26 tofauti
  • kwakuwa kurudia alama sio tatizo (mfano T234AAA) basi kuna alama 26 kwa nafasi ya pili, 26 tena kwa nafasi ya tatu
  • Hivyo kuna miundo 26*26*26 ya alama tofauti. Of course hapa unaweza ukatoa maneno yenye maana mbaya kama ASS, UKE, MBO,nk, so let say yako 100, hivyo ni 26*26*26-100
Jumla ya namba tofauti zinazoweza kugawiwa ni 900*26*26*26-100=15,818,300 (takribani milioni 16)

Nina uhakika idadi ya magari na pikipiki Tanzania haifiki hata milioni 5. Hivyo hakuna wasiwasi, na hata tukifikia hiyo namba, kuna option ya kugawa namba kikanda-hivyo ukiongeza herufi nyingine kuwakilisha kanda basi kila kanda itakuwa na namba tofauti milion 15 na laki 8.

Nyongeza:
Kila herufi mpya inapoanza kutumika (Mfano T111PAA) inakuwa na namba tofauti 9*10*10*1*26*26=608,400
Tatizo wengi walikimbia hisabati na kwenda kusomea ubishi. Mambo ya permutation, combinations and intergrations wala hawatakuelewa.
 
Let me implement my very limited knowledge of mathematics.
The format is T 999 XXX

Tuna possibility ya kuwa na namba 100 - 999. Sijawahi kuona T 099 XXX. I stand to be corrected.
Hivyo kimahesabu tuna namba tofauti 999 - 100 = 899

X stands for alphabetic characters except O and I -> 24 letters
Out of the 24 letters, 3 can be arranged in format XXX.
Kupata the total possible number of XXX arrangement ni 24*24*24
The result: 13,824 arrangements (from AAA to ZZZ)

Kwa kila namba kati ya 100-999 tuna combinations za herufi 13,824.
Kwahiyo total number of T 999 XXX combinations ni 899 * 13,824 = 12,427,776

Hivyo basi, mfumo huu wa usajili unaweza kuhandle jumla ya vyombo 12,427,776 (Milioni kumi na mbili laki nne ishirini na saba elfu mia saba sabini na sita).

Tangu mfumo huu uanze kutumika mnamo mwaka 2005 tumekwisha exhaust combinations through T 999 DZZ (Assumption). Tujaribu kuangalia ni vyombo vingapi vimekwisha sajiliwa.

Arrangements kati ya AAA - DZZ. Hi ni A(AA-ZZ) B(AA-ZZ) C(AA-ZZ) D(AA-ZZ).
Kila (AA-ZZ) combo ina possibilities 24*24 = 576
Hivyo kwa A mpaka D ni A(552) + B(552) + C(552) + D(552) = 4 * 576 = 2,304
Jumla ya vyombo = 899 * 2304 = 2,071,296

Hivyo nasi, kuanzia T 100 AAA mpaka T 999 DZZ vyombo 2,071,296 vimekwisha sajiliwa. Mind you kuna pikipiki na bajaji zilizokuwa zinakimbiza sana namba.
Hii ina maana kuanzia T 100 EAA mpaka mwisho wa mfumo, magari 10,356,480 yanaweza kusajiliwa.

Imetuchukua miaka 12 kusajili vyombo 2,071,296. Je, tukitoa pikipiki na bajaji, itatuchukua miaka mingapi kusajili vyombo 10,356,480?? Data zaidi zinatakiwa. Kama kuna mwenye gari DAA atuambie ilisajiliwa mwaka gani tujue ni muda gani umepita.

N.B Wataalamu wa hesabu tafadhalini sahihisheni logic yangu. Jibu hili sio definitive.
nimependa ulivyoelezea..
 
Mpaka mwaka 2015, Tanzania ilikuwa na magari 1.5 milioni tu yaliyoandikishwa na TRA(source:GHO | By category | Registered vehicles - Data by country), kwahiyo mpaka tumalize namba milioni 15.8 sio leo wala kesho, wastani wa magari mapya kwa mwezi ni chini ya 10,000. Hivyo waweza sema tunaandikisha wastani wa magari mapya laki moja kwa mwaka. Kwa mujibu wa post zangu za awali, mfumo huu waweza kutumika kwa miaka zaidi ya 100.
 
Ndio kahisabati kadooooogo kalikomshinda. Sasa ukimfafanulia 999 mpaka ZZZ ndio kichwa chake kitaamka.
Tatizo unafikiri bila fact, pia hamzingatii na mabadiliko mengine ya kiuchumi etc. Naona unatumia vyema hesabu zako .
 
Tukifika T999 ZZZ
Tunanza AAA 111T
Pia mpaka tufike huko, kuna magari mengine yatakuwa yamefutiwa usajiri kutokana na uchakavu na siku nyingi yamefanywa spare na mengine yameuzwa kama chuma chakavu kwenye viwanda vya nondo hivyo wengine wakinunua gari unashanga unapewa T...AAD
 
Tatizo unafikiri bila fact, pia hamzingatii na mabadiliko mengine ya kiuchumi etc. Naona unatumia vyema hesabu zako .
Shida yako wewe unafikiri kwa unachokidhania kuwa ni facts, lakini hutuelezi hapa, badala yake unaleta HISIA facts unaziacha moyoni. Ni wapi umeeleza au kufafanua ni jinsi gani mfumo utafeli zaidi ya kuongea pumba?

Kuna mabadiliko gani ya kiuchumi ambayo yatatufanya tuwe na magari (899 x AAA, ABA, ABB, ABC, ABD, ...ZZZ) kwa muda mfupi kiasi tuone mfumo ni mbaya? Ukitaka kujua umeongea pumba, kagua thread yako ina likes ngapi...pengine watu hawaelewi madai yako.
 
Unapo Fanya uchambuzi wa mfumo gani utumike (Identification Code) lazima uhakikishe vitu hivi unavizingati.

1. Mfumo wako unataka uwe na muda gani bila namba kujirudia.

2. Mfumo wako lazima ubebe taarifa , mfano nikisoma namba ya gari nipate taarifa Fulani za gari, sisi hapa utakuta rangi ndio zinatumika.

na mengine mengi.

nikianza na hill kwanza , nimeshtuka sana kuona hadi sasa tumesha anza kutumia namba za DKX XXX INA maana miaka michache ijayo itabidi tunaanze upya maana namba zitakua zote zimesha tumika.

Je aliyependekeza mfumo wa namba za magari alikua anafikiria jambo hili?

Haziishi, fikiri mpaka zifike ZZZ ni leo? Halafu baada ya ZZZ unaweza anza T1 AAA xxx mpaka umalize ni lini.
 
Haziishi, fikiri mpaka zifike zzz ni leo? Halafu baada ya ZZZ unaweza anza TZ1 AAA xxx mpaka umalize ni lini.
Au unaweza ukapata tena la AAG maana kwa usawa kuna baadhi ya magari yatakuwa yamechoka yapo juu ya mawe na wamilki wengi wataenda TRA kusimamisha registration maana kwa sheria ya TRA hata kama gari uliuza chuma chakavu kama hujaenda kulifuta kwenye data base linahesabiwa
 
Back
Top Bottom