Alichokifanya Mwalimu Nyerere Mwaka 1995 mbele ya Macho yangu

maishapopote

JF-Expert Member
May 28, 2009
3,277
5,514
Nikiwa Darasa la Saba Mwaka 1995, kama kijana yoyote wa Moshi Mjini Nilikua na Hamasa Kubwa Kisiasa, Na Moshi Mjini Ilikua Imewaka Moto Kisiasa.

Bwana Mrema Alikua Amejiunga na NCCR Mageuzi, Nayo NCCR ikaunganisha Nguvu Na CHADEMA Wakaweka mgombea Ubunge Bwana MTUI...na Urais Akawa Bwana Lyatonga Mrema..Kampeni Zikapamba Moto.

Timu ya Mrema ikapita kuomba Kura Uwanja wa Mashujaa Moshi ukajaa na kutapika..mimi nimo mbele kabisa Huku Mrema,Pale Makongoro Nyerere.

Wakatuelekeza kwa unyenyekevu kabisa Kwamba Wiki Ijayo Baba wa Taifa Na Mgombea wake Bwana Mkapa watakuja kwahiyo Fanyeni Hivi Na Hivi..Hao wakaondoka zao wakaenda Arusha.

Baada Ya wiki Kweli Mzee wetu Baba wa Taifa akaingia Moshi,Niliwahi Uwanjani Tokea saa Tano, Kumbe Hakuja Na Mzee Mkapa Bwana, Akaanza Hotuba na vile vichekesho vyake

Mwisho Akainua Picha ya Mkapa Nakumbuka ile picha ni ya kuchora akasema Nawaomba Mumpe kura huyu kwa Maendeleo ya nchi Yetu...

Uwanja Wote wa Mashujaa Ukanyamaza kimya Kabisa,kimya halafu wakainua vidole viwili ile Alama inayotumiwa na CHADEMA uwanja wote ukawa unapunga huku watu wamenyamaza kimya kabisa..

Mwalimu Akiwa amefura kwa hasira,akatamka nikiwa namuona na kumsikia. MTAKE, MSITAKE HUYU ATAKUA RAIS halafu akatupa ile picha chini...akaitupa kabisa halafu akashuka jukwaani Akaenda zake mkutano ukafia hapo.

Ilasikuwahi kumuona Tena Live Mwalimu Hadi Alipokufa nikiwa Form Four mwaka 1999...ila nilikua namfatilia sana hotuba zake

Tutamsema Vibaya Lakini Hakuna wa Kuvaa Viatu Vyake na Hatatokea Alikua Baba, kiongozi, mkombozi, mwalimu, mwanafalsafa, mpenda kusali, na mengine mengi. Namkumbuka na Atakumbukwa na Taifa Hili kwa Miaka Yote Hadi Ukamilifu wa Dahari...Siku Mwenye Mali Yake Atakapopenda na kusema Mwisho ndio Huu..

MP...JF LEGEND
.
 
Ahsante mleta Uzi kwa kutupa sura nyingine ya mwalimu. Kumbe ndo aliwafundisha CCM kuiba kura. Ndipo Nape akaja na bao la mkono,Bashiru akaja na dola kutumiwa kubaki .madarakani na mama mwinigine namsahau jina na bahati mbaya ni marehemu kwa sasa yeye alienda mbali zaidi akasema ushindi kwa CCM haina Mungu akipenda Mana kwao Mungu apende hasipende ushindi kwao no lazima. CCM ni walewale.
 
Hii habari haiendani na aiba ya Mwalimu

Akafura, na Akatupa Picha Chini...,
Moja akatupa picha chini ili iweje ?,

Mbili haikuwa ajabu watu kutoka uwanjani wala kukataa na kumpinga Mwalimu kuhusu Mkapa; watu hawakumjua Mkapa, watu walimkubali Mrema na kila kiwanja alichoenda Mwalimu watu walikuwa wanapinga..., Sasa kwa kufura ghafla na kushangaa ingekuwa ni mtu aliyeshangazwa na kilichotokea wakati nina uhakika alikitegemea kilichotokea...., ila hakukata tamaa aliendelea kutembea nchi nzima na kupata upinzani mkubwa... (Mkapa alikuwa habebeki)
 
Kama tulivyo binadam hatuwezi kuwa wakamilifu 100%

Ila ukimfuatilia sana huyu babu yetu, kias flan alikuwa na sifa flan ambayo vijana wa mtaani wanaita MKUDA! Kalikuwa kakuda kakuda Sana tu. Na Kama angetawala mpaka kwenye tekinolojia ya Sasa hv ahaaaa kangetunyosha haswaaaaaaa
 
Sasa huyo mkuu anawasiwas wa hii story, weee utudanganye upate faida gan kwa mfano ? Ikizingatiwa hatukujui!!!
 
Hata mimi aise...NCCR mageuzi na alama ya CHADEMA wapi na wapi?
By then CHADEMA ya akina Kasanga Tumbo na ofisi yao pale Magomeni, haikuwa hata mashuhuri...
Mkuu mtu wa kutusaidia hapa ni pascal huyohuyo...naamini ana fact na ana connection..kwa mtu aliyekua moshi ataelewa ninachokisema..CHADEMA Na NCCR viliungana kwenye urais wakawa wanamuunga mkono mrema aliekua NCCR na Ubunge Moshi mjini kila mtu aliweka wake Mtui alieshinda alikua NCCR Na CHADEMA wakamuweka mzee ndesamburo, mtui alishinda kutokana na Nguvu ya Mrema ila alikaa kipindi kimoja tu,Then ndesamburo akafuatia hadi alipoachia mwenyewe
 
Back
Top Bottom