Albert Msando afunguka kuhusu Zitto Kabwe

Albert Msando afunguka kuhusu Zitto Kabwe

Which came first the escrow scandal or Zitto's removal from the party?. I think Mr. Msando is trying to insinuate indirectly the negative involvement of Chadema in the scandal, which I find to be very pathetic.

huyu Msando ni mburula. kwanza Escrow ilianzia Mwananchi then Kafulila akaipeleka bungeni. Zitto aliingia kwa vile ni mwenyekiti PAC na ikumbukwe hata Filikunjombe alifanya kazi kubwa PAC.
kusema Zitto ndo anaisimamia escrow scandal ni ujuha. bora mimi wa MEMKWA kuliko huyu Msando.
wafatane ACT wakawachukue na wake wakina Shonza.
 
mimi Nadhani msando Anajidhalilisha tu...Hivyi kweli mwanasheria unaweza kuuliza maswali ya kipuuuzi hivyo?

Mwambieni ataficha wapi uso wake huku anajiiita mwanasheria msomi?

Huo ndio usomi?

Msando ni kichwa nazi kweli yani....
 
Chadema imeinuka kipindi cha huyo huyo zitto na Slaa kipind yuko bungeni.......hili linaonekana dogo ila litawacost sana me binafsi nilikuwa naikubali sana Chadema hata kwa usaliti wanaosema ameufanya sidhani kama kilichofanyika kitakijenga chama ukilinganisha kama wangeendelea kumuacha huku akiwa katika uangalizi wa kila mipango anayoendelea kuifanya....
Hapa kinachoonekana ni mgongano wa maslahi wasituambie chochote.
Kuna tatizo na hili kama watanzania wako makini inabidi liwe funzo kubwa. Watanzania wanahitaji chama mbadala cha kuwaletea matumaini. Na Mara nyingi pa kukimbilia huwa ni chadema Kwa Kuwa ndo tu chama kikubwa. Watanzania hatuna utamaduni wa kusoma kwani hata katiba yetu mama hatuijui. La hili linatakiwa liwe fundisho kwani wanasiasa ni watu hatari sana duniani kote. Tunahitaji tuzibebe katiba zote tuzisome ili tuzielewe. Chadema imeonyesha kwa namna mbali mbali Kuwa katiba yake imebakwa na viongozi wachache. Basi inaniaminisha Kuwa kwa kuwa sisi si wasomaji kuna kila uwezekano wa Kuwa na vipengele vya kuwaandaa akina Mugabe wa Tanzania kwani wanachama wameshajengewa utamaduni wa ndio mzee. Viongozi hawasemwi na hawaguswi na yeyote. CCM imetutawala na katiba yake tunaijua ila imechafuliwa na viongozi wake. Ni dhahri haina hizo chembe za ukandamizaji. Basi nawashauri watanzania wenzangu tuamke tuzisome katiba za vyama vyetu. Mpaka hapa nashindwa kuamini kwa dunia Ya leo kama kuna chama kinaweza Kuwa na katiba inayokandamiza utafutwaji wa haki. Na tumeshuhudia katiba ikibadirishwa kinyemela ,kwa Kuwa watanzania hawako serious wa nashindwa kupata message inayotumwa na hao wanaotaka utawala.na hii inatakiwa Kuwa message tosha kwani leo wanakandamizwa wanachama kesho utakuwa umma wote wa watanzania.
 
Mwanasheria ambaye pia ni diwani kupitia CHADEMA, Ndugu Albert Msando amehoji yafuatayo;

1. Amehoji je, kama
CHADEMA kinasema ni Cha Kidemokrasia kwanini kinaaamuru Afukuzwe tu kwa kuwa ameenda mahakamani?

2. Amehoji je, ni nani mwenye mandate ya kumvua mwanachama uanachama wake.

3. Je, uamuzi wa kumvua uanachama ulipaswa kutangulia kwa umma au kwa Zitto kwanza?

4. Amehoji je, imekuwaje mtu anayesimamia sakata la Escrow afukuzwe kwa sasa?

5. Amesema pia kuwa Zitto hana haja ya kubaki
CHADEMA kwa kuwa hata akiomba kubaki haitakuwa na mashiko. Pia ameuliza itakuwaje akae meza moja na Tundu Lissu,Wakati Tundu Lissu anatangaza amesema walishamfukuza toka mwaka jana. Naye anaona kuwa Zitto hahitajiki CHADEMA.

6. Pia amesema lengo la kumfukuza Zitto limefanywa kinafiki tu.

7. Amesema kuwa haoni haja ya kulazimisha kila mtu awaze kama Tundu Lissu au Mbowe au Slaa.

9. Pia amesema kuwa mgogoro huu ni funzo kwa Zitto, Wanachadema na Watanzania kujua aina ya viongozi walionao.Pia amesema kuwa migogoro hii isitumike kujenga chuki.

Chanzo: Clouds TV

Huyu si mwanasheria. Angekuwa mwandishi wa habari angeitwa kanjanja. Huyu ni msakatonge tu.
 
Kupeleka Chama kwa court ni direct termination.

Zitto simama uesabiwe na ACT yako.
 
Huyu Msando yupo CDM au NCCR ? Kama yupo CDM nayeye anaubiri nini kusepa ?!
 
Ninavyomjua Zitto anaweza akawapiga U-turn hata ACT mkashangaa anaingia TLP au NRA...Ngoja muone siku atakapoamua...Ila kwa upande wangu naomba Spika Makinda asikubaliane na CDM amwache mpaka bunge litakapovunjwa July, maana jamaa bado anamajukumu makubwa ya kumalizia eg Escrow, TPA, Pesa zilizoko Uswis etc
Tutammis sana kwenye Bunge lijalo, au ikiwezekana awe mbunge wa kuteuliwa kama Mbatia..maana jamaa bado tunamhitaji sana kwenye siasa za Tanzania ya leo.

Majukumu yatamaliziwa na kamati, maana bado kuna jembe la ccm Filikunjombe litachukua jukumu la kuiongoza kamati! Tuache kumvimbisha kichwa huyu mburula! Kavurunda mwenyewe, aende zake huko! Hili linarudisha nyuma sana harakati za vijana kuweza kuaminiwa!!
 
Nakuunga mkono kuwa Zito atakumbukwa na CHADEMA na hata Watanzania walio wengi. Atakumbukwa jinsi alivyosaliti harakati za Watanzania kutaka kujikomboa kutoka kwa ugandamizaji na wizi unaofanyika chini ya mwavuli baradhuli CCM.

CHADEMA watamkumbuka sana ZITTO.
 
Nyinyi mbona vipengele vya katiba mnachagua? Alichokikanyaga mbowe mbona hakuna mwenye guts za kusimama na kumsema? au mnachagua nani wa kubanwa na katiba,acheni unafiki kama ni katiba basi imbane kila anayeivunja.

What did Mbowe do on his own? Unataka kuwaaminisha watu kuwa Mbowe alibadilisha vipengele vya katiba akiwa peke yake? This is ridiculous. Where was this Zitto Kabwe by then? Mtu ambaye kweli anampenda Zitto amshauri kuwa hata huko ACT bado chama kitakuwa juu kuliko yeye. Kwa hiyo hata kama yeye ni mwanzilishi akiwaletea usaliti watamfukuza.
 
Kuna tatizo na hili kama watanzania wako makini inabidi liwe funzo kubwa. Watanzania wanahitaji chama mbadala cha kuwaletea matumaini. Na Mara nyingi pa kukimbilia huwa ni chadema Kwa Kuwa ndo tu chama kikubwa. Watanzania hatuna utamaduni wa kusoma kwani hata katiba yetu mama hatuijui. La hili linatakiwa liwe fundisho kwani wanasiasa ni watu hatari sana duniani kote. Tunahitaji tuzibebe katiba zote tuzisome ili tuzielewe. Chadema imeonyesha kwa namna mbali mbali Kuwa katiba yake imebakwa na viongozi wachache. Basi inaniaminisha Kuwa kwa kuwa sisi si wasomaji kuna kila uwezekano wa Kuwa na vipengele vya kuwaandaa akina Mugabe wa Tanzania kwani wanachama wameshajengewa utamaduni wa ndio mzee. Viongozi hawasemwi na hawaguswi na yeyote. CCM imetutawala na katiba yake tunaijua ila imechafuliwa na viongozi wake. Ni dhahri haina hizo chembe za ukandamizaji. Basi nawashauri watanzania wenzangu tuamke tuzisome katiba za vyama vyetu. Mpaka hapa nashindwa kuamini kwa dunia Ya leo kama kuna chama kinaweza Kuwa na katiba inayokandamiza utafutwaji wa haki. Na tumeshuhudia katiba ikibadirishwa kinyemela ,kwa Kuwa watanzania hawako serious wa nashindwa kupata message inayotumwa na hao wanaotaka utawala.na hii inatakiwa Kuwa message tosha kwani leo wanakandamizwa wanachama kesho utakuwa umma wote wa watanzania.


Nawewe kweli unatia aibu kwa maelezo yako.Unasema kwanini katiba haitumiki kwa viongozi,huyu Zitto alikuwa ninani kama hakuwa kiongozi?.Mbona ilivyofanya kazi kwa madiwani sehemu kubwa nchini kuwafukuza haukuleta povu?.Tumia akili ndugu
 
Swali la mdingi, nani mwenye mandate ya kumfukuza ZITTO?

Kabla hujajiuliza swali LA kijinga namna hii ambalo we we unaliita LA msingi. Ulipaswa kujua ni mandate IPI ilompa uhalali zitto kujiunga chadema . ukiipata kojoa ukalale.
 
Ni diwani na mwanasheria wa aina gani ambae hajui hata Katiba ya Chama chake inasemaje?? Hii ni aibu kuwa na wanasheria wa aina hiyo.Msando kwa haya maswali haya inaonyesha alivyo mnafiki. Naamini kama kweli Msando ni mwanaaheria alimua kula hela Aza Zitto.
 
Kuna structure katika chama Zitto alitakiwa kuzifata hili kudai haki yake.Kama alikuwa haziamini kwa nini aliendelea kuwa mwanachama wa Chadema.Ndo maana ata kwenye Katiba za vyama vya mchezo kama mpira,mtu akakimbilia mahakamani kuna adhabu Kali ya kufungiwa kutojihusisha na mchezo husika.Kwani katiba zao zimehainisha procedure za kufuata once hujaridhika na kitu na sio mahakamani.The same applies to Chadema.[/QUOTE
haaaaaa haaaa unajaribu kumlinganisha football association na political party???? Unalinganisha impact Ya political party na vyama vya michezo. Basi hamjakomaa kujua demokrasia ni nini na impact Ya political party kwa jamii. Na kama bado mnajilinganisha na vyama vya michezo mkajipange upya tutang'ang'ana na mafisadi Hadi kieleweke.
 
Ninavyomjua Zitto anaweza akawapiga U-turn hata ACT mkashangaa anaingia TLP au NRA...Ngoja muone siku atakapoamua...Ila kwa upande wangu naomba Spika Makinda asikubaliane na CDM amwache mpaka bunge litakapovunjwa July, maana jamaa bado anamajukumu makubwa ya kumalizia eg Escrow, TPA, Pesa zilizoko Uswis etc
Tutammis sana kwenye Bunge lijalo, au ikiwezekana awe mbunge wa kuteuliwa kama Mbatia..maana jamaa bado tunamhitaji sana kwenye siasa za Tanzania ya leo.

Makinda hapaswi kuvunja kanuni. Zitto hana alilobakisha kufanya kama Zito, zile ni kazi za kamati na zitaendelea tuu. Kwani Mungu akitaka kumchukua mtampinga eti kuna bla bla za Uswiss hajamaliza? Mbona Mungu anaruhusu ndoa na kabla mume hajamzalisha mkewe anamchukua? Aende tuu, heshima kwa wenzio ni kitu muhimu sana.
 
Habari ikitoka clouds najua itakuwa imefagilia ccm, moja kwa maja au kiaina flani
 
Back
Top Bottom