Albert Msando afunguka kuhusu Zitto Kabwe

Albert Msando afunguka kuhusu Zitto Kabwe

Pole saana Mh. Zitto Zuberi Kabwe na hongera kwa CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO. Kwani kwenye mpambano wa aina yeyote lazima kuwapo na mshindi na mshindwa. Binafsi sina uhakika kwa kinachoenedelea kuwa kinatokana na watu wenye dhamira moja ama ni dhamira tofauti zenye maslahi binafsi?
Napata wakati mgumu saana pale ambapo chama kinachosisitiza demokrasia kuwa na sheria ya kumtimua mwanachama wake yeyote atakayekwenda kupeleka mashtaka ya aina yeyote mahakamani dhidi ya chama hicho na akashindwa. Mh. Zitto aliona kwamba hatendewi haki na chama chake Je angekimbilia wapi kama sio kwa Mtafsiri wa sheria? Nafikiri chadema kama chama cha demokrasia basi hapa hakina budi kufanya mabadiliko ili kuwa mfano hai kwani tumeshuhudia katka nchi za jirani zetu wale wote waliokuwa hawakutendewa haki ndani ya taasisi za ndani za serikali wamekuwa wakikimbiza mashtaka yao UGHAIBUNI.
Kihistoria kuna habari ya kwamba ndani ya chadema kulikuwa na mgogoro wa kimaslahi kati ya Mh Zitto zuberi kabwe na viongozi waandamizi wa chama hicho, baadae shutma zikarudi kwa Mh. Zitto kushirikiana na CCM pamoja na taasisi za juu za serikali katika kudhoofisha hali ya upinzani hasa Bungeni. Sina hakika na shutuma za Chadema kwa kuwa uwezo wa Mh. Zito Kabwe wa kujenga hoja juu ya kuikosoa serikali ulishuhudiwa na watanzania wote. Na kuhusu mgongano wa maslahi, kwa kumbukumbu zangu ni kwamba si wa kwanza Mh. Zitto kutamka hayo bali kuna waliotangulia ambao walijaribu kutoa hoja za Kukijenga chama imara CHADEMA kwa kupingana na maslahi na matakwa ya viongozi waandamizi lakini waliishia umauti.
Naomba niseme kwamba kwa hayo yote yaliyokuwa yanaendelea ndani ya chadema ni dhahiri kwamba nchi hii bado haina upinzani wa kweli wenye dhamira ya kumkomboa Mtanzania bali una upinzani wa kichama wenye maslahi na chama..Nomba nikitakie safari njema CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO na pia namuomba mungu amuongoze Mh Zitto Zuberi Kabwe katika jitihada zake za kumpigania Mtanzania, nina imani bado wananchi wa kigoma na watanzania wote tuna imani na Mh. Zitto Zuberi Kabwe katika harakati za kumkomboa mtanzania.

Mkuu hakika umesema ukweli mtupu.
 
Katiba ya Chadema kiboko. Kwa mbowe na Lema inawekwa kando. Kwa Zitto inatumika
 
Mungu ni waajabu sana ametua IQ tofauti za kuelewa ila ina maana yake
 
Hiki kipengele kimekaa kidikteta sana.Hii katiba haina tofauti na katiba pendekezwa ya CCM,inayotaka raisi asishitakiwe hata akitoka madarakani.


Katiba ni makubaliano/maridhiano/jinsi ya kujiongoza au kujisimamaia katika utekelezaji wa mambo flani mtakayokuwa mmekubaliana kufuatwa na kila mmoja wenu.Katiba ya Chadema haikufanyika na mtu mmoja ,kama yapo makosa katika baadhi ya vifungu vyake yatawasilishwa kwa mujibu wa utaratibu lakini kwa sasa kifungu kinasema hivyo.

Tafadhali sana usiifananishe katiba ya Chadema na hii (rasimu ya ccm)kama ulivyoainisha kwa sababu zote kwa macho ya nje ni katiba lakini nyengine haikufuata utaratibu uliokusudiwa.
 
Ninavyomjua Zitto anaweza akawapiga U-turn hata ACT mkashangaa anaingia TLP au NRA...Ngoja muone siku atakapoamua...Ila kwa upande wangu naomba Spika Makinda asikubaliane na CDM amwache mpaka bunge litakapovunjwa July, maana jamaa bado anamajukumu makubwa ya kumalizia eg Escrow, TPA, Pesa zilizoko Uswis etc
Tutammis sana kwenye Bunge lijalo, au ikiwezekana awe mbunge wa kuteuliwa kama Mbatia..maana jamaa bado tunamhitaji sana kwenye siasa za Tanzania ya leo.

Kwa sheria za bunge mbunge akishavuliwa uanachama anapoteza mandate ya kuwa mbunge mara moja, kwa kuwa alipata ubunge kwa tiketi ya chama.
 
Kwa kuweka kumbukumbu vizuri kwa wasiojua ,suala la katiba za vyama vya siasa kisheria zinatakiwa kuhakikiwa na ofisi ya msajili wa vyama vya siasa ili kuangalia kama kipo au vipo vifungu vya katiba(chama husika)vitakavyopingana au kwenda kinyume na katiba ya nchi hii ya Tanzania.

Katiba ya chama cha Demokrasia na maendeleo ni sahihi na ipo kihalali kisheria kwa sababu ilishapitishwa katika hatua hizo kuihalalisha.


....com.

Kwa hiyo katiba ya chadema inatumika kwa zitto tu, kwa Mbowe haitumiki
 
akili yako ni pana sana, ni wachache sana wanaweza kuelewa kama ww, huwezi jiita mwanademocrasia wakati katiba yako inaziba watu midomo wasipige kelele unapowakanyaga.

Kweli kabisa mkuu,kama demokrasia ipo kuna haja gani ya kuzibana midomo?.
 
Chadema hawaipendi mahakama,hawaamini katika HAKI (Mahakama) na kama mwanachama ataenda mahakamani basi atafukuzwa.Halafu wanakiita chama cha demokrasia.Lakini utashangaa viongozi wake kama Dr Slaa wakizusha uongo na ukihoji uhalali wake wanakuambia "NENDA MAHAKAMANI" Inahitaji ulimbukeni na akili ya mwendawazimu kuwaelewa hawa jamaa.
 
Which came first the escrow scandal or Zitto's removal from the party?. I think Mr. Msando is trying to insinuate indirectly the negative involvement of Chadema in the scandal, which I find to be very pathetic.
 
Kuna structure katika chama Zitto alitakiwa kuzifata hili kudai haki yake.Kama alikuwa haziamini kwa nini aliendelea kuwa mwanachama wa Chadema.Ndo maana ata kwenye Katiba za vyama vya mchezo kama mpira,mtu akakimbilia mahakamani kuna adhabu Kali ya kufungiwa kutojihusisha na mchezo husika.Kwani katiba zao zimehainisha procedure za kufuata once hujaridhika na kitu na sio mahakamani.The same applies to Chadema.
 
Hiki kipengele kimekaa kidikteta sana.Hii katiba haina tofauti na katiba pendekezwa ya CCM,inayotaka raisi asishitakiwe hata akitoka madarakani.

Nakuunga mkono

Ni kipengele kinacho mnyima mwana CHADEMA haki yake ya msingi ya kukimbilia Mahakamani

Ni kipengele cha "kishetani"
 
Katiba ya Chadema kiboko. Kwa mbowe na Lema inawekwa kando. Kwa Zitto inatumika

Hivi katiba ya CCM ndo inasema ukijua kutukana na ukiwa fisadi unapandishwa cheo eti! basi chadema hakuna aliye juu ya katiba mchukueni huko kama amewauma na mnamuina kuwa ni jembe.
 
ni kwa kiasi gani katiba ya chadema imefuatwa kwenye kila maamuzi ya utendaji ndani ya chama?

Nadhani hilo ndilo lilikuwa swali liliohitaji mahakama iamue, na mahakama imeamua kulitupilia mbali na kuruhusu CHADEMA waendelee kupiga rungu msaliti
 
Mbona hoja zake ni kama za kisiasa vile, wakati nilitegemea za kisheria? Ni wakili au msemaji wa ZZK?
 
Madai ya msingi ya Zitto ni kupatiwa muktasari wa kikao kilichomvua nyadhifa zake ndani ya chama, na wakati anasubiria muktasari huo ili ajipange kukata rufaa aliomba mahakama itoe zuio kwa chama kujadili uanachama wake mpaka pale atakapokata rufaa kupinga kuvuliwa nyadhifa zake. Kwa kuwa kupewa muktasari wa kikao ni haki ya msingi ya Zitto, kwa kuwa kukata rufaa ndani ya chama cha kidemokrasia ni haki ya msingi ya mwanachama, na kwa kuwa huwezi kukata rufaa au kulalamikia uamuzi mpaka pale ukatapoelezwa tuhuma rasmi kupitia muktasari. Hapa ndipo kwenye swali la msingi: Kwanini chama hakitaki kumpa huo muktasari wa kikao ambao unaeleza tuhuma zake kinagaubaga? Nini dhumuni la kutompa huo muktasari? Je chama cha kidemokrasia kinahitaji kweli mwananchama wake kwenda mahakamani kuomba muktasari wa kikao cha kikatiba ndani ya chama?
 
Mwanasheria feki huyu. Mh tundu ametoa kwenye katiba ya CHADEMA hakutunga yeye yakwambaaa mwana CHADEMA yeyote atakae shitaki mahakaman moja kwa moja atakua amejivua uanachama so huyu mwanasheria Alienda shule kafanya nn? Da!

Yaani zaid ya ufake mkuu!!
 
Huyo mwanasheria mbona ana akili ndogo sana??

Ndio shida ya wanasheria njaa , kakurupuka na ujinga wake huko katoa point za kijinga hapo na maswali ya kijinga ambayo hayana maana yoyote!!
 
Back
Top Bottom